Monday, November 4, 2013

MAKALA:TANZANIA TUNAONEWA AMA HATUJAPELEKA WAIMBAJI WENYE VIPAJI TUSKER PROJECT FAME?



Imeandikwa na Bongo5.com
Kwanza kabisa, naomba nijilaumu kwa kuwa na matarajio mengi kwa wawakilishi wa Tanzania kwenye msimu huu wa shindano la Tusker Project Fame. Ndio maana waliosema ‘Less expectation, Less hurt, don’t expect too much’ ama ‘too much expectation leads to disappointment’ hawakuwa wajinga.


Niliandika tweet hiyo kwa kujiamini mno kwakuwa naufahamu uwezo wa Tanah na Angel hata kabla ya hapo.

Nani asiyeijua sauti tamu ya Angel kwenye wimbo wa Ommy Dimpoz, Baadaye? Utamu wa sauti yake, ndio uliichanganya hadi academy ya Kili Music Awards imtaje mwaka huu kuwania kipengele cha Msanii Bora Anayechipukia, pamoja na kwamba hajawahi kutoa wimbo wake mwenyewe.

Kama umewahi kusikiliza nyimbo za kundi la Tanchy linaoundwa na Tanah na Chibwa, bila shaka utakuwa na picha kidogo ya uwezo wa Tanah.

Nitaanza kumzungumzia kwanza Tanah aliyeanza kutolewa kwenye shindano hilo wiki ya kwanza tu. Nilisema wazi, kutolewa kwa Tanah kulikuwa kwa uonevu zaidi kuliko kwa washiriki wengine hasa kwakuwa siku hiyo aliimba vizuri kuwazidi washiriki wengi tu waliobakia kwenye academy.

Nilikuwa na uhakika na bado ntaendelea kuwa na msimamo huo kuwa, Tanah alionewa. Ama tuseme alichukuliwa poa, na masikio ya majaji yalilazimisha kumsikia tofauti? Ama pengine chaguo la wimbo wa Alicia Keys, ‘No One’ aliouimba siku hiyo lilishindwa kumpa wigo mpana wa kukinadi kipaji chake? Lakini nahisi, wakati mwingine, majaji na walimu wanapaswa kutoa hukumu kwa kuangalia mengi zaidi ya uchaguzi mbaya wa wimbo. Ni rahisi kukitambua kipaji cha mtu, hata kama wimbo aliouchagua utamnyima fursa ya kutoa kile anachoweza kukifanya.

Nakubali kuwa, ni rahisi mimi kusema hivyo kwakuwa naujua uwezo wake tofauti na ule aliouonesha kwenye jukwaa la TPF6 kiasi kilichowafanya majaji wamuone Tanah wa kawaida, lakini siungi mkono yeye kuondolewa mapema hivyo.

Kwa upande wa Durbat aliyetolewa siku moja na Tanah, sina cha kumtetea hasa kwakuwa alionesha uanagenzi wa hali ya juu kwenye tumbuizo lake. Lawama ni kwa jopo la majaji lililompitisha kwenye usaili wa Dar. Ni kweli huo ndio mwisho wa vipaji vya Tanzania hadi yeye kuchukuliwa na kwenda kuboronga? Si kweli.

Nashindwa kueleza ni kwa kiasi gani niliumia Jumamosi baada ya Angel kutolewa. Niliumia kiasi cha usingizi wangu wa siku hiyo kuharibika. Kama shabiki wa mpira anavyoweza kuumia hadi kukataa kula chakula kwakuwa timu yake imefungwa, basi nami pia ndivyo nilivyoumia siku hiyo. Kama nilivyosema awali, matarajio makubwa siku zote hulipwa na fedheha, maumivu na uchungu.

Nakubaliana na Hermy B kuwa, kilichomponza Angel Jumamosi ni kutojiamini. Bahati mbaya ni kuwa, wasiwasi na uimbaji ni kama kuchanganya Big G na karanga, kamwe haviendani. Wasiwasi ulimfanya Angel aimbe kama mwanafunzi aliyeshika kipaza kwa mara ya kwanza. Woga ulikikandamiza kipaji cha Angel aliyekuwa tegemeo la Watanzania na akaonekana si kitu.

Kama wasemavyo waswahili kuwa ‘Siku ya kufa nyani miti yote huteleza’ ndivyo ilivyotokea Jumamosi kwakuwa washiriki hawakuruhusiwa tena kumwokoa mshiriki kama mwanzo. Huenda Angel angeliokolewa na angeendelea kushiriki.

Kingine ambacho TPF inapaswa kukibadilisha ni kuondoa utaratibu wa wasanii walioingia kwenye probation kuimba nyimbo zilezile zilizowapeleka probation. Sitaki kuamini kama msanii aliyeimba vibaya wimbo fulani atakuja auimbe vizuri ama tofauti baada ya mazoezi ya wiki moja. Chaguo baya ni baya tu. Ni sawa na kujipaka mafuta bila kuoga. Ni bora wangepewa fursa ya kuchagua nyimbo zingine na kutozirudia zile zilizowapeleka kwenye probation.

Na sasa Tanzania, imebakiza mshiriki mmoja tu. Tunamtegemea kuwa atatuokoa na aibu ya kuchekwa na wenzetu hasa katika kipindi hiki ambacho Jumuiya ya Afrika Mashariki inaendelea kuyumba. Kinachotia wasiwasi ni jinsi wenzetu wanavyotuchukulia poa kwenye shindano hilo.

Nilifurahi kuwa Jumapili hii Hisia aliimba vizuri kiasi cha kuwafurahisha majaji wote, akiwemo jaji mgumu, Ian Mbugua. Hakika aliutendea haki wimbo wa Adam Levine ft Wiz Khalifa, Payphone. Kitu kingine ni kuwa Hisia ni kipenzi cha mabinti, huenda wakamuokoa kila atakapoingia kwenye probation.

SAJENTI, MAIMARTHA WASHINDANISHA WOWOWO!


Na Richard Bukos
MWIGIZAJI Husna Idd ‘Sajent’ na mtangazaji maarufu Bongo, Maimartha Jesse wamenaswa wakishindana ukubwa wa makalio yao wakiwa wamelala kitandani.

Tukio hilo lililowashangaza wadau, lilitokea hivi karibuni wakati mastaa hao walipokuwa wanarekodi moja ya vipindi vya washiriki wa Shindano la Vigori katika Hoteli ya Kebbys Mwenge jijini Dar.

“Jamani mimi ninalo (wowowo) kuliko wewe, ukubwa dawa mimi na wewe wapi kwa wapi Sajent?” alisikika Maimartha.

Tuesday, October 29, 2013

MWIGAMBA AANZA KUIANIKA CHADEMA..AWAONYA WANAO MWITA MSALITI


*Awaonya wanaomwita msaliti
*Dk. Slaa aibua mapya
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba, aliyesimamishwa uongozi asema atakichafua chama hicho kama ataendelea kuitwa msaliti.

Hatua hiyo, imekuja baada ya Mwigamba kukiri hadharani kusambaza waraka unaowatuhumu viongozi wa chama hicho katika mtandao wa Jamii Forum (JF), akitumia jina la Maskini Mkulima. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Arusha jana, Mwigamba aliwaonya viongozi wa Chadema wanaomwita msaliti. Alisema kama wanataka awe msaliti, yupo tayari kumwaga mambo yote hadharani, tena kwa ushahidi usio na shaka hata kidogo. 

Mwigamba, aliyejiunga na Chadema mwaka 2004, akiwa mwanachama wa kawaida, alisema akiwa makao makuu mjini Dar es Salaam kama mhasibu mkuu wa chama, ndipo alipoanza kutambua udhaifu mkubwa wa kiuongozi ndani ya chama chake.

“Niliondoka pale makao makuu kwa mizengwe, kiongozi mmoja mkubwa kabisa alinifukuza kazi kwa kunipigia simu, tena baada ya kuwasiliana na Mkurugenzi wa Fedha,Anthony Komu akiwa nje ya Dar es Salaam na kumwagiza anifukuze,” alisema Mwigamba.

Alisema kwa bahati mbaya, udhaifu huo umeshindwa kushughulikiwa na vikao rasmi vya chama, kwani yeyote anayejaribu kukosoa ama kuhoji iwe ndani ya vikao rasmi ama nje, hutangazwa kuwa ni msaliti.

Alisema kutokana na hali hiyo, ni wajumbe wachache ndani ya Chadema, hasa kwenye Kamati Kuu, ambao wanaweza kusimama kidete na kukosoa uongozi.

Aliwataja wajumbe hao, kuwa ni Dk. Kitila Mkumbo, Profesa Mwesiga Baregu, Mzee Shilungushela na marehemu Magadula Sherembi kabla hajafariki dunia.

Hata baada ya kuondolewa Aprili, mwaka jana, alirejea Arusha na hakuwahi kujitokeza kwenye vyombo vya habari ama mitandao kuzungumzia tatizo la viongozi na uongozi ndani ya chama.

“Matatizo yaliyomo ndani ya chama ambayo wanachama wa kawaida wanaokiamini chama na viongozi wake wangeyasikia, hakika wangeweza kukata tamaa.


“Nimefanya hivyo kwa mapenzi na kwa maslahi ya chama changu, sasa kama viongozi wenzangu wanataka niwe msaliti basi waniambie hata leo nimwage ambayo yote hadharani, tena kwa ushahidi usio na shaka hata kidogo.

MCHEZAJI WA MPIRA AUMBUKA BAADA YA MZIGO WAKE KUVIMBA AKIWA UWANJANI



Huyu  ni  staa  wa  mpira  aitwaye Zlatan Ibrahimovic  akiwa  katika  wakati  mgumu  baada  ya  mzigo  wake  kuvimba  akiwa  uwanjani…


Taarifa  zinaarifu  kuwa, mzigo  huo  ulivimba  baada  ya  mchezaji  mwenzake  kumkumbatia  kwa  nyuma..

UWEZI AMINI TANZANIA IMETEGWA TENA KATIKA MKUTANO WA EAC


NCHI za Tanzania na Burundi, kwa mara nyingine zimetengwa na wenzao wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), baada ya marais wa Kenya, Uganda na Rwanda kukutana mjini Kigali jana. Marais hao walitarajia kujadili namna ya kuimarisha Jumuiya ya Afrika Mashariki kupitia uimarishwaji wa miundombinu, uchumi, biashara pamoja na kuweka mikakati ya shirikisho la kisiasa.

Kitendo cha kuziacha Tanzania na Burundi ambazo ni wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, kinazidi kutia shaka mtangamano wa jumuiya hiyo.

Nchi hizo mbili zimeshaeleza kusikitishwa na muungano wa nchi hizo tatu, ambao zimesema unakwenda kinyume cha makubaliano na mkataba wa EAC.

Katika mkutano huo, marais hao, Paul Kagame wa Rwanda, Yoweri Museveni wa Uganda na Uhuru Kenyatta wa Kenya, pamoja na mambo mengine, walitarajia kusaini makubaliano ya kuanzisha kituo kimoja cha kukusanya ushuru kinachotarajia kurahisisha uchukuzi wa bidhaa kutoka Mombasa nchini Kenya, Uganda hadi Rwanda.

Aidha Sudan Kusini ilialikwa ikiidhinishwa kama mshirika katika kikao hicho.

Mkutano huo unakuja baada ya ule uliofanyika mjini Kampala, Uganda, Juni mwaka huu na mwingine uliofanyika Mombasa, Agosti, ambako viongozi hao watatu walipendekeza kupanuliwa kwa Bandari ya Mombasa, ili kuwezesha uharaka wa bidhaa kupitishwa katika kuhudumia kanda nzima.

Mkutano mwingine wa marais wa nchi 15 za Afrika, ikiwamo Tanzania, utafanyika leo nchini hapa, katika kongamano la siku nne ambalo linatarajiwa kuweka kipaumbele kwa uimarishwaji wa huduma za internet katika mataifa hayo.


Kwa mujibu ya waandaaji, zaidi ya wajumbe 1,500 watahudhuria mkutano huo, chini ya uenyeji wa Rais Paul Kagame na Dk. Hamadoun I. Toure, Katibu Mkuu wa Muungano wa Kimataifa wa Mawasiliano ya Kiteknolojia (ITU).
-Mtanzania

MGANGA AKUTWA NA KIGANJA CHA BINADAMU AKIMUUZIA MTEJA WAKE KWA MILIONI 100 HUKO MWANZA.


Mtu mmoja jijini Mwanza anadaiwa kukamatwa na kiganja cha mtu akiwa anajiandaa kumuuzia mteja kwa sh million 100.

Washukiwa walikamatwa  jana  karibia na uwanja wa ndege wa Mwanza  wakifanya  biashara  hiyo  haramu.... 
 Baada  ya  upekuzi  wa  kina, mteja  alikuwa  ana  milioni  100  na mganga alikutwa  na   kiganja cha  binadamu  ambacho kilikuwa  kibichi kikitoa damu.


Kiganja  hicho  kilikuwa  kimevishwa  tunguri  na nywele za binadamu.

Saturday, October 26, 2013

POLISI 56 WAFUKUZWA KAZI KWA MAKOSA YA KUOMBA NA KUPOKEA RUSHWA

 

JESHI la Polisi nchini limewafukuza kazi askari wake 56 katika kipindi cha mwaka mmoja, kutokana na makosa ya kuomba na kupokea rushwa pamoja na utovu wa nidhamu.
  
Kamishna msaidizi wa jeshi hilo, Patrick Byatao, alisema hayo jana alipokuwa akitoa ufafanuzi juu ya mambo mbalimbali hususan masuala ya nidhamu kwa askari wake katika warsha ya siku maalumu ya polisi iliyofanyika mjini Bukoba.
  
Alisema kuwa askari waliofukuzwa ni kutoka katika mikoa mbalimbali nchini ambao wamekutwa na tuhuma za utovu wa nidhamu ikiwemo kuomba rushwa kwa wananchi. Kwa kipindi cha mwaka 2012, waliwafukuza askari 35 na mwaka huu 21.
  
Kwa mujibu wa Byatao, wapo baadhi ya askari ambao wamekuwa wakitoa visingizio vya kuomba rushwa kwa sababu mishahara yao ni midogo na haitoshelezi mahitaji yao.
  
Alisema ni heri askari wa aina hiyo wakaacha jeshi, vinginevyo wataendelea kuchukuliwa hatua kama hawatafuata masharti ya kazi yao.

Akitoa mada juu ya kuimarisha maadili ndani ya jeshi hilo, Mrakibu Msaidizi wa Polisi kutoka makao makuu, Andrew Makungu, alisema wameanzisha mkakakati wa kudhibiti vitendo vya ukiukwaji maadili kwa askari wake ikiwemo rushwa.
  
Alitaja maeneo lengwa kuwa ni chumba cha kupokea taarifa za mashitaka, usalama barabarani na upelelezi wa makosa ya jinai. Bado juhudi zinaendelea ili kuboresha maeneo mengine.
  
Makungu alisema ubia wa kiutendaji wa jeshi hilo umekuwa ukiimarika kila siku baada ya sehemu kubwa ya jamii kutambua nafasi yao katika jukumu hilo. 
  
Alisema mambo hayo yanaonekana kutokana na wananchi kufanya ulinzi wa maeneo yao, kuchangia rasilimali kwa jeshi, kutoa taarifa sahihi za uhalifu, kujenga vituo vya polisi na kuanzisha vikundi vya ulinzi shirikishi. Hadi sasa viko vikundi 5,344 nchi nzima huku Mkoa wa Kagera ukiwa na 431.
  

Naye mgeni rasmi katika warsha hiyo, Meya wa Manispaa ya Bukoba, Anatory Amani, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali mstaafu Fabian Massawe, alisema kuwa Jeshi la Polisi limekuja na mkakati wa polisi jamii/ulinzi shirikishi unaoelekeza kuwapo kwa mashauriano, majadiliano ya kiutendaji yanayosisitiza uwepo wa maadili katika kazi, ikiwemo mapambano dhidi ya rushwa ndani ya jamii.

RAIS WA USWISI AIFUNDA TANZANIA JINSI YA KUPATA FEDHA ZA KIFISADI


Katika mahojiano maalumu na timu ya waandishi wa Mwananchi na The Citizen jana, Graf alisema kuwa Serikali ya Tanzania inapaswa kusaini mkataba wa kimataifa wa kubadilishana taarifa za masuala ya usimamizi wa fedha na kodi ili kuweza kujua ni kina nani wameweka fedha nchini kwake na kunufaika na kodi.

Graf, ambaye alikuwa katika ziara ya kikazi nchini, alisema kuwa hivi karibuni Serikali ya Uswisi ilisaini mkataba wa kimataifa wa kubadilishana taarifa kuhusu masuala ya fedha, ambao unajulikana kwa lugha ya Kiingereza kama `Convention on Mutual Administrative Assistance in Tax Matters’.

Alisema ikisaini mkataba huo ina maana itasaidiwa na Serikali ya Uswisi kupata fedha zilizofichwa na Watanzania.

“Serikali ya Tanzania inatakiwa kuweka mkakati wa kisheria utakaotengeneza mazingira ya kubadilishana taarifa za fedha na mataifa mengine. Kwa jambo hilo hata Serikali ya Uswisi inaweza kusaidia katika kupatikana kwa fedha zilizofichwa,” alisema Graf, ambaye anaongoza Serikali ya Uswisi kwani kwa kawaida Rais wa Bunge ndiye pia kiongozi wa taifa hilo.

Graf alisema kwa sasa itakuwa ngumu kwa Tanzania kupata fedha hizo kwani haijasaini mkataba wa kimataifa wa kubadilishana taarifa za fedha na mataifa mengine.

Alieleza pia katika miaka ya karibuni Serikali ya Uswisi imeandaa muswada wa sheria wa kubana fedha zilizopatikana kwa njia za kifisadi na kufichwa katika benki za Uswisi. Graf alisema sheria hiyo ikipita itaruhusu Serikali ya nchi hiyo kutaifisha fedha ambazo zimepatikana kwa njia haramu na kufichwa katika benki za huko.

Muswada huo unaoitwa kwa lugha ya Kiingereza `Freezing and Restitution of Assets of Politically Exposed Persons obtained by Unlawful Means Bill’ ulisomwa kwa mara ya kwanza kwenye Bunge la nchi hiyo mwezi Mei, mwaka huu.

Graf alisema faida nyingine ya Tanzania kusaini mkataba huo ni kuwa, itaweza kuwatoza kodi Watanzania hao walioweka fedha huko.

Alifafanua kuwa siyo fedha zote zinazowekwa kwenye benki za Uswisi kuwa ni haramu kwani kuna nyingine zimepatikana kihalali, lakini zinaweza kutozwa kodi.

“Tanzania inakosa kodi kutokana na fedha zilizohifadhiwa na Watanzania wenye akaunti kwenye benki za Uswisi,” aliongeza Graf, ambaye alichaguliwa kuwa Rais wa nchi hiyo Novemba 26, 2012 na kutakiwa kukaa madarakani kwa mwaka mmoja.

Graf alisema pia fedha za kodi zingeisaidia Tanzania kugharimia sekta mbalimbali za maendeleo.


Zito aitupia lawama Serikali

Naye Waziri Kivuli wa Fedha, Zitto Kabwe, ambaye yuko nchini Uswisi akifuatilia masuala ya utoroshaji fedha na kufichwa kwenye benki za huko, alisema kuwa wakati shinikizo la dunia sasa limeelekea kumaliza tatizo la ukwepaji kodi na utoroshaji wa fedha kutoka nchi za Afrika, lakini Serikali ya Tanzania inasuasua juu ya kupambana na jambo hilo.

Zitto alisema katika taarifa yake kwa vyombo vya habari kuwa moja ya njia ya Serikali za nchi maskini kupata taarifa za kampuni kubwa za kimataifa yanayokwepa kodi ni mfumo wa kupashana taarifa unaoitwa kwa lugha ya Kiingereza `automatic exchange of tax information’.

“Kutokana na shinikizo la nchi mbalimbali, hivi sasa nchi zinazoitwa `tax havens’ (nchi zinazohifadhi fedha kwa siri) fedha zimeanza kuweka sahihi makubaliano ya kutoa taarifa,” alisema Zitto, ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema).

Alisema kuwa Tanzania mpaka sasa haijaweka saini na Serikali haijatoa taarifa yoyote kwa umma juu ya sababu ya kutokufanya hivyo. “Ghana, Afrika Kusini na Nigeria nchi zinazotegemea sana rasilimali kama Tanzania zimeweka saini mkataba huu tayari,” aliongeza Zitto.Alisema asilimia 44 ya fedha za kigeni inazopata Serikali ya Tanzania zinatokana na mauzo ya madini nje. Kampuni za madini ndizo zinazoongoza kukwepa kodi.

Alisema Tanzania inapoteza jumla ya Dola 500 milioni (Sh783 milioni) na Dola 1.25 bilioni (Sh2 trilioni) kwa mwaka kutokana na kampuni kubwa za kimataifa kukwepa kodi.

“Hii ni sawa na kusema Tanzania inapoteza Dola2 milioni (Sh3.1 bilioni) kila siku kwa uporaji huu,” alisema Zitto.

Zitto alisema Serikali lazima ichukue hatua mara moja kuhakikisha Tanzania inaingia makubaliano ya kupashana taarifa za kikodi.

Jaji Werema agoma kujibu

Alipoulizwa juu ya Tanzania kutokusaini mikataba ya kimataifa ya kubadilishana taarifa za utoroshaji fedha na mambo au kodi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema alisema hawezi kujibu suala hilo.

“Muulize huyo aliyekwambia kuwa Tanzania haijasaini mikataba ya kubadilishana taarifa za utoroshaji fedha na masuala ya kodi. Naomba uniache nifanye kazi zangu,” alijibu Jaji Werema kwa mkato na kukata simu.

Mahojiano kamili na Rais wa Uswisi, soma Mwananchi Jumapili.

CCM WASUTANA DODOMA-WANYOOSHEANA VIDEOLE MATUMIZI YA PESA


*Mada ya rushwa yaibua malumbano Dodoma
*Wagombea wanyoosheana vidole matumizi ya fedha
BAADHI ya wanasiasa wanaotajwa kutaka kuwania ukuu wa dola mwaka 2015 kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM ), sasa wanadaiwa kusababisha malumbano makali kando ya semina ya mafunzo ya utendaji, yanayowahusisha Wenyeviti na Makatibu wa wilaya na mikoa wa chama hicho, iliyomalizika jana mjini Dodoma. 

RAI limedokezwa kuwa malumbano hayo yametokana na kitendo cha baadhi ya wanasiasa kuitumia semina hiyo kama njia ya ushawishi kwa kutoa rushwa ili kujijengea mazingira ya kuteuliwa kuwa wagombea urais katika uchaguzi mkuu wa 2015, hali iliyowaibua baadhi ya makada wa chama hicho ambao wamewanyooshea vidole vigogo hao.

Habari zilizolifikia RAI kutoka ndani ya semina hiyo iliyohitimishwa jana na Rais Jakaya Kikwete mjini Dodoma, zimeeleza kuwa baadhi ya wajumbe, waliwashambulia kwa maneno makali makada wenzao kuwa tamaa yao ya uongozi inayowasukuma kutumia fedha nyingi kutafuta uungwaji mkono, inakichafua chama.

Mmoja wa wajumbe wa semina hiyo aliyezungumza na gazeti hili (jina lake tunaliifadhi) alisema kuwa, yaliibuka malumbano makali wakati mmoja wa mawaziri vijana na kada wa CCM mwenye ushawishi kwa vijana alipokuwa akiwasilisha mada yake iliyohusu mwelekeo wa CCM na taswira ya wapiga kura katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015.

Inaelezwa kuwa katika mada hiyo, Naibu Waziri huyo kijana alieleza namna CCM kilivyoanza kupoteza mwelekeo na mvuto kwa wapiga kura kwa sababu ya uwepo wa makundi ya wanachama wake wanaotumia fedha kusaka uongozi.

Mtoa habari huyo alieleza kuwa kauli ya waziri huyo ambaye pia amekuwa akitajwa kuendesha mikakati ya chini kwa chini ya kutafuta uungwaji mkono kwa ajili ya kuwania urais 2015, iliibua malumbano kando ya ukumbi wa semina na baadhi ya wajumbe wakimnyooshea kidole kuwa hata yeye anatuhumiwa kutumia fedha katika harakati zake.

Kwa mujibu wa mtoa taarifa wetu, baadhi ya wajumbe walihoji alikopata uhalali wa kuzungumzia jambo hilo ili hali yeye mwenyewe ameutumia mkutano huo kugawa rushwa ya Sh 50,000 kwa makatibu 50 na wenyeviti 50 wa baadhi ya mikoa na wilaya.

Haikufahamika mara moja waziri huyo kijana alikotoa fedha hizo, lakini taarifa zaidi kutoka ndani ya semina hiyo zinaeleza kuwa kuna idadi kubwa ya wapambe wa watu waliokwishaonyesha nia ya kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao, ambao wamekuwa wakijipitisha kwa wajumbe wa mkutano huo na kuwagawia fedha.

RAI limetajiwa majina ya vigogo wawili wa CCM wenye asili ya Kanda ya Ziwa ambao wapambe wao wameonekana wakiwapatia bahasha za kaki baadhi ya wajumbe ambao baada ya kuzifungua wamekaririwa wakieleza kukuta fedha ndani.

Mmoja wa vigogo hao anatajwa kuwa ni waziri mwandamizi katika Serikali ya Rais Jakaya Kikwete, naye anamtumia mmoja wa wabunge wa mkoa wake kugawa kiasi cha Sh 200,000 kwa wajumbe aliokwishawafikia.

Inaelezwa kuwa mpambe huyo wa Waziri aliibua malalamiko kutoka kwa wajumbe wa Zanzibar, ambao hakuwapatia fedha na walipomhoji ni kwanini anawabagua katika mgawo huo, alijibu kuwa hakupewa majina yao lakini watu walio karibu naye wameeleza kuwa Wazanzibari hawapo kwenye mgao kwa sababu hawana nguvu ya ushawishi katika vikao vya uteuzi vya wagombea urais.

Mbali na waziri huyo, anatajwa pia aliyepata kuwa waziri katika moja ya wizara nyeti kabla ya kufanyika kwa mabadiliko ya baraza la mawaziri, ambayo yalimuacha pembeni kuwa naye ametuma wapambe wake katika semina hiyo ambao wamekuwa wakiwafikia wajumbe wa semina hiyo kwa kuwaomba wamuunge mkono katika nia yake ya kuwania urais mwaka 2015.

Wapambe hao wa mwanasiasa huyo kijana, ni wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) na pia walikuwa wabunge katika Bunge lililopita ambao wanawagawia wajumbe wanaowafikia bahasha zenye Sh 100,000 hadi Sh 150,000 ili kuhakikisha mgombea wao anaungwa mkono wakati utakapofika.


Jitihada za gazeti hili kumpata Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahiman Kinana kuzungumzia suala hilo, hazikufanikiwa baada ya simu yake ya kiganjani kuita muda mrefu bila kupokelewa.

CLUB ZA USIKU, MAMBO HUWA HIVI POMBE NA MZIKI VINAPOKOLEA


 Haya ndio Mambo ya Clubs Mziki na Pombe vinapokolewa ...Wengi hujikuta wanasaula kabisa kama picha zinavyoonyesha hapo juu na chini ...Je wewe Umeshawahi Shuhudia Vimbwanga kama hivi ukiwa club?

Friday, October 25, 2013

ANAYE SHITAKIWA PAMOJA NA PAPA MSOFE KWA MAUAJI AWACHOMA POLISI

Mshtakiwa Makongoro Nyerere anayekabiliwa na kesi ya mauaji pamoja na Mfanyabiashara maarufu Abubakar Marijan [50] maarufu kama Papaa Msofe, amedai mahakamani kuwa amebambikiwa kesi hiyo.

Kadhalika alidai kuwa mahakama ikipitia jalada la kesi hiyo itabaini kwamba amebambikiwa kesi hiyo.

Nyerere alitoa madai hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu jijini Dar es Salaam, Hellen Riwa.

“Mheshimiwa hakimu, mahakama ikilipitia jalada la kesi hiyo kwa umakini, utabaini kwamba mimi sikuhusika na mauaji, nimebambikiwa baada ya askari polisi kuniomba rushwa ya Sh. milioni 8... nilipowakatilia kuwapa wakaamua kunipa kesi hii,” alisema Nyerere.

Alidai kuwa pamoja na mawakili wa upande wa Jamhuri kuwa ni wasomi wazuri, lakini wanafanya mambo yao tofauti na elimu waliyonayo na wanasabisha ateseke mahabusu bila sababu.

Hakimu Riwa alisema kwa kuwa upande wa Jamhuri umedai upelelezi bado haujakamilika, kesi hiyo itatajwa Oktoba 31, mwaka huu na washtakiwa wataendelea kukaa mahabusu.

Katika kesi ya msingi, ilidaiwa kuwa washtakiwa wote kwa pamoja walimuua kwa makusudi Onesphory Kituli, kinyume cha kifungu cha 196 cha Kanuni za Adhabu sura ya 19 kama kilivyofanyiwa marekebisho mwaka, 2002. 

Ilidaiwa kuwa, Oktoba 11, 2011, nyumbani kwake Kituli, Magomeni Mapipa, wilayani Kinondoni washtakiwa walitenda kosa hilo. 


Hata hivyo, kwa mujibu wa Mwenendo wa Sheria ya Makosa ya Jinai (CPA), washtakiwa hawakutakiwa kujibu chochote hadi upalelezi utakapokamilika kesi yao itahamishiwa Mahakama Kuu Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam.

INASIKITISHA SANA! MTOTO AMBAYE NDUGU ZAKE WALITAKA AUAWE, AFARIKI DUNIA





INAUMA SANA! Yule mtoto ambaye Amani liliripoti kuwa ndugu wanataka auawe wiki iliyopita, Mwajuma Haji (16), amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar.

Mwanyuma alikuwa na ugonjwa wa kusinyaa na vipimo vya madaktari havikuonesha ugonjwa uliokuwa ukimsumbua, ingawa viungo vyake vyote vilikuwa vimesinyaa na kujikunja tangu alipozaliwa. Kutokana na tatizo hilo, baadhi ya ndugu walifikia hatua ya kutaka auawe kwa walichodai alikuwa mzigo kwa familia.
Akizungumza na mwandishi wetu kwenye mazishi ya mtoto huyo kijijini kwao Kimange, Wilaya ya Bagamoyo, Tatu alisema mwanaye alizidiwa kwa siku tatu mfululizo huku akiwa anapumulia mashine kabla mauti hayajamkuta. Alisema madaktari walijitahidi kwa hali na mali kuokoa maisha yake lakini ilishindikana kwani alikuwa akipumua kwa shida. “Mwanangu ameteseka sana dakika za mwisho kwani kwa siku tatu mfulululizo alikuwa akipumulia gesi tu mpaka Mungu alipomchukua,” alisema mama huyo. Katika mazishi ya mtoto huyo, waliokuwa karibu na mama Mwajuma ni majirani zake baada ya ndugu kuingia mitini.

Majirani wa karibu na mama Mwajuma waliliambia Amani kuwa wanasikitishwa na tabia za ndugu zake waliosusia msiba huo na kudai ndiyo tabia yao kwani kipindi Mwajuma alipokuwa hai walikuwa hawamjali hata walipomkuta akinyeshewa mvua hawakumuingiza ndani hadi mama yake alipofika. “Tabia za ndugu wa mama Mwajuma hazijaanza leo kwani walikuwa wakimtenga sana mtoto huyo kwa kuwa hata walipomkuta ananyeshewa na mvua walikuwa wakimuacha hadi mama yake arudi,” alisema jirani mmoja ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini.

ANNA MAKINDA"WABUNGE WASTAAFU WANA HALI NGUMU-HUJA OFISINI KUOMBA OMBA


Akiongea na Spika wa Bunge la Uswisi, Maya Graf, Spika Anne Makinda amenukuliwa akisema kuwa Wabunge wengi Wastaafu wana hali ngumu kiuchumi pindi wanapomaliza muda wao.
Yumkini Wabunge wetu wastaafu huwa na hali ngumu kiuchumi baada ya kustaafu, lakini, tafsiri zaweza kuwa nyingi. Si kwamba Waheshimiwa hao hawakuwa wabunifu walipokuwa Mjengoni. Yawezekana baadhi yao wanahangaika sasa kwa vile walikuwa waadilifu sana. Hawakuiba senti za Wananchi.
Kwa kuwasengenya hata waliokuwa waadilifu yaweza walio Mjengoni sasa na wanaojitahidi kuwa waadilifu nao kuanza kukata tamaa. kwamba, hakutakuwa na tuzo ya wao kuwa waadilifu, bali masimango.(P.T)
Kwamba wameitumikia nchi bila kufanya ujanjaujanja na hivyo mitaani kuonekana wako hoi. Maana, kwa mshahara wa kawaida wa Mbunge, kwa kweli kuwa na magari na nyumba za kifahari ni jambo gumu.
Tukumbuke Wabunge hao wana familia zao za watoto wa kuwasomesha , wana pia ndugu na jamaa wanaowategemea. Achilia mbali wananchi wa majimbo yao wenye kuwataka misaada kila kukicha.
Hapa Mbunge mwadilifu kwa kiwango kikubwa hawezi kumaliza kipindi chake akiwa tajiri.
Haya, kwa masengenyo haya, Spika Makinda hatawaona tena Wabunge wenzake Wastaafu wakifika kwa wingi ofisini kwake. Maana, hata wale waliokuwa wakitaka kupita tu kumsabahi Spika, na hata kumpa ushauri wa hapa na pale, nao huenda wataogopa kuonekana ni 'omba omba'.
Na kwa Wabunge hao wastaafu nitawakumbusha wimbo wa kwenye Lizombe, ngoma ya Wangoni, na wanaweza kuingiza maneno yao wakipenda, usikike hivi; ...
" Tulipokuwa Mjengoni wee, Spika hakutusemaa..
Tumeondoka kidogooo, nyuma anatusengenyaa... Weee!"
Naam, dhiki haina mwenyewe!
Maggid.

Dar es Salaam.


DINI YA AJABU YAANZISHWA MBEYA INAABUDU MUNGU ILA UCHAWI, POMBE NA UZINZI RUKSA


Habari Wadau:

Dini inayoamini katika MUNGU lakini ikiruhusu yale ambayo dini zingine zinapinga imeanzishwa eneo la mji mdogo wa Makongolosi wilayani Chunya mkoani Mbeya,

Dini hiyo haiamini katika kutoa sadaka bali inasema tunamtolea nani sadaka wakati Vitu vyote tulivyonavyo ni mali ya MUNGU,kwa nini tunampa MUNGU mali zake Mwnyewe.!

Dini hiyo inaruhusu ulevi,uchawi na uzinzi kwa sababu vimeumbwa na MUNGU,Vile vile inaamini hakuna dhambi duniani,Dini hiyo inaitwa DIMAYO, sasa imeanza kuenezwa Mbeya

=========================
Ufafanuzi
=========================

Quote By GAMBISHI DWESE View Post
Yawezekana kweli Bwana Domy umekutana nami. Mimi Ndiyo PAPA-DIMAYO 1: GAMBISHI DWESE,( nabii wa kwanza wa DIMAYO) hata hivyo pengine umeninukuu kimakosa.Kwanza kabisa Dimayo haiamini katika uwepo wa mungu muumbaji aliye hai wala aliyekufa anayedaiwa kuhusika na kila kinachoendelea ulimwenguni.

Na nimeshatoa kitabu kinachoitwa HAKIKA HAKUNA MUNGU MUUMBAJI ALIYE HAI WALA ALIYEKUFA anayehusika na kila kinachoendelea. kijitabu hiki kinaeleza kinagaubaga kwanini Dimayo haiamini katika uwepo wa mungu muuumbaji. nikipata nafasi nitakiingiza kwenye mtandao ili watu wengi wakisome.

Ni kweli hakuna kitu Dhambi bali kuna makosa. na kosa linaweza kuwa kosa kulingana na mazingira na wakati katika jamii tofauti. Na ni kweli kwamba dini yetu ni ya starehe wala si ya mateso, maana tunaamini hakuna maisha zaidi ya haya tuliyonayo. Dimayo haijampa mtu ruksa ya kuvunja kanuni halisi asili wala sheria halali ya serikali yake halali na wala haina upotoshaji hata kidogo. 

Kinachoitwa sadaka kwetu huwapa watu wenye matatizo. Ni kweli kuna michango mingine lakini ni ya hiari na ni kwa ajili ya ushirika. Ni kweli kwenye JUMADI (jumba la makutano la Dimayo kutakuwa na kaunta ya vinywaji). unajua kunywa na ulevi ni vitu viwili tofauti; ulevi ni tabia ya mtu ya kutumia vileo kupindukia, lakini kwetu tunasema kunywa uwezavyo ilimradi huumii wala kuumiza vyote kisaikolojia na kimwili, kwa mantiki hiyo ulevi kwetu noma ila unywaji ni safi.


Uchawi ni sayansi, ila utumike kwa faida siyo kwa kuleta madhara. kuwaambia watu eti acheni ngono eti mungu hapendi wataacha?. wambie wafanyeje ngono kulingana na wakati na mazingira. Dimayo inamfundisha mtu kutenda inavyofaa yanayofaa kutendwa kwa kufuata kha na kahaka. Anyway nashukuru kwa kuianzisha mada hii, nafikiri nitachukua nafasi kuielezea zaidi kila inavyowezekana. Nina uhakika kwa mtu yeyote mwenye uwezo mkubwa wa kutumia akili zake hawezi kupingana hata kidogo na DIMAYO.
JF

KUMBE MSHAHARA WA RAIS WA TANZANIA SI KITU ONA MARAIS WENGINE WANAVYOLIPWA-KUFURU


Rais wa Marekani analipwa Dola 400,000 (Sh 640 milioni) kwa mwaka, sawa na Sh 53.3 milioni kwa mwezi. 

Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma analipwa Randi 2 ,917 038 sawa na zaidi ya Sh400 milioni za Kitanzania kwa mwaka, 

Rais wa Ufaransa, Francois Hollande Sh475 milioni, 

Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron Sh338 milioni, 

Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya Sh277 milioni na Rais wa Namibia, 

Hifikepunye Pohamba Sh226 milioni kwa mwaka. 

Wengine na malipo wanayopata kwa mwaka ni Marais wa Urusi, Vladimir Putin, Sh174 milioni, 

Ellen Johnson Sirleaf wa Liberia Sh137 milioni,

Michael Satta wa Zambia, Sh126 milioni, 

Rais wa Angola, Jose dos Santos Sh91 milioni, 

Rais wa Lesotho, Profesa Pakalitha Mosisili Sh88 milioni, 

Armando Guebuza wa Msumbiji, Sh84 milioni na 

Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Xi Jinping Sh60 milioni. 

Wengine ni Rais wa India, Pranab Mukherjee Sh49 milioni, 

Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe Sh27 milioni,

Naibu Rais wa Afrika Kusini, Kgalema Mothlanthe Sh331 milioni, Waziri Mkuu wa Namibia, Nahas Angula Sh160 milioni.


Ok kumbe Mshahara wa Rais wa bongo bado ni mdogo sana kulinganisha na mishahara ya Marais wenzake hapa Africa na Duniani, Mheshimiwa Zitto my hero kwenye hili hakumtendea haki Rais wetu alipotoa hadharani Mshahara wa Rais wetu ambayo nia na madhumuni yake ilikuwa kuonyesha kwamba analipwa mahela mengi sana, alitakiwa kutuonyesha pia na mishahara ya Marais wengine na vipato vya Taifa pia, kwa sababu as a nation tuna pato kubwa sana kuliko nchi nyingi zingine ambazo Marais wao wanalipwa mahela ya ajabu kulinganisha na Rais wa bongo.


- Piwa ifahamike wazi kwamba hata leo Rais wa Jamhuri akitokea Chadema, bado mshahara wake utakuwa ni huo huo unless akigoma na kutaka upunguzwe, kitu ambacho historia ya chama hicho na Mishahara au posho za Taifa haiko kabisa upande wao, kuna wakati walidai posho ya wabunge ni kubwa sana lakini mpaka leo hatujasikia wakiomba kupunguziwa, walilalamika kuhusu hela za magari ya wabunge lakini mpaka leo hawajagomea kupokea hela hizo, Mwenyekiti wao alilalamikia magari ya kifahari ya wabunge na yeye mpaka leo anatumia gari hilo hilo alilolalamikia!
-Wiliam Malecela

AIBU:CHANGU DOA AMUUMBUA MUME WA MTU BAADA YA KUFANYA NGONO KWENYE GARI




Stori: Musa Mateja


OKTOBA 19, 2013 ilikuwa  ya aibu kwa mmiliki wa gari aina ya Toyoya Noah kufuatia kuangushiwa varangati na kahaba ambaye jina lake halikupatikana mara moja baada ya mmiliki huyo ambaye ni mume wa mtu kula naye uroda kisha kutaka kumfanyia kitu mbaya.

Tukio hilo lililojaza watu kibao, lilitokea usiku wa saa 5:19 Jumapili iliyopita ambapo kikosi cha Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ kikiwa katika ‘patroo’ ya kunasa matukio ya usiku.
Ilikuwa wakati OFM wakipita eneo hilo, walikuta umati ukiwa umelizunguka gari hilo huku kahaba huyo akianika ya ‘chumbani zaidi’.

Alisema: (huku ameshika jiwe) nakwambia sikubali, huwezi kunifanyia hivi. Wewe umelala na mimi kwenye gari kule halafu unakuja hapa unanitenda hivi? Jaribu kuondoa gari uone nitakavyovunja vioo.

OFM: Kwani dada ilikuwaje?

Kahaba: (huku akilia) Huyu baba amelala na mimi kule (hakutaja jina) tena ndani ya gari lake, si angalieni muone kile kiti cha upande wa abiria kilivyolala. Tumemaliza, tumekuja wote kufika hapa akanisukumia nje, nikaangukia nje na kuumia mkono. Ndiyo nikaokota jiwe ili nivunje vioo vya gari lake.

Mume wa mtu: Sasa wewe unapiga kelele za nini? Elfu kumi yako si nimekupa? Unataka nini tena, au lengo lako kunivunjia heshima?
Kahaba: Umenipa ndiyo, nataka hela ya kwenda kujitibia huu mkono ulioniumiza, nataka matibabu tu mimi.

Kahaba huyo alionesha sehemu ya mkono inayovuja damu. Aliumia baada ya kuanguka kwa kusukumwa na mwanaume huyo. 
Mwanaume huyo alitaka kuondoka kwa kuwasha gari, lakini OFM wakamzuia wakimtaka asubiri polisi kwa vile msichana huyo aliumia kiganja cha mkono wa kushoto.

Mume wa mtu: (huku akimnong’oneza sikioni OFM) jamani sikieni, tumalizane kiume. Unajua mimi nina mke na watoto, sasa kusubiri polisi hamuoni kama nitaumbuka mwenzenu?

OFM: Hamna, haatungumzii biashara yenu mliioifanya ndani ya gari, hapa tunasimamua majeraha ya mkono uliyomsababishia. 

Mashuhuda mbalimbali nao waliunga mkono OFM kwamba, mwanaume huyo asiondoke mpaka polisi wafike kushughulikia tatizo lao.


Ndipo mwanaume huyo bila kujua anaoongea nao ni OFM, alisema:

“Sawa, tusubiri polisi lakini no media (akimaanisha amekubali kusubiri polisi lakini kusiwepo wanahabari).
OFM: Ndiyo, no media, lakini polisi wanakuja sasa hivi.
Ndani ya dakika saba, mwanaume huyo alishangaa akipigwa picha na paparazi mmoja wa OFM aliyeliwahi tukio akitokea Sinza-Makaburini, Dar alikokuwa akifanya kazi nyingine za OFM.

Alipoona mwanga wa kamera ukimmulika mara kadhaa, mwanaume huyo aliingia ndani ya gari na kuondoka kwa kasi huku wananchi wakimzomea.

Cha ajabu, kahaba huyo naye alipoona mwanga wa kamera alianza kuondoka huku akisema haogopi kupigwa picha. 

Thursday, October 24, 2013

KTN’S MOHAMMED ALI OF JICHO PEVU AND JOHN ALLAN NAMU HAVE BEEN SUMMONED BY CID OVER KDF XPOSE


KTN’s top investigative journalists Mohammed Ali of Jicho Pevu and John Allan Namu of the Inside Story have been summoned by Criminal Investigative Department (CID) today , to shed more light on how Kenya Defence Forces (KDF) looted at Westgate Shopping Mall and how the terrorists escaped as purpoted by their famous Jicho Pevu investigation . According to police sources, the two who released a clip showing KDF soldiers looting and drinking beer will be questioned on how they accessed the clip which has damaged the reputation of KDF. 


According to Jicho Pevu all the terrorists escaped after KDF went for a looting exercise and up to now police are y et to arrest anybody who was directly linked to the attack where over 7 0 people died and hundreds injured. In their expose, Mohammed and Namu said KDF tried all means including bringing down the building and destroying things in the mall to hide the evidence of looting. More to follow…

YANGA YAUA TAIFA, SIMBA YASHIKWA SHARUBU TANGA


Wachezaji wa Simba SC, Haruna Shamte (kushoto) na Joseph Owino wakijadiliana jambo baada ya sare ya 0-0 dhidi ya Coastal Union leo kwenye Uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga. (Picha na Richard Bukos / GPL,TANGA).

Yanga SC leo imeweka kimbindoni pointi tatu baada ya kuichabanga mabao 3 - 0 timu ya Rhino Rangers kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Mabao ya Yanga yamefungwa na Hamis Kiiza aliyefunga mawili katika dakika ya 12 na 81 wakati lingine likifungwa na Frank Domayo mnamo dakika ya 72.


Wakati Yanga wakitoka vifua mbele leo, watani wao Simba SC wao wameshikwa sharubu baada ya kulazimishwa sare ya 0 - 0 na Coastal Union ya mkoani Tanga. Mechi hiyo imepigwa katika Uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga.

WATANZANIA 3 WATIWA MBARONI WAKIWA NJIANI KWENDA KUJIUNGA NA AL-SHABAAB NCHINI SOMALI



Jeshi la Ulinzi la Kenya liliwatia mbaroni Watanzania watatu ndani ya Somalia wakiwashuku kuwa walikuwa njiani kwenda kujiunga na Al-Shabaab, gazeti la The Standard la Kenya liliripoti siku ya Jumapili (tarehe 20 Oktoba).

Ali Ramadhan mwenye umri wa miaka 22, Musa Daudi miaka 19 na Shabaan Bakiri Waziri miaka 21, walitiwa mbaroni baada ya kuingia Somalia kutoka Kenya na sasa wanahojiwa katika kituo cha polisi cha Kiunga.

Polisi walisema kwamba washukiwa hao walitokea Dar es Salaam, wakasafiri hadi mpaka wa Tanzania na Kenya huko Lungalung, baadaye wakaenda kwa gari hadi Mombasa, Malindi na Lamu kabla ya kuingia Somallia.

Kwa mujibu wa polisi, watatu hao walikuwa wanaelekea Kismayu kwenda kujiunga na "vita vitakatifu, walivyodai vinaongozwa na [Al-Shabaab]".

JOKATE:MH! DIAMOND ANAPENDA KUZAA,SIO KWANGU TU WANAWAKE WAKE WOTE HUWA NASIKIA ANATAKA KUZAA NAO


MTANGAZAJI maarufu Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ amefunguka kuwa aliyekuwa mpenzi wake, Nasibu Abdul ‘Diamond’ alitaka wazae kipindi walipokuwa wapenzi.
Jokate alifunguka hayo juzikati alipokuwa akifanya mahojiano maalum na mapaparazi wa Global Publishers, pamoja na kufunguka mengi, alibainisha kuwa Diamond huwa anapenda watoto kwenye uhusiano.

“Mh! Diamond anapenda kuzaa, tena siyo kwangu tu wanawake wake wote huwa nasikia anataka kuzaa nao,” alisema Jokate.

Monday, October 21, 2013

BUKOBA FLOW ZONE: Solo Thang kudondosha single mpya "Mdudu" October ...

BUKOBA FLOW ZONE: Solo Thang kudondosha single mpya "Mdudu" October ...: October 25,mkali wa lyrics na vina,Solo thang anatarajia kuachia historia nyingine this time inaonekana akiwa na Mr Blue. Single in...

Solo Thang kudondosha single mpya "Mdudu" October 25

October 25,mkali wa lyrics na vina,Solo thang anatarajia kuachia historia nyingine
this time inaonekana akiwa na Mr Blue. Single inaitwa "Mdudu" kaa mkao mzuuri wa kuisikiliza. Definately is gonna be the bomb 

Yanga watangulia lakini je walifika?

Baadhi ya mashabiki walizima kwa mshangao wa kilichokuwa kinaendelea uwanjani
Ama kweli kutangulia si kufika,au kama wanavyosema wakongomani kuwa KOKENDE LIBOSO,EZA KOKOMATE.
Usemi huo ulidhihirika hapo jana kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam baada ya Mabingwa watetezi Ligi kuu soka Tanzania Bara Timu ya Yanga,pamoja na kutangulia kufunga bao 3 dhidi ya Simba hadi mapumziko,walijikuta wakiambulia sare ya bao 3-3 hadi Mwisho wa mchezo baada ya Simba kusawazisha bao zote katika Kipindi cha Pili.
Huku Simba wakiwa wamepoteana hasa idara ya Ulinzi,ilianza kuruhusu wavu wake kutikishwa katika dakika ya 14 baada ya Mchezaji wake wa msimu uliopita Mrisho Ngasa kutia chuma wavuni kufuatia pasi ya Didier Kavumbagu.
Lango la Simba lilikuwa matatani tena katika dakika ya 35 pale Mganda Khamis Kiiza alipoandika bao la pili kwa shuti la mguu wa kulia baada ya mpira uliorushwa na Mlinzi Mbuyu Twite kuparazwa kichwa na Didier Kavumbagu kabla ya kumkuta Mfungaji aliyeujaza wavuni.
Mganda huyo Khamis Kiiza almaaruf Diego aliandika bao la tatu kwa Yanga sekunde chache kabla ya Mapumziko kufuatia kazi nzuri ya Haruna Niyonzima alieyekokota mpira na kumpasia Didier Kavumbagu ambaye naye alimsogezea Mfungaji.
Huku Mpira ukienda Mapumziko Yanga wakiongoza kwa bao 3-0 ,baadhi ya mashabiki wa Simba walianza kuondoka uwanjani kwa kukata tama hasa kutokana na kiwango duni cha mchezo kilichoonyeshwa na timu yao,huku Mashabiki wa Yanga wakishangilia na kuwadhihaki Simba kwa kuonyesha kuwa wangeweza kulipiza kichapo cha bao 5-0 walichoshushiwa na Simba mwaka jana kwenye uwanja huo huo wa Taifa.
Kipindi cha Pili kilianza kwa Simba kuwapumzisha Abdul halim Humoud na Haroun Chanongo na kuwaingiza Said Ndemla na William Lucian,katika idara ya Kiungo,mabadiliko ambayo kwa kiasi kikubwa ndiyo hasa yaliyobadili sura ya mchezo baada ya idara ya kiungo ya Yanga kuanza kuzidiwa na kasi ya vijana hao ambapo katika dakika 53 Betram Mwombeki aliipatia Simba bao la kwanza baada ya pasi ya Mrundi Khamis Tambwe.
Dakika tatu baadae Mpira wa Kona uliopigwa na Ramadhan Singano ulimkuta Joseph Owino ambaye aliujaza wavuni na kuipatia Simba bao la Pili lililozidi kuwapa morali wachezaji na mashabiki waliokuwa wameamka upya.
Hatimaye Simba wakaweza kusawazisha katika dakika ya 83 kufuatia Beki Kaze Gilbert kujitwisha mpira wa adhabu ndogo uliopigwa na Mlinzi Nassor Masoud Chollo.
Kwa Matokeo hayo Simba sasa inashika nafasi ya tatu kwa kuwa Pointi 19 nyuma ya Azam na Mbeya City zenye pointi 20 kila moja lakini Simba imecheza mechi moja pungufu.
Nao Mabingwa watetezi Yanga wako nafasi ya nne kwa kuwa na pointi 16.
Hakika lilikuwa Pambano ambalo Yanga walijiamini kuwa wameshinda kwa kutangulia kuongoza bao 3-0 ambalo si kawaida katika mechi za watani hao wa jadi katika Soka la Tanzania,na ndiyo Maana Simba walishangiliwa kwa nguvu kana kwamba wameshinda baada ya Kutoka nyuma na kusawazisha bao tatu.
Kwa upande mwingine mashabiki wengi walianguka na kuzimia ama kwa kushangilia matokeo au mshtuko kutokana na kutoamini kilichokuwa kinaendelea uwanjani hapo.
Kwa upande mwingine kukamilika kwa mechi hiyo kunafanya maisha yaendelea kama kawaida baada ya tambo za kila upande kwa takriban zaidi ya wiki moja ambapo mashabiki wa pande zote walikuwa wakitambiana kuwa kila mmoja timu yake ingeshinda Pambano hilo ambalo kwa kawaida huwagawanya mashabiki wa nchi hii pande mbili.

Wahalifu wa DRC hawakupelekwa mahakamani

Wanajeshi wa serikali ya Congo
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Demokrasi ya Congo unasema unasikitika kuwa watu waliofanya ukatili katika mji wa Minova mwaka jana hawakufikishwa mahakamani.
Umoja wa Mataifa unasema una ushahidi wa kesi 135 za ubakaji pamoja na mauaji na wizi wa ngawira uliofanywa katika eneo la Minova mwezi Novemba mwaka jana.
Ulilishutumu jeshi la Congo kufanya uhalifu huo.
Inaarifiwa maafisa 12 wa jeshi la Congo walisimamishwa kazi kwa muda, lakini Umoja wa Mataifa unasema hakuna aliyefikishwa mahakamani.Wanajeshi wa serikali ya Congo

Wanafunzi wapambana na polisi Cairo

Mapambano mjini Cairo
Polisi wa Misri wamefyatua moshi wa kutoza machozi kuvunja maandamano mjini Cairo, ya wanafunzi wanaomuunga mkono rais wa zamani, Mohamed Morsi.
Mawe yalirushwa na pande zote mbili huku wanafunzi mia kadha wakijaribu kutoka chuoni kuelekea Medani ya Rabaa, pahala pa kambi ya wafuasi wa Morsi ambayo ilifungwa na wakuu miezi miwili iliyopita.
Hii ni siku ya pili ya mapambano katika Chuo Kikuu cha Al-Azhar, ambako kuna wafuasi wengi wa chama cha Muslim Brotherhood cha Bwana Morsi.
Bwana Morsi aliondolewa madarakani na jeshMapambano mjini Cairoi mwezi wa Julai.                                     

Je wanajeshi wa Kenya walipora Westgate?


Mmoja wa wanamgambo wa Al Shabaab wanaosemekana kuuawa kwa shambulizi la Westgate
Picha za wanajeshi wa Kenya waliokwenda katika jumba la Westgate katika juhudi za uokozi na kisha baadaye kuonekena kwenye kamera za CCTV wakiondoka na mifuko ya plasitiki yenye bidhaa za madukani, bila shaka zimewashangaza wengi.
Picha hizo mwanzo zimeonyesha wanajeshi wakiingia ndani ya jengo hilo wakiwa wamebeba silaha kukabiliana na wanamgambo walioshambulia jengo hilo wiki nne zilizopita na baadaye wakitoka wakiwa wamebeba mifuko hiyo wakiwa na silaha zao kwa wakati mmoja.
Hata hivyo haijulikani walichokuwa wamekibeba kwenye mifuko hiyo .
Pamoja na picha za wanajeshi wakiwa wamebeba mifuko, pia kulikuwa na picha zengine zilizoonyesha mashine ya pesa zikiwa zimeporwa ndani ya mikahawa huku picha za alama za risasi kwenye maeneo ya kuhifadhia pesa, pia zikionekana.
Inaarifiwa ilikuwa jaribio ya kufungua hifadhi hizo ambalo halikufanikiwa.
Madai haya ya wanajeshi kufanya uporaji wa maduka katika jingo hilo, yalikanushwa vikali na jeshi la Kenya kiasi cha kutaka hatua kuchukuliwa dhidi ya waliokuwa wanatoa madai hayo, lakini haijulikani jibu lao litakuwa nini hasa kwa picha hizo za CCTV zilizoonyesha wanajeshi hao wakifanya uporaji.
Wamiliki wa maduka waliorejea kwenye maduka yao bbaada ya shambulizi , walidai kuwa maduka yao yaliporwa ingawa jeshi lilikanusha madai hayo baadhi ya taarifa zikisema kuwa ilikuwa njama ya wafanyabiashara kudai fidia kwa mali zao zilizoharibika.
Sio wanajeshi pekee waliotuhumiwa kwa uporaji, kwani polisi mmoja naye alifikishwa mahakamani kwa kosa la uporaji baada ya kupatikana na pochi la mtu liliokuwa na damu.
Wangambao wa Al Shabaab waliteka nyara jengo la Westgate kwa siku nne na kusababisha vifo vya watu 60 pamoja na kuwajeruhi zaidi ya watu miamoja.

Boko Haram waua madereva 19 Nigeria

Mabaki ya magari ya madereva waliouawa na Boko Haram
Wanamgambo waliokuwa wamevaa nguo za kijeshi, wamewaua watu 19 katika kuzuizi cha barabarani walichokuwa wameweka kukagua magari katika jimbo la Borno.
Wanaume hao waliokuwa wamejihami , waliwasimamisha madereva na kuwaamrisha kuondoka kutoka katika magari yao kabla ya kuwapiga risasi na kuwaua.
Walioshuhudia tukio hilo waliambia BBC kuwa wanaume hao walikuwa wanachama wa Boko Haram, ingawa kundi hilo bado halijatamka chochote kuhusu mauaji hayo.
Jimbo hilo la Kaskazini mwa Nigeria liko chini ya sharia ya hali ya hatari, huku Boko Haram wakiwa vitani na serikali kutaka utawala wa kiisilamu.
Kundi hilo huwalenga raia na wanajeshi kwa mashambulizi ikiwemo shule na makabiliano ya mara kwa mara na jeshi la taifa.
Shambulizi la hivi karibuni, lilifanyika Jumapili, asubuhi karibu na mji wa Logumani, ambao hauko mbali sana na mpaka na Cameroon.
Walionusurika shambulizi hilo walisema kuwa washambuliaji walivaa nguo za jeshi na walikuwa wanaendesha pikipiki kabla ya kuwashambulia waathiriwa.
"Takriban wanaume 9 walituamuru kuondoka kwenye magari yeu na kulala chini,’’ alisema mwanamume
"Waliwaua watu 5 kwa kuwapiga risasi na kasha kuwanyonga wengine 14 kabla ya mtu mmoja kuwapigia simu na kuwambia kuwa wanjeshi wanakuja.’’
Alisema washambuliaji baadaye walitoroka na kujificha msituni kwa pikipiki zao.
Manusura mwingine alisema kuwa alisikia mtu aliyekuwa karibu naye akiuawa kwa kisu. Alisema ana uhakika kuwa washambuliaji walikuwa Boko Haram kwa sababu ya kuwa na ndevu.
Mwandishi wa BBC Tomi Oladipo alisema kuwa ni jambo la kawida kwa polisi kuweka vizuizi barabarani hasa katika maeneo yenye misukosuko na huenda washambuliaji waliiga mbinu hioyo ya jeshi ili kuwanasa waathiriwa. I,
Boko Haram limezua mgogoro mkubwa wa kisiasa Nigeria tangu mwaka 2009, nia yao kuu ikiwa kuunda utawala wa kiisilamu, hasa katika maeneo ya kaskazini mwa nchi
Kundi hilo limelaumiwa kwa mashambulizi kadhaa ambao yamesababisha takribna vifo 2,000 tangu mwka 2011.

HATIMAYE JICHO PEVU WATOA VIDEO YA MAKALA INAYOELEZEA UKWELI WA TUKIO LA WESTAGATE ANGALIA HAPA

Hayawi hayawi hatimaye yamekuwa, zimekuwa siku nyingi za kubashiri, na siku nyingi za kunongonezana kuhusu kilichojiri wakati taifa lilitekwa nyara na magaidi kwa siku nne mtawalia. Wakenya zaidi ya sitini walipoteza maisha yao katika jumba la Westgate lakini hadi sasa Wakenya hawajajua ukweli kuhusu yaliyojiri katika jumba la Westgate. Je ni kweli kuna waliokuwa wametekwa nyara na magaidi na kuzuiliwa katika jumba hilo? Je ni kweli kuna magaidi waliouawa na wanajeshi? Meza ya upekuzi ya Jicho Pevu na Inside Story usiku na mchana wamekuwa wakidurusu kila ukurasa na, kufanya mahojiano na kupitia hatua kwa hatua video za cctv kutoka jumba la Westgate na sasa wako tayari kukusimulia kilichojiri bila kuficha lolote. Meza hii ilifanikiwa picha za pekee kuhusu matukio ya Westgate. Usiambiwe tena tizama makala haya yatakayokujia katika muda usiokuwa mrefu ukiwanaye mwanahabari mpekuzi mohammed ali.

ZITTO KABWE KUSHITAKIWA KWA KUUTANGAZA MSHAHARA WA RAIS NA WAZIRI MKUU


HATUA ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe kutaja hadharani mshahara wa Rais na Waziri Mkuu, imechukua sura mpya baada ya Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) kulaani hatua hiyo na kuomba Spika Anne Makinda kuchukua hatua kwa vile ni ukiukaji wa sheria.
  
Chama hicho kimeeleza kusikitishwa na kitendo hicho kufanywa na Mbunge aliyehusika na upitishaji wa sheria hiyo huku wabunge wenyewe wakiwa wakali pale wananchi na wadau mbalimbali wanapohoji mapato yao.

Katibu Mkuu wa Tughe Taifa, Ally Kiwenge alisema Dar es Salaam jana kwamba pamoja na hatua hiyo kukiuka sheria ya kazi na uhusiano kazini inayosema mshahara ni siri ya mwajiri na mwajiriwa, pia kitendo hicho si ajenda ya wafanyakazi hivi sasa.
  
Alisema ajenda ya wafanyakazi kwa sasa ni kuona wabunge wanapigana kufa kupona katika kuhakikisha kuwa mshahara wa mfanyakazi unaongezeka kukidhi mahitaji ya mwezi mzima na kuwaondolea mzigo wa mikopo inayowaandama.
  
“Huu si wakati wa wafanyakazi kutaka kujua mishahara ya Rais au Waziri Mkuu, ajenda yetu kwa sasa ni kuona wabunge wanapigana ili kuboresha mishahara ya wafanyakazi ili ukidhi mahitaji muhimu tofauti na sasa,” alisema Kiwenge.

Alisema pamoja na hilo ni mkakati wa wafanyakazi sasa kuona wabunge wanatumia muda wao uliosalia kabla ya Bunge kuvunjwa kuhakikisha mambo makubwa mawili yanaingizwa katika Katiba mpya, moja ikiwa ni nafasi ya mfanyakazi kikatiba ikoje na pia kuona Katiba mpya inasema nini juu ya hatima ya maslahi ya wafanyakazi.
  
“Tunataka Katiba mpya itamke wazi juu ya mishahara ya wafanyakazi ili iwe ni ile inayokidhi haja,” alisema.

 Aeleza kuwa ni jambo la kusikitisha kuona wabunge wanaanza kutaja mishahara ya viongozi wa taifa hadharani kwa kudhani kuwa ndio njia sahihi ya kuwasaidia Watanzania bila kujua kuwa hatua hiyo itasababisha mgawanyiko wa matabaka na kuligawa Taifa, jambo ambalo ni la hatari.

“Sisi mishahara ya viongozi wote tunaifahamu na hata ya wabunge, lakini sheria inasemaje juu ya kutangaza mshahara wa mtu hadharani? Wafanyakazi wanaweza kuitaja lakini kwa vile wameandaliwa hawafanyi hivyo, wanazingatia sheria, kanuni na taratibu za nchi.
  
“Naamini kama wafanyakazi wangekuwa ni watu wa kukusanyana na wangekuwa hawana maadili wangeweza kusema mengi ambayo yangeshangaza jamii lakini hawafanyi mambo kwa kukurupuka au kuutafuta umaarufu usio na msingi,” alisema.
  
Katibu Mkuu huyo wa Tughe alisema kwa kufuata mfano wa wafanyakazi, viongozi wakiwemo wabunge watoe kauli za kujenga nchi na si zenye kuashiria matabaka na ubaguzi, jambo linaloweza kusababisha migogoro mikubwa na kuliingiza taifa katika machafuko yasiyo na tija,” alisema.
  

Alisema wabunge wafahamu pia kwamba suala la mishahara litaendelea kubakia kuwa ni la mwajiri na mwajiriwa na ndio maana katika fomu au nyaraka nyingine zinazoelezea majukumu ya wabunge suala la mishahara na marupurupu yao haliwekwi wazi kwa vile ni siri kati yao na taasisi ya Bunge kisheria.

Washambuliwa wakitoka kanisani Misri

Waumini walishambuliwa wakiwa wanatoka kanisani
Watu watatu akiwemo msichana mdogo mwenye umri wa miaka 8 aliuawa wakati watu waliokuwa wamejihami wakiwa kwenye pikipiki kushambulia sherehe za ndoa nje ya kanisa la Kikopti mjini Cairo.
Takriban wengine 9 walijeruhiwa kwenye shambulizi hilo mjini Giza.
Hata hivyo hakuna taarifa zozote kuhusu nani aliyehusika na shambulizi hilo.
Jamii ya wakristo wa kikopti wamekuwa wakishambuliwa na baadhi ya waisilamu wanaotuhumu kanisa kwa kuunga mkono jeshi katika kumpindua aliyekuwa Rais Mohammed Morsi mwezi Julai.
Washambuliaji hao ambao hawakutambuliwa, waliwafyatulia risasi kiholela watu waliokuwa wanaondoka kanisani.
Mwanamume mmoja na mtoto huyo waliuawa nje ya kanisa hilo wakati mwanamke mmoja akifariki akipelekwa hospitalini.
"Tulisikia mlio mkubwa sana mfano wa kitu kilichokuwa kinaanguka,’’ alisema shahidi mmoja.
"Nilimkuta mwanamke mmoja akiwa ameketi kwenye kiti chake, akiwa amejeruhiwa kwa risasi. Watu wengi walikuwa wameanguka kando yake akiwemo mtoto mdogo.’’
Kasisi wa kanisa hilo Thomas Daoud Ibrahim alisema kuwa alikuwa ndani ya kanisa hilo, wakati, milio ya risasi ilikuwa inasikika.’’
"Kilichofanyika ni kitu kibaya sana na sio waksristio wakopti waliolengwa pekee yao , tunaharibu nchi yetu,’’ alisema kasisi huyo.
Kasisi mwingine aliambia vyombo vya habari kuwa kanisa hilo liliachwa bila polisi wala mlinzi tangu mwishoni mwa mwezi Juni.
Kanisa hilo ni moja ya makaisa ya zamani ya kikristo iliyoanzishwa mjini Alexandria mapema miaka ya 50 AD.
Idadi ya wakristo nchini Misri ni asilimia 10 ikiwa waumini milioni 80, na wamekuwa wakiishi kwa amani na waisilamu wa kisunni kwa miaka mingi.
Hata hivyo, kuondolewa mamlakani kwa Morsi kijeshi, kumefuatiwa na mashambulizi mabaya dhidi ya makanisa na rasilimali za waumini hao kwa miaka mingi.
Wakati mkuu wa majeshi Generali, Abdul Fattah al-Sisi, alitangaza kwenye televisheni kuwa rais Morsi aliondolewa mamlakani baada ya maandamano makubwa yakimtaka ajiuzulu aliandamana na papa Tewadros.
Tewadros alisema kuwa mkakati uliofikiwa na Al-asisi ulitokana na mawazo ya viongozi waheshimiwa ingawa hakuwataja.

Sunday, October 20, 2013

Wachezaji wa Zambia kukamatwa

Zambia ndio mabingwa wa kombe la mataifa ya Afrika mwaka 2012
Zambia imetoa vibali vya kukamatwa kwa wachezaji wake watatu waliokosa mechi ya kirafiki dhidi ya Brazil mjini Beijing China. Hata hivyo Zambia ilishindwa na Brazil mabao mawili kwa nunge.
Klabu ya DRC TP Mazembe ilisisitiza kuwa wachezaji hao Rainford Kalaba, Stoppila Sunzu na Nathan Sinkala walijeruhiwa na kusababisha mgogoro kati ya shirikisho la soka la Zambia na serikali ya Zambia.
Baada ya wachezaji hao kufanyiwa ukaguzi mjini Lusaka, shirikisho la soka la Zambia likasisitiza kuwa bado wanaweza kusafiri kwenda China kwa mchuano huo,lakini klabu ya Mazembe ambako wachezaji hao hucheza soka ya kulipwa ikawataka kurejea.
Hatua hiyo ilisababisha serikali ya Zambia kuingilia kati kwa kuwapokonya wachezaji hao pasi zao za usafiri ili kuwazuia kwenda kuchezea klabu yao mjini Lubumbashi.
Hata hivyo, wachezaji walifanikiwa kuvuka mpaka na wanaaminika kuwa nchini DR Congo.
Shirikisho la soka la Zambia limeandikia barua shirikisho la soka duniani Fifa, na kulalamika kuwa klabu ya Mazembe haikuwaruhusu wachezaji hao kushirki majukumu yao ya kimataifa.
Zambia ilishindwa kwenye mechi hiyo ya kimataifa mjini Beijing
Zambia ambao ni mabingwa wa kombe la taifa bingwa Afrika walikuwa wanashirki mechi yao ya kwanza wakiongozwa na kocha wao mpya Patrice Beaumelle, ambaye alichukua usukani siku nane zilizopita baada ya Herve Renard kucha kazi.