Monday, September 30, 2013

SERIKALI YASUTWA KWA KUYAFUNGIA MAGAZETI YA MWANANCHI NA MTANZANIA....YADAIWA KIKWETE KAZIDIWA NGUVU

SIKU mbili baada ya serikali kutumia sheria ya magazeti ya mwaka 1976 inayolalamikiwa na wadau wa sekta ya habari kuyafungia magazeti mawili ya kila siku ya Mwananchi na Mtanzania, wadau mbalimbali wamejitokeza na kuipinga adhabu hiyo.
  
Sheria hiyo inampa ruhusa waziri mwenye dhamana ya habari kupiga marufuku uchapaji na matumizi ya gazeti lolote ambalo anafikiri liko kinyume na maslahi ya umma.
  
Katika adhabu hiyo, gazeti la Mtanzania limefungiwa kwa siku 90 huku Mwananchi likifungiwa kwa siku 14, adhabu mbazo zimeanza Septemba 27, mwaka huu, yakidaiwa kuchochea.
  
Wakizungumzia adhabu hizo, wadau hao, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA), mhadhiri mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Azavel Lwaitama, Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA) na mwandishi nguli, Ndimara Tegambwage walidai kuwa serikali imeendelea kutumia sheria mbovu kubana uhuru wa habari nchini.

Zitto: JK amezidiwa
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Zitto alisema kuwa serikali imechukua uamuzi huo kwa kutumia sheria ya kidikteta ya magazeti ya mwaka 1976, ambayo Tume ya Jaji Francis Nyalali iliiorodhesha kama sheria kandamizi.

Alisema kuwa sababu zilizotolewa kuhalalisha uamuzi huu hazina maana, na kwamba serikali ingeweza kufungua mashitaka ya kawaida mahakamani kushitaki magazeti hayo iwapo haikupendezwa na habari walizochapisha.

“Moja ya sababu ya kufungiwa kwa gazeti la Mwananchi ni kuchapisha taarifa kuhusu mishahara ya serikali. Serikali inasema habari hii ni siri.
  
“Serikali hii hii ambayo imesaini makubaliano ya kuendesha serikali kwa uwazi (Open Government Initiative) na kumwagiwa sifa na Rais Barack Obama wa Marekani, inalifungia gazeti kwa kuandika habari za mishahara ya watumishi wa serikali,” alisema.
  
Zitto aliongeza kuwa mishahara kuanzia wa rais hadi mtendaji wa kijiji haipaswi kuwa jambo la siri.
  
“Kwamba kuonyesha kuwa jambo hili linapaswa kuwa wazi, mkutano ujao wa Bunge tutatafuta kila namna kutaja mshahara wa rais, makamu wa rais, waziri mkuu na baadhi ya watendaji wa mashirika makubwa ya umma kama njia ya kuwaunga mkono gazeti la Mwananchi kwa habari yao hiyo,” alisema.
  
Kwa mujibu wa Zitto, mapato ya mbunge yanajulikana sasa kuwa ni sh milioni 11.2 kwa mwezi kabla ya kuongeza posho za vikao za sh 200,000 kwa siku na posho ya kujikimu ya sh 130,000 kwa siku.
  
“Watanzania wana haki ya kujua wanawalipa kiasi gani watumishi wao. Tutaanza na mshahara wa rais,” alisema.
Alisema kuwa gazeti la Mtanzania limefungiwa pamoja na mambo mengine kwa kuandika ‘mapinduzi ni lazima’. Kwamba inashangaza Serikali ya CCM inaogopa neno mapinduzi.
  
“Marehemu Mzee Steven Salum Nandonde, aliyekuwa mbunge wa Tandahimba alipata kusema bungeni kuwa ‘lazima nchi ipinduliwe’. Ni matumizi ya lugha tu. Mzee Nandonde yeye alikuwa analalamikia maendeleo duni ya mikoa ya kusini na kutaka kaskazini iwe kusini na kusini iwe kaskazini,” alisema.
  
Zitto aliongeza kuwa serikali inafungia gazeti kwa sababu ya kuandika ‘Mapinduzi ni lazima’ ilhali kila siku Zanzibar wanasema ‘Mapinduzi daima’.
  
“Gazeti la Mtanzania linahaririwa na Absalom Kibanda, mwandishi wa habari ambaye bado anaponya majeraha ya mwili na kisaikolojia ya kuteswa na watu ambao hadi leo hawajakamatwa.
  
“Badala ya serikali kuwakamata watesaji wa Kibanda, inamnyima kazi Kibanda ili ateseke kwa njaa kwa kukaa miezi mitatu bila kazi,” alisema.
  
Pia aliongeza kuwa inawatesa Watanzania kwa njaa ya kupata habari ambayo ni haki ya msingi ya kikatiba. Kwamba hiyo ndiyo zawadi serikali inampa Kibanda baada ya kung’olewa kucha, kunyofolewa jicho, kukatwa vidole na kuteswa kwa namna isiyoelezeka.
  
“Matukio ya hivi karibuni na namna serikali inavyoyachukulia yanaonyesha dhahiri kwamba Rais Kikwete kazidiwa nguvu na kundi la wahafidhina ndani ya chama na serikali yake.
  
“Rais ambaye alianza kwa kuhubiri uvumilivu wa hali ya juu, na hata yeye mwenyewe kupata kusema uvumilivu huu wengine wanauona kama udhaifu, lakini ameamua kujenga taifa la kutovumiliana,” alisema.
  
Kwa mujibu wa Zitto, rais alipata kulalamika hadharani kwamba kuna wenzake wanataka aongeze ukali, hivyo ni dhahiri kundi hili la wahafidhina sasa ndilo linalomwongoza Rais Kikwete.
  
“Kitu kimoja tu rais azingatie, kundi hili linaongozwa na maslahi binafsi ya kubakia kwenye utawala wakati yeye anapaswa kuacha ‘legacy’,” alisema.
  
Alisema kuwa Rais Kikwete asipokuwa makini atakuwa rais karatasi (lame duck) tu tunapoelekea mwisho wa utawala wake.
  
Kwamba uamuzi wa hovyo na wa kidikteta wa kufungia magazeti unamchora vibaya mbele ya wananchi na jamii ya kimataifa.
  
“Wananchi sasa waifanye serikali kujutia uamuzi wake wa kufungia magazeti. Nimeamua mimi binafsi kama mbunge (leo Septemba 30, 2013) kupeleka taarifa rasmi kwa Katibu wa Bunge ya kupeleka muswada bungeni wa kuifuta kabisa sheria kandamizi ya magazeti ya mwaka 1976,” alisema.
  
Ndimara anena
Katika andiko lake kwenye mtandao wa kijamii, mwandishi wa habari nguli, Ndimara Tegambwage alisema kufungia magazeti ni uhalifu dhidi ya haki.
  
Alisema: Serikali inaendelea kufungia vyombo vya habari. Orodha inaongezeka. Mara hii ni zamu ya Mwananchi na Mtanzania.
  
MwanaHALISI lilifungiwa miezi 15 iliyopita (mwaka mmoja na robo). Hakuna dalili za kulifungulia. ‘Redio mbao’ zinasema hata wamiliki wake wasiruhusiwe kuanzisha gazeti jingine. Limekuwa suala la binafsi.
  
Hatua ya serikali ya kufungia gazeti hilo imeathiri na inaendelea kuathiri waandishi, wake/waume zao na watoto wao; wazazi wao, ndugu waliowategemea, wauza magazeti, wenye maduka karibu na ofisi za gazeti hili, wauza matunda, mihogo, karanga, kahawa na kashata waliokuwa wakitua MwanaHALISI.
  
Wengi wameathirika hivyo kiuchumi. Sasa waandishi wamekuwa wabangaizaji kwa kuomba vibarua katika magazeti ya wengine. Wananchi wengi wameathirika kwa njia ya kukosa taarifa.

Mtu mmoja serikalini au kundi la watu; wanatumia nafasi zao kutaka kuua kwa njaa waandishi na familia zao; na kunyima wananchi taarifa muhimu zinazowawezesha kupata uelewa juu ya wanavyotawaliwa na jinsi ya kujinasua kutoka mkenge wa ghiliba, wizi na ufisadi.
  
Jana serikali iliongeza machungu kwa waandishi na wananchi na orodha yote niliyotaja hapo juu kwa amri ya kufungia magazeti ya Mwananchi na Mtanzania. Na serikali inajua. Hiyo siyo njia sahihi ya kutenda kazi. Serikali inaingilia kazi na majukumu ya mahakama.
  
Kwa ufupi, serikali inapuuza na kudharau mahakama. Kuna sheria ya magazeti ya mwaka 1976, katili kama ilivyo, lakini bado inatumika na watawala ndio wameiweka mbelekoni. Kwanini serikali haiitumii kwa njia ya kwenda mahakamani? Inaogopa nini? Woga wake ni upi?
  
Kuna Baraza la Habari Tanzania (MCT). Limejaa na linashirikisha wataalamu wa nyanja muhimu katika tasnia hii - waandishi wa habari na wanasheria. Lina uwezo mkubwa wa kusikiliza na kutolea uamuzi malalamiko ya mtu au taasisi yoyote. Serikali hailitumiii.

 Wahusika ndani ya serikali wanatumia ubabe wa amri kwa nia ya ‘kuua sisimizi kwa kutumia nyundo’, lakini nje ya mkondo wa sheria au ushauri wa kitaaluma ambao unaheshimika zaidi kuliko amri au mitulinga.
  
Kesho serikali itazima gazeti au chombo kingine cha habari. Itaondosha ajira za waandishi. Itafinyaza fursa za kujiendeleza katika taaluma hii. Itanyakua haki ya uhuru wa kupata taarifa na habari.
  
Itafanya kazi zake gizani na kwa hiyo bila mrejesho kutoka kwa jamii pana iliyokuwa inapata taarifa kupitia vyombo vya habari vinavyofungiwa.
  
Kufungia au hata kufuta chombo cha habari, licha ya kwamba ni kuvunja haki za binadamu; vilevile ni kuziba mifereji ya fikra ya jamii; kuongeza umasikini, kuasisi woga miongoni mwa watu, kujenga visima vya chuki na hasira dhidi ya serikali; kutaka watu waishi kwa umbeya na kurudisha jamii katika ujima.
  
Hatupendi kuamini kuwa haya yanatendwa na serikali inayojiita ya ‘kidemokrasia’ na inayojigamba kuwa na uwazi na utawala bora. Hapana! Kuna serikali ngapi - moja itende demokrasia na nyingine itende uhalifu dhidi ya haki ya uhuru wa habari? Ghiliba!
  
Tumependekeza tangu 1985. Kwamba serikali iache wananchi na waandishi wa habari waiseme wanavyoiona. Kama sivyo ilivyo, basi ipuuze. Kama ndivyo ilivyo, basi ijisahihishe.
  
Serikali ina maguvu mengi ya kutumia kuleta mabadiliko kwa maslahi ya watu; na siyo kwa kuangamiza uhuru wa kufikiri na kutoa mawazo. Inakokwenda serikali, siko!
  
Lwaitama
Mhadhiri mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Lwaitama alisema si sahihi kufungia magazeti na serikali kuanza kupangia wananchi wasome au wasisome nini.
  
“Tunaomba tuambiwe mahojiano hayo na maonyo yalifanyika chini ya uangalizi wa nani? Na yalifanyikia wapi? Hapa ninaona kuna kikundi kidogo cha watu fulani katika serikali wameamua kuanza kufungia magazeti kwa manufaa yao,” alisema.

Dk. Lwaitama aliongeza kuwa tuhuma zinapotolewa zipelekwe kwenye chombo cha uamuzi ili hukumu itolewe, kwamba haiwezekani serikali ndiyo inatoa tuhumu na kuhukumu yenyewe.
  
“Tumekuonya, hatupendezwi na uandishi wako, hivyo tunakufungia siku 14 au siku 90,” hizi ni kauli za utawala wa kibabe, na udikiteta. Hakuna dhana ya utawala bora,” alisema.
  
Alihoji kuwa kama kosa ni uchochezi, mbona kuna kesi mahakamani inayomhusu Kibanda na mwandishi Samson Mwigamba wakidaiwa kuchapisha makala ya uchochezi?
  
Kwamba kesi hiyo ina utofauti gani na tuhuma hizi zinazoitwa uchochezi hadi kusababisha magazeti ya Mwananchi na Mtanzania kufungiwa bila kupelekwa mahakamani?
  
Dk. Lwaitama alisisitiza kuwa kitendo kilichofanywa ni kama vile Tanzania hakuna mahakama wakati rais anateua majaji kila mara, na hivyo kuhoji kazi zao ni zipi kama mawaziri wanajipangia hukumu.
  
Wanaharakati
Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THIRD Coalition), Onesmo Olengurumwa alisema leo wanakutana na wadau mbalimbali wa habari kwa lengo la kujadili na kutoa tamko rasmi kuhusiana na suala la kufungiwa magazeti hayo.

Alisema mara baada ya kukutana watazungumza na waandishi wa habari kutoa maazimio waliyofikia katika kikao hicho.

Hata hivyo, alisema sheria ya magazeti ya mwaka 1976 ni kandamizi na inahitaji kuondolewa.

Olengurumwa aliongeza kuwa sheria zilizopo zinakandamiza uhuru wa vyombo vya habari.
  
“Sheria hii ni kandamizi kwa kuwa serikali wao ndio walalamikaji, lakini wao wenyewe wanatoa uamuzi bila kushirikisha upande wa pili, jambo ambalo ni unyimwaji wa uhuru wa vyombo vya habari,” alisema.
  
Zanzibar wacharuka
Jumuia ya Waandishi wa Habari za Maendeleo Zanzibar (Wahamaza) nayo imeungana na watetezi wa uhuru wa vyombo vya habari kusikitikia uamuzi wa serikali kufungia magazeti ya Mwananchi na Mtanzania.
  
Katibu wa Wahamaza, Salma Saidi alisema uamuzi wa serikali umetolewa wakati wanatasnia ya habari wanadai uhuru zaidi wa habari, na wakati bado wanalalamikia kufungia gazeti la MwanaHALISI kwa muda usiojulikana.
  
“Wahamaza inaamini kuwa adhabu ya kuyafungia magazeti ni kubwa mno na haikusitahiki, na sababu zilizotolewa na serikali kuyafungia magazeti hayo hazitoshelezi,” alisema.
  
Alisema kuwa wanaamini kwamba njia bora ya serikali kujenga utawala bora wenye kuheshimu sheria ni kutumia mahakama katika malalamiko dhidi ya habari zinatolewa na vyombo vya habari.
  
“Wahamaza inatoa wito kwa wadau wa vyombo vya habari nchini kuendelea na harakati za kuitaka serikali kufuta sheria zote zitazotumia kukandamiza vyombo vya habari ikiwa pamoja na sheria ya kufungia magazeti,” alisema.


SEMINA YA KAMATA FURSA TWENDZETU KWA VIJANA YAFANYIKA LEO JIJINI MWANZA.

 Naibu Waziri wa Nishati na Madini,Mh Stephen Masele akizungumza mada iliyohusu fursa mbalimbali zinazopatikana kwenye nishati na madini ndani ya semina ya kamata fursa twendzetu,iliyofanyika mapema leo ndani ya ukumbi wa Gold Crest.
  Naibu Waziri wa Nishati na Madini,Mh Stephen Masele akimtambulisha mmiliki wa hotel kubwa ya kitalii hapa jijini Mwanza, Gold Crest,Bwa.Mathias Erasto,ambaye pia ni mchimbaji mdogo wa madini,aliyajipatia fursa mbalimbali na kuzitumia ipasavyo na kufikia hapo alipo kimafanikio.
 Mkuu wa Wilaya ya Iramba mkoani Singida,Mh.Yahaya Nawanda akizungumzia mada yake iliyohusu suala la ufugaji,hasa kuku wilayani mwake,ambapo pia amewataka vijana kuitumia fursa ya ufugaji wa aina yoyote katika suala zima la kujiletea maendeleo kwa namna moja ama nyingine badala ya kusubiri Serikali iwafanyie ama iwaletee kila kitu hapo walipo.
Naibu Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia,Mh Januari Makamba akizungumza kwenye mada yake iliyohusu masuala mbalimbali, kuhusiana na Fursa ya kuongeza thamani na kutengeneza jina,sambamba na fursa ya matumizi ya Teknolojia mbele ya maelfu ya vijana waliojitokeza kwa wingi mapema leo kwenye semina ya kamata fursa twendzzetu,iliyofanyika leo,ndani ya ukumbi Gold Crest,jijini Mwanza.
 Sehemu ya wakazi wa mji wa Mwanza waliojitokeza kwa wingi mapema leo kwenye semina ya kamata fursa twendzetu,wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ukumbini humo,ambapo mada mbalimbali zilikuwa zikizungumzwa. 
  Mmoja wa wasanii wa bongofleva,Nikki Wa Pili akizungumza kwenye semina ya kamata fursa twendzetu.
 Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Maxcom inayouza bidhaa yake ijulikanayo kama Max Malipo,Bwa.Juma Rajab akizungumzia kuhusiana na fursa ya bidhaa yake ya Max Malipo inavyoweza kuisadia jamii kwa namna moja ama nyingine.
Baadhi Washiriki wakifuatilia.
Mmoja wa waigizaji mahiri wa filamu hapa nchini Elizabeth Michael akijulikana zaidi kwa la kisanii kama Lulu akiwasili kwenye semina ya kamata fursa Twendzetu,ndani ya ukumbi Gold Crest,jijini Mwanza asubuhi hii,ambapo pia atazungumzia mambo kadhaa mbalimbali kwenye semina hiyo,ambayo itawakutanisha Naibu Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia,Mh Januari Makamba,Mbunge wa jimbo la Kigoma Kaskazini na watoa mada wengine mbalimbali

Mkurugenzi  Mtendaji wa Benki ya Wanawake Tanzania (TWB),Bi.Magreth Chacha alipokuwa akiwasili kwenye  semina ya kamata fursa Twendzetu,ndani ya ukumbi Gold Crest,jijini Mwanza asubuhi hii.

Naibu Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia,Mh Januari Makamba akiwa ameambatana na Naibu Waziri wa Nishati na Madini,Mh Stephen Masele (mwenye miwani) akisalimiana na Mkurugenzi wa Benki ya Wanawake Tanzania (TWB),Bi.Magreth Chacha walipokuwa wakiwasili kwenye  semina ya kamata fursa Twendzetu,ndani ya ukumbi Gold Crest,jijini Mwanza asubuhi hii,pichani kati ni Mkurugenzi wa vipindi na uzalishaji Clouds Media Group,Bwa.Ruge Mutahaba.

Baadhi ya Wakazi wa mji wa Mwanza na vitongoji vyake wakiwa wamejitokeza kwa wingi kwenye  semina ya kamata fursa Twendzetu,ndani ya ukumbi Gold Crest,jijini Mwanza asubuhi hii. 
 Sehemu ya meza kuu.

Wednesday, September 18, 2013

KIGOGO WA MAGARI YA WIZI DAR ATIWA MBARONI


Stori: Makongoro Oging' na Haruni Sanchawa
Jengo ambalo linadaiwa ndiyo kiwanda hatari cha kubadilisha magari ya wizi, kimefumuliwa na mmiliki wake sasa hivi yupo nyuma ya nondo akingoja kufikishwa mahakamani.
Benovilla Luhanga, 43, ametajwa kuwa ndiye mmiliki wa kiwanda hicho na siku ananaswa, alikutwa na magari ya kihafari matano ambayo yote inadaiwa ni ya wizi.
Vilevile, Luhanga alikutwa na Bajaj moja ambayo imedaiwa nayo ni ya wizi na kwamba alikuwa tayari ameshaibadili rangi.
Luhanga alikamatwa akiwa na mkewe ambaye jina lake halikupatikana mara moja.
Moja ya gari alilokutwa nalo mtuhumiwa.
Kigogo huyo na mkewe, wanaishi ndani ya nyumba hiyo iliyopo Mbezi Beach, Dar es Salaam, kwa nje huonekana kama gereji lakini ndani ni makazi ya watu na shughuli za ubadilishaji magari, Bajaj na pikipiki hufanyika humo.
Luhanga na mkewe walikamatwa baada ya polisi kuvamia kiwanda hicho, saa 5 asubuhi lakini mchakato wa ukamataji ulikamilika saa 10 alasiri.
Mchakato wa kuwakamata uliwagharimu polisi jumla ya saa 5 kukamilika kwa sababu ilibidi kufanya upekuzi wa hali ya juu kwenye kiwanda hicho ili kubeba kila kitu kilichoonekana ni cha wizi.
Magari yote yaliyokutwa kwenye kiwanda hicho pamoja na Bajaj moja, ilidaiwa ni mali za wizi huku tayari yakiwa yameshabadilishwa rangi na kufungwa namba feki za usajili, isipokuwa gari moja.
Gari aina ya Nissan Navara lenye thamani ya shilingi milioni 45 alilokutwa nalo mtuhumiwa.
ZA MWIZI ZILIVYOTIMIA
Habari zinaeleza kuwa kuwa kiwanda hicho kiligundulika kutokana na kijana mmoja ambaye aliwahi kuibiwa gari aina ya Toyota Canter, Goba, Dar, hivi karibuni.
Imebainika kuwa kijana huyo baada ya kuporwa gari hilo ambalo yeye alikuwa ameajiriwa kama dereva, maisha yalimwendea kombo kabla ya kwenda kwa Luhanga kuomba kazi, akidhani ni gereji.
Chanzo chetu kilitamka kuwa akiwa ndani ya kiwanda hicho, kijana huyo aliliona hilo Toyota Canter ndani ya uzio wa kiwanda hicho, hivyo kutoa taarifa Kituo cha Polisi Kawe, Kinondoni, Dar.
“Baada ya kuripoti, askari walifuatilia na kukuta kweli kuna gari aliloibiwa kijana huyo na walipofanya upekuzi wakayakuta magari mengine matano yaliyoripotiwa kuibwa,” kilisema chanzo hicho.
Habari zinasema, polisi waliweza kubaini kuwa magari hayo baadhi yake yalibadilishwa rangi na kupakwa nyeusi huku namba za usajili nazo zikiwa zimebadilishwa.
Nyumba anayoishi kigogo huyo.
KAMATAKAMATA IKAANZA
Polisi baada ya kugundua wizi huo, kamanda aliyeendesha oparesheni hiyo ambaye jina lake halikufahamika mara moja, aliamuru Luhanga na mkewe wakamatwe na magari yaliyokuwa na uwezo wa kutembea yaliendeshwa, mengine yalikokotwa kwa ‘breakdown’ hadi Kituo cha Polisi Kawe.
Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa watuhumiwa hao tayari wamefunguliwa jalada katika kituo hicho kwa namba KW/RB/8194/2013 WIZI WA MAGARI.
Waandishi wetu walipofika kituoni Kawe Jumapili iliyopita, walikuta ndugu sita wa Luhanga wakihaha kutaka kuwawekea dhamana.
MAGARI YALIYOIBWA
Magari yaliyoibwa ni aina ya Nissan Navara lenye thamani ya shilingi milioni 45, lililokutwa na kibao cha usajili namba T519 BNP.
Lingine ni Toyota Harrier, ambalo thamani yake ni shilingi milioni 30. Hili lilikutwa na namba za usajili T 924 AXB, wakati kuna Toyota Rav4 new model, lenye thamani ya shilingi milioni 40 ambalo lilikutwa na namba T 581 BBL.
Gari lingine ni Toyota Canter, vilevile kulikuwa na Rav4 new model nyingine lenye rangi ya kijivu, hili lilikuwa limeng’olewa namba zake halisi bila kuwekewa nyingine.
Rav4 hilo ambayo halikufungwa namba, imeelezwa lilikuwa halijabadilishwa rangi, kwani kwa kawaida yale yanayoporwa na kuingizwa kiwandani humo, hupakwa rangi nyeusi.
OFISINI KWA KAMANDA WA POLISI
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi, Kinondoni, ACP Camillius Wambura, hakuweza kupatikana licha ya waandishi kufika ofisini kwake. Hata hivyo, ofisa mmoja mwandamizi wa jeshi hilo, alithibitisha kutokea kwa tukio.
“Tukio hilo lipo na tunaendelea na uchunguzi,” alisema ofisa huyo huku akiomba asiandikwe jina lake gazetini kwa kuwa siyo msemaji wa jeshi hilo.

Sunday, September 15, 2013

MWAKYEMBE ABAINI KUTOBOLEWA KWA BOMBA LA MAFUTA BANDARINI..ATOA SIKU MBILI


Waziri wa uchukuzi Dkt. Harrisoni Mwakyembe amebaini wizi wa mafuta katika boya la mafuta mjimwema na kuagiza maskari wa usimamizi wa bandari Tanzania kuwakilisha majina ya wahusika ndani ya siku mbili.

Mwakyembe ameyasema hayo wakati akizungumza na wafanyakazi wa mamlaka ya usimamizi wa bandari Tanzania (TPA) na kulaani kitendo cha baadhi ya watu kutoboa bomba hilo na kuunganishia mabomba yao madogo na kuyafungia kwenye maputo yenye uwezo wa kubeba mafuta kati ya lita 16-18 kinyume cha sheria na kukiita kitendo hicho ni kuhujumu uchumi wa nchi ambapo ameishutumu kampani ya ulinzi ya tipa kuhusika na kitendo hicho na kuwataka kumpa picha za wafanyakazi wote waliokuwa kitengo cha ulinzi na kama hawatafanya hivyo kampuni hiyo italipishwa fidia.

Naye kaimu mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya usimamizi wa bandari Tanzania Mhandisi Madeni Kipande wakati akijibu mapendekezo yaliyotolewa na waziri mwakyembe kuhusu wafanyakazi wa mamalaka hiyo amesema kuwa wafanyakazi waliokuwa wameajiriwa kama vibarua watapewa ajira za kudumu na kubainisha kuongezewa posho wafanyakazi hao kutoka laki moja awali na kufikia laki mbili pamoja na laki moja na nusu kama ghrama za chakula

-ITV bukobastarlink.com

Tuesday, September 10, 2013

KANALI ALIYETOROKA JESHINI AIPASUA KICHWA JWTZ



LUTENI Kanali Coelestine Seromba aneyedaiwa kutoroka ndani ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), bado hajulikani alipo hadi hivi sasa. Msemaji wa JWTZ, Meja Erick Komba ameliambia gazeti hili jana kuwa kazi ya kumtafuta Luteni Kanali Seromba inaendelea kimyakimya na kusisitiza kuwa suala hilo halihitaji kutangazia umma wamefikia hatua gani. 

Komba alisema wanajeshi kadhaa walikimbia katika jeshi hilo lakini hawajatangazwa na wao kama jeshi hawaoni sababu ya kufanya hivyo kwani wana utaratibu wao. “Huyo Luteni Kanali Coelestine Seromba anayedaiwa kukimbia ni mwanajeshi mtoro kama wanajeshi wengine watoro na pindi atapopatikana atatiwa hatiani kama kanuni za jeshi zinavyosema,” alisema Meja Komba.

Akijibu swali aliloulizwa na mwandishi wa habari hizi kuhusu kuchelewa kukamatwa kwa Luteni Kanali Seromba, Meja Komba alisema hatua za kumfuatilia si lazima zitangazwe na pia mahali lilipofikia jeshi hilo katika kumtafuta ni siri yao.

Meja Komba alisisitiza kuwa Luteni Kanali Seromba hakuondoka na nyaraka yoyote ya jeshi hilo wala vifaa vyovyote kama inavyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari. 

Komba aliwasihi waandishi wa habari kuzingatia maadili ya uandishi kwa kuandika habari za kweli na zenye tija kwa pande zote ili kutojenga chuki baina ya jeshi na taasisi zingine. 

Alitolea mfano kuwa miaka ya hivi karibuni ambapo baadhi ya wanasiasa walitamka wazi kuwa jeshi hilo linakula bure hivyo hakuna umuhimu wa kutengewa bajeti kubwa huku wakisahau jukumu la jeshi hilo ni kulinda amani ya nchi na mipaka yake ili wananchi waishi kwa usalama.

Meja Komba alitoa mfano wa vurugu zilizotokea bungeni hivi karibuni kuwa kama Polisi wangeshindwa kudhibiti vurugu hizo hatua ya mwisho ilikuwa jeshi kuingilia kati, lakini watu wanadai wanajeshi wanakula bure. “Kikubwa ninachoweza kueleza hapa ni kalamu za waandishi kutumika vizuri ili kutoweka chuki kati ya taasisi zingine likiwemo jeshi letu nje ya nchi,” alisema Meja Komba huku akigusia namna msuguano kati ya viongozi wa Tanzania na Rwanda ulivyoripotiwa.

“Mengi yaliyoripotiwa ni kama nchi hii na Rwanda zinaingia vitani na uhasama huo kuhamia kwa wananchi na kujenga chuki na baadaye kuchukiana na hata kuweza kugombana wenyewe kwa wenyewe,” alisema.

Pia aliwakumbusha wananchi kuendeleza amani iliyopo kwani vita vina gharama kubwa na endapo nchi ipo vitani hata Bunge linaweza kusitishwa kutokana na fedha nyingi kupelekwa katika mapigano. 

Chanzo kimoja kutoka ndani jeshi hilo kimesema kutoroka kwa Luteni Kanali Seromba aneyedaiwa kukimbilia Rwanda hakuwezi kuleta tishio lolote ndani ya jeshi hilo.

Pia taarifa zilizopatikana ndani ya jeshi hilo zinadai kuwa kitengo alichokuwa Luteni Kanali Seromba ni kitengo cha kawaida na kwamba mafunzo yake hutolewa kimataifa na kila nchi ina mtu kama huyo.

18+ ONLY: PICHA ZA BEHIND THE SCENE ZA MOVIE YA NGONO YA KWANZA YA KENYA


The controversial and highly hyped House of Lungula is about to hit the silver screens. If you have not heard about the film, it’s about the weird s3x#@l habits of Kenyans packaged with some humor.

Some of the actors and actresses acting in the controversial film which will rock the industry include TPF judge Ian Mbugua, former BBA contestant Sheila Kwamboka, KTN’s Nice Githinji, Citizen TV’s Sarah Hassan, Liz Njagah among others.

Below are behind the scene photos of the making of the film:



















SPIKA WA BUNGE NDUGAI AJIGAMBA KUMTOA FREEMAN MBOWE BUNGENI

*Asema wanaompinga ni mbumbumbu wa kanuni za Bunge
NAIBU Spika, Job Ndugai ametetea uamuzi wake wa kuagiza kutolewa ndani ya ukumbi wa Bunge, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe akisema alikuwa sahihi.

Mabishano hayo ambayo yalisababisha kuibuka kwa vurugu bungeni yalitokea mwishoni mwa wiki, muda mfupi baada ya kipindi cha maswali na majibu, ambapo kiongozi huyo wa Bunge aliruhusu mjadala kuhusu Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba uendelee.

Kutokana na hali hiyo, Mbowe alisimama kutaka kutoa ufafanuzi juu ya mjadala huo, lakini Ndugai alimzima na kumtaka kukaa chini, jambo ambalo halikumfurahisha Mbowe na kumfanya agomee agizo lake.

Akizungumza na MTANZANIA jana kwa njia ya simu, Ndugai alitumia muda mwingi kutetea uamuzi wake na kukosoa hoja za watu wanaompinga juu ya uamuzi wake huo.

Ndugai alisema katika kikao hicho, Mbowe alifanya jeuri kubishana na kiti na kueleza kuwa kanuni za Bunge zinasema hakuna mbunge yeyote atakayesimama kuzungumza bila kuruhusiwa na kwamba uamuzi wa kiti ndiyo wa mwisho.

Ndugai alisema wanaomtuhumu kwamba hakutenda haki kumuamuru Mbowe akae chini, wanafanya hivyo kwa vile hawajui kanuni za Bunge.

Ndugai alisema kwa mujibu wa kanuni, ni Rais wa Jamhuri pekee ndiye anayeruhusiwa kulihutubia Bunge kwa wakati anaoona yeye unafaa, lakini si mbunge.

“Hata rais mwenyewe ni lazima amwandikie barua spika, huu ndiyo utaratibu lakini si mbunge au waziri anayeruhusiwa kusimama kwa wakati anaoutaka yeye kuzungumza akaruhusiwa, ni lazima ataomba ruhusa kwa Spika na kama ipo nafasi ya kufanya hivyo Spika atamruhusu, kama haipo hataruhusiwa.

Alipoulizwa kwamba haoni kama alivunja kanuni kwa kumzuia Kiongozi wa Upinzani bungeni wakati kanuni za mabunge ya Jumuiya ya Madola zinatoa upendeleo kwa kiongozi huyo na waziri mkuu ndani ya Bunge, Ndugai alisema:

“Katika vikao vya Bunge, uamuzi wowote wa Spika unakuwa wa mwisho na hauwezi kupingwa na mbunge au waziri yeyote.

“Mbowe nilimuomba kwa heshima sana atupishe kwanza, nilimuelekeza karibu mara tatu…lakini mtu mzima anavunja utaratibu.

“Huyu Mbowe amejivunjia heshima mwenyewe, hata kanisani anayeendesha ibada ni mtu mmoja tu, na wengine wanapaswa kufuata utaratibu.

“Kwanza Mbowe alijitoa mwenyewe kwenye orodha kwa maandishi na ninayo hapa.... yeye na Halima Mdee, sasa alisimama kufanya nini kama sio ujeuri?

“Kanuni anazijua mimi ningemruhusu tu, lakini kwa ujeuri hakufanya hivyo. Kuna taratibu za bunge, mbunge anakaa chini pale Spika anaposimama na wasome kanuni, sasa hapo mjeuri ni nani? 

“Tujifunze kanuni haiwezekani mtu yeyote asimame saa yoyote, kila mmoja hawezi kufanya anavyotaka, kuna taratibu zake, kiti kikimuona atapewa nafasi kama ipo na iwapo kiti kikiridhika,” alisema Naibu Spika.