Sunday, March 2, 2014

Uefa yampiga marufuku Pellegrini

 
Kocha wa Manchester City Manuel Pellegrini
Kocha wa Manchester City Manuel Pellegrini amepigwa marufuku mechi mbili na UEFA asisogelee eneo la kiufundi la uwanja kwa kumlaumu mwaamuzi baada ya klabu yake kushindwa na Barcelona katika michuano ya klabu bingwa ya Ulaya.
Pellegrini alisema baada ya timu yake kushindwa 2-0 nyumbani kwamba mwaamuzi kutoka Sweden Jonas Eriksson "hakua mwaadilifu kwa timu zote mbili".
Alituhumiwa kwa ukosefu wa nidhamu na amepewa adhabu ya kukaa jukwaani pamoja na mashabiki katika mkondo wa pili wa mchuano na Barcelona mnamo Machi 12 March, poja na Mechi nyingine za ziada.
Adhabu ya mechi moja nyingine imesimamishwa kwa miaka miwili.

No comments:

Post a Comment