Friday, February 28, 2014

HUYU NDIYE MSICHANA ALIYEONGOZA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2013..AFUNGUKA MENGI


Tovuti ya Times Fm imefanya mahojiano ‘exclusively’ na Robina Nicholaus, msichana aliyeshika nafasi ya kwanza/ aliyeongoza kitaifa (Tanzania One) kwenye matokeo ya mtihani wa kidato cha nne mwaka 2013.

Robina, mwenyeji wa wilaya ya Bunda mkoa wa Mara ambaye alikuwa anasoma katika shule ya wasichana ya Marian, akiwa na ndoto ya kuwa daktari wa watoto amejibu maswali kumi muhimu na majibu yake yanaweza kuchukuliwa kama mfano wa kuigwa kwa wanafunzi walioko shuleni ambao wanakumbwa na changamoto kadhaa, na wazazi wanaowapeleka watoto wao shule.
Ulifanya nini ghafla ulipopata taarifa kuwa umekuwa wa kwanza Tanzania nzima, na je, ulitegemea?
 Nilipopata matokeo kwamba nimekuwa wa kwanza, kwanza nilifurahi sana na kilichobaki zaidi ilikuwa ni kumshukuru Mungu kwa sababu yeye ndiye kayawezesha yote. Nilihisi kama kupaa vile…nilifurahi sana halafu my mom alikuwa pale… alikuwa analia akaniinfluence na mimi machozi yatoke, I was very happy yaani. Sikutegemea kuwa wa kwanza lakini nilikua na uhakika wa kufanya vizuri kwa sababu niliplan kufanya vizuri.
Kama msichana ulifanya nini kuzivuka changamoto za kimasomo na kufanikisha kwa kiasi kikubwa? 
Safari ya taaluma ni ndefu ndio, kwenye safari ya masomo kuna changamoto za hapa na pale, ambapo mara nyingi wasichana waga tunafanya maamuzi ambayo sio sahihi. Lakini kwangu mimi nimeweka interest yangu sana kwa wazazi. Kwa hiyo nilikuwa open kwa wazazi na kuwaomba ushauri wa hapa na pale nifanye nini. Na katika vyote nilivyokuwa nafanya ni kufanya kile kitu ambacho hakiwezi kusubiria kwanza ambacho ni masomo. Kwa hiyo naweka juhudi pale ili ukishafanya kila mtu ajue kwamba umefanya.


Ilikuwa mbaya sana kwenye kusoma hasa form three ambapo nilianza kushuka and all that. Kwa hiyo wazazi pamoja na walimu pia walikaa na kuweza kunisaidia na mimi mwenyewe nilikuwa tayari kusikia ushauri wao na kuweza kusoma kwa bidii zaidi ili niweze kupata ile nafasi yangu niliyokuwa naipata toka nianze.

Nini kilichofanya ushuke kimasomo wakati huo?

 Kilichofanya nishuke ni ile kupoteza malengo na juhudi zangu, na pia kuona kwamba vitu vinaanza kuwa vigumu halafu kuweka hiyo kwenye akili kwamba hicho ni kigumu siwezi kukifanya. Lakini nilipoamua kuweka juhudi na kuona kwamba ni vitu vya kawaida kwamba navyozidi kukua na vitu vinazidi kuwa vigumu na natakiwa nitafute njia ya kuvi-overcome, ndo hivyo nikaweza kufanikiwa.

Ratiba yako ya siku ulipokuwa shule kwa ujumla wake ilikuwa vipi na muda gani ulikuwa unajisomea?

Asubuhi nilikuwa naamka mapema kabla ya time table ya shule haijaanza kwa sababu tunatakiwa tuamke mapema kwenda misa kwenye saa kumi na moja hivi. Kwa hiyo naamkaga kwenye saa tisa najiandaa naenda darasani kwa sababu siwezi kusoma usiku kwa sababu usiku nakuwa nimechoka, kwa hiyo my extra time inakuwa asubuhi ambako I’m still fresh. 
Nasoma then ikifika muda wa misa naenda kusali. Nikitoka kusali kuna kazi ndogo ndogo za kufanya kujiandaa na time table ya school and all that. And my free time ile mchana nikitoka darasani kuanzia saa nane, nakuwa nimepanga nini natakiwa nifanye, ni somo gani natakiwa kulisoma at that time ambapo ni saa nane mpaka saa kumi na nusu. Ambapo ni muda wa concentration, kama kuna kitu ambacho sijaelewa naenda kuwafuata waalimu kwa sababu wanakuwa wapo at that time. And kuna some free time kama ile break time, ni kuanzia saa nne na dakika 40 mpaka saa tano na robo, pale hauwezi kusema unatake breakfast all the time, unatake breakfast for a short time halafu nyingine inabaki unaweza kufanya maswali matano ya physics. Yaani every little time ambayo unaweza kuipata, you don’t let it go to waste tu, una-utilize.
Marafiki ulionao wanaweza kusaidia kukupandisha au kukushusha. Wewe ulikuwa na marafiki wa aina gani? 
Marafiki wangu nimewachagua kwa category..yeah (anacheka), ikifika muda wa kusoma nakuwa na mtu ambaye najua atanisaidia, kwa hiyo nilikuwa na rafiki yangu anaitwa Sarafina amekuwa wa nne. Alikuwa ananiinfluence sana kusoma, huyo ni wakati wa kusoma, kwenye academics namfata yeye.

Ikifika wakati wa social siwezi kumfata sarafina kwa sababu she is not that social, yeye yuko kama mimi we are not that social, kwa hiyo ninaye social friend. Pia ikifika muda wa kuspend, I have an economical friend. Ambaye I’m sure nikikaa nae nikiwa naspend siwezi kwenda beyond my budget. Kwamba siwezi kufulia. Kwamba we are all in the same status, same friends, yeah.
Ni kitu gani kilikuwa kinakuboa sana shuleni na kukunyima furaha muda mwingine?
Kitu ambacho kilikuwa kinaniboa sana, ikifika wakati ambapo kwa mfano watu wachache kwenye darasa wamefanya kosa halafu sasa mnakuwa included as a whole class halafu mnapata adhabu. Hiyo adhabu directly itaharibu time table yangu ya kusoma. Kwa hiyo badala ya kusoma nafikiria ningekuwa nasoma physics, I’m either slashing an area..yaani hiyo ilikuwa inaniboa sana yaani.
Ulishawahi kuitwa ‘Msongo’ au majina kama hayo? Ulikuwa unaichukuliaje na je, ilikutenga na marafiki zako? 
Yeah, msongo…kauzu. Yeah mimi naipenda hivyo kwa sababu nafanya nachotakiwa kufanya ambacho ni kusoma. Hiyo haikunitenganisha na marafiki zangu. 

Vuta taswira, je, ingetokea ukapata division Zero na kuwa wa mwisho Tanzania nzima ungefanyaje? Na unawashauri nini waliofeli kwa kiasi hicho?
Kama ningepata zero, kwanza ningefikiria…na ningekuwa very disappointed kweli, lakini pia ningefikiria kuhusu kujipa second chance, ningeenda kusoma tena. 
Kwa waliofeli ningependa kuwashauri wasikate tamaa hata kidogo and wajipe second chance. Kwa wengine pia ambao wana vipaji vyao wanaweza kuviendeleza. But pia kwa kuwa elimu ni muhimu..ku-reseat pia ingekuwa ana option.
Robina Nicholaus ni msichana wa aina gani?

Robina ni mtu mkimya lakini mcheshi pia. Nisingependa nikae na mtu halafu nikawa kimya just because ni mkimya... I will try kuchekesha, and of course I’m funny anyway.

MAISHA NI BUNGE, MNAJUA KUNA NINI DOM?

Nianze kwa kuwapa ‘hi’ madenti wote Tanzania nzima, anko wenu nipo katika Viwanja vya Bunge mjini Dodoma kama mmoja wa mashahidi wa nini wale wawakilishi wa makundi mbalimbali ambayo Rais Jakaya Kikwete aliwateua kujumuika pamoja kupitia rasimu ya katiba ili waweze kutengeneza katiba mpya ambayo huenda ni watoto wenu nyinyi au wajukuu zangu mimi, watakaa tena miaka 50 ijayo kuirekebisha kulingana na mazingira ya wakati huo.
Ni jambo zito sana, ingawa najua kabisa ni wachache sana kati yenu ambao mnafuatilia na kwa jinsi mnavyoishi, mimi hata sishangai. Ni rahisi nyinyi kujua kibao gani kipya Rihanna katoa, Jay Z kasema nini au Beyonce kafanya tukio gani lililovunja rekodi.
Labda niwaambie kitu kimoja. Hapa Dom, ambako ni Makao Makuu ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ndipo niliposoma sekondari na kidogo shule ya msingi. Ninapajua kama kiganja changu. Naijua mitaa balaa, ingawa hiyo ni miaka 20 iliyopita.
Kama nilivyosema mwanzo, zaidi ya Watanzania 600 wapo hapa kujadili rasimu ya katiba iliyowasilishwa na Tume Maalum ya Mabadiliko ya Katiba iliyoongozwa na Jaji Joseph Sinde Warioba ambaye miaka ya nyuma, nyinyi mkiwa wadogo na baadhi yenu hamjazaliwa, alipata kuwa Waziri Mkuu na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Yeye alikuwa mwenyekiti na makamu wa tume hiyo ambayo iliundwa na Rais Jakaya Kikwete.  Lakini pia ndani ya tume hiyo, walikuwepo viongozi wengi wa enzi zetu sisi, walioheshimika sana, akiwemo katibu mkuu wa zamani wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika, enzi hizo ikijulikana kama OAU, Dk. Salim Ahmed Salim.
Hawa watu walizunguka nchi nzima, kuwasikiliza wananchi wa aina na rika zote, nini wanadhani wanaona kinafaa kuwa ndani ya katiba yetu. Labda niwaulize, mnajua katiba ni nini? Najua wengi wenu hamjui, labda kama ‘Diamond Platinumz’ ataamua kuiweka katika moja ya vibao vyake, labda mtaijua.
Katiba ni sheria mama ya nchi, ndani yake haki ya kila mtu, kila kada, kila jamii imetafsiriwa. Sheria zote, zile za polisi, ardhi, misitu, mahakama na kila aina ya sheria utakayoambiwa, msingi wake mkubwa ni ndani ya katiba. Hakuna sheria wala kanuni yoyote itakayokubana wewe kama haipo ndani ya katiba hii ambayo inajadiliwa, kukubaliwa na hatimaye kutiwa saini kama sheria na wenzetu hawa wapatao 600!
Hili ni jambo kubwa sana ambalo kwa makusudi, tumekataa kulitambua uzito wake badala yake bado tunapigiana simu, kutumiana SMS, kuchati katika Facebook na Twitter kuelezana wapi leo tutakutana, wapi kuna tamasha na nani atatumbuiza!
Tukio hili ni la kihistoria, halijawahi kutokea katika nchi yetu tokea ipate uhuru mwaka 1961! Hata hao wanasiasa wakubwa mnaowasikia, hawajawahi kushuhudia utayarishwaji wa katiba mpya ya nchi yetu. Wote kwa ujumla wetu, hii ni mara ya kwanza ambayo ninaamini kabisa, kama ikienda sawa, mimi anko wenu sitashuhudia tena Watanzania wakikaa na kujadili katiba mpya!
Unajua kwa nini sitashuhudia? Hiyo labda itatokea miaka 50 ijayo. Unadhani nitakuwepo kwa maisha haya ya chipsi kuku, juisi za magumashi za Buguruni na viroba? Thubutu!
Ninachotaka kuwaambia sasa, hili jambo siyo la wale jamaa wanaosema posho ya shilingi  laki tatu kwa siku haiwatoshi, hili ni jambo lenu nyinyi maanko kwa sababu vile vibabu pale  vinawaandalia mustakabali wa maisha yenu kama taifa hapo baadaye.
Ni lazima mfuatilie kwa umakini mkubwa kinachoendelea hapa Dodoma, mjue wanawapa nini, kwa sababu baadhi yao, ambao mimi ninawapinga, eti wanataka katiba ya kulinda maisha yao ambayo imebaki miaka mitano au kumi ijayo!
Fuatilieni, hasa nyinyi ambao mpo vyuoni na hata sekondari, msikubali wawape katiba ambayo kumbe baadaye mtagundua kuwa inawalinda watoto wao, vimada wao na hata mashemeji zao. Bado hamjachelewa, mkiona wanawazingua niiteni, niambieni na mimi kwa kushirikiana na wapambanaji wenzangu, tutawapa za chembe!
Niwaage kwa kuwaambia kuwa maisha ya Dodoma wala siyo magumu kihivyo, wanatudanganya tu baadhi ya hawa wabunge. Wanasema eti shilingi laki tatu kwa siku haziwatoshi, kivipi? Nionavyo mimi hata laki moja kuimaliza kwa siku inahitaji ufujaji wa hali ya juu.
Huwa haziwatoshi labda wana myanya mingi ya matumizi, labda matanuzi yao ni ya kujionysha, isije kuwa wanawapa nyinyi madenti. Kataeni.

KIPUTE CHA LEO KOCHA WA YANGA ASEMA"KILA NAFASI BAO"


Kocha wa Yanga, Hans Van Der Pluijm amewataka wachezaji wake kuhakikisha wanatumia kila nafasi wanayopata kufunga bao dhidi ya Al Ahly ya Misri.

Yanga na Al Ahly zitakutana kesho katika pambano la raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika litakalopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Yanga ilitinga hatua hiyo baada ya kuibwaga Komorozine kwa kuicharaza  jumla ya mabao 12-2, ikiwa ni baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 7-0 nyumbani na ushindi wa mabao 5-2 ugenini.

Akizungumza na gazeti hili jana, Pluijm alisema anaamini njia pekee itakayomwezesha kuizamisha Al Ahly ni wachezaji wake kupachika bao katika kila nafasi watakayopata.

“Tulishinda mabao 7-0 dhidi ya Ruvu Shooting kwa sababu tulikuwa makini kutumia nafasi. Jambo zuri ni kwamba uwezo wa kutengeneza nafasi tunao  hivyo ni wajibu wetu kuzitumia,” alisema Plyuijm.

“Nataka  tunatengeneza nafasi nyingi basi na mabao yawe mengi. Tukiwa makini katika hilo sina shaka kwamba tutawafunga.”

Katika hatua nyingine, Pluijm alisifu mazingira ya kambi yake kwa kusema hayana tofauti na yale waliyoweka nchini Uturuki mapema Januari.

“Hoteli ni nzuri pia uwanja tunaoutumia kufanyia mazoezi ni bora kabisa kiasi ambacho kimemfanya kila mmoja wetu kuifurahia,” alisema Pluijm.

Hata hivyo, Pluijm alishindwa kuthibitisha kama atamtumia beki Mbuyu Twite ambaye aliumia wakati wa mechi ya Ligi Kuu dhidi ya Ruvu Shooting.

“Twite jana (juzi) aliniambia anajisikia maumivu, lakini leo amefanya mazoezi hivyo nasubiri kama atakuwa fiti hadi kufikia Jumamosi lakini kwa sasa siwezi kusema moja kwa moja kama nitamtumia au la,” alisema Mdachi huyo.

Mwigulu Nchemba azindua kampeni za CCM Kalenga

Wanaccm wakiwa wamembeba juu juu mgombea ubunge katika Jimbo la Kalenga,Iringa Godfrey Mgimwa katika uzinduzi za kampeni za chama hicho zilizozinduliwa jana katika Jimbo hilo.

Mchangie Mtoto Huyu Anayeteseka na Majeraha ya Moto..!


Salome Kiegu (Mama mkubwa wa mtoto) mkazi wa Mtaa wa Maendeleo Iyunga Jijini Mbeya akiwa amempakata mtoto Adolotea Njavike (1.4) aliyepata ajali ya moto akiwa na mamayake na kusababisha viungo vyake kuungana kwa sasa.
Salome Kiegu (Mama mkubwa wa mtoto) mkazi wa Mtaa wa Maendeleo Iyunga Jijini Mbeya akiwa amempakata mtoto Adolotea Njavike (1.4) aliyepata ajali ya moto akiwa na mamayake na kusababisha viungo vyake kuungana kwa sasa.
Salome Kiegu (Mama mkubwa wa mtoto) mkazi wa Mtaa wa Maendeleo Iyunga Jijini Mbeya akiwa amempakata mtoto Adolotea Njavike (1.4) aliyepata ajali ya moto akiwa na mamayake na kusababisha viungo vyake kuungana kwa sasa.
Salome Kiegu (Mama mkubwa wa mtoto) mkazi wa Mtaa wa Maendeleo Iyunga Jijini Mbeya akiwa amempakata mtoto Adolotea Njavike (1.4) aliyepata ajali ya moto akiwa na mamayake na kusababisha viungo vyake kuungana kwa sasa.
MTOTO Adolotea Njavike (1.4) anaomba msaada wa matibabu kutoka kwa wasamaria wema ili aweze kufanyiwa upasuaji kutokana na kichwa na kiwiliwili kuungana baada ya kupata ajali ya moto akiwa na mama yake mzazi.
Akizungumzia mkasa huo mamamkubwa wa mtoto Salome mkazi wa Mtaa wa Maendeleo Iyunga Jijini Mbeya alisema mtoto huyo alipata ajali ya moto katika mazingira ya kutatanisha kwani waliangukia kwenye moto yeye na mama yake hivyo mtoto huyo kujeruhiwa vibaya. Alisema tukio hilo lilitokea Agosti, 2013 lakini alipopatiwa matibabu katika kituo cha afya mtoto huyo aliungana ngozi ya kidevu na kifua hali inayomletea shida wakati wa kula na hata kucheza na wenzake.
Alisema tangu kipindi hicho alimchukua mtoto huyo kwa mama yake na kuanza kuomba msaada wa matibabu baada ya kumpeleka katika Hospitali ya Ikonda iliyoko Makete mkoani Njombe ambapo Wataalamu walimwambia atafute shilingi 100,000 ili mtoto wake aweze kutibiwa.
Alisema kuwa baada ya muda wataalamu walimwambia asubiri wazungu kutoka Ulaya ambao baada ya kusubiri kwa muda wazungu hao walifika na kumcheki mwanaye kisha kumwambia wao hawana utaalamu isipokuwa aende CCBRT Dar es Salaam ambako ataweza kutatuliwa tatizo lake.
Aidha kutokana na kuambiwa hivyo mama huyo anaomba msaada kutoka kwa wasamaria wema ili aweze kumpeleka mtoto wake kwa matibabu kwani hana uwezo wa kugharamia safari hadi Dar es Salaam pamoja na matibabu. Alisema kwa mujibu wa waliomshauri kwenda kwenye matibabu anahitaji zaidi ya shs milioni 2 ili ziweze kumsafirisha na kugharamia matibabu pamoja na huduma za kawaida akiwa kwenye matibabu ya mwanaye.
Mtu yeyote mwenye kuguswa na tatizo hilo anaweza kuwasiliana moja kwa moja na Mama huyo kupitia simu yake ya Mkononi namba 0752 986879 au Nyumbani kwake Iyunga Mtaa wa Maendeleo Jijini Mbeya.

Ajali Basi la Bunda Lagongana na Treni,watu wanne wafariki dunia.

Basi la Bunda Express lililokuwa likitokea Dodoma kwenda Mwanza asubuhi hii limegongana na Treni Eneo la Manyoni mkoani Singida.Kwa mujibu wa chanzo cha habari kutoka eneo la tukiokinasema kuwa watu wanne wamefariki dunia na kadhaa kujeruhiwa.
Majeruhi Tayari wamepelekwa kwenye Hospitali ya Wilaya ya Manyoni

WASANII WAZINDUA KAMPENI YA KITAIFA KUISHINIKIZA SERIKALI KUWATAMBUA WASANII KIKATIBA

  • Leo asubuhi pande za Kinondoni Vijana Social Hall kulikua wasanii wa fani mbalimbali walikusanyika kuzindua kampeni ya kitaifa kuishinikiza serikali kuwatambua wasanii. Kuna maandamano ya amani pia yatafanyika sambamba na kumpongeza rais Jakaya Kikwete kwa kumteua mmoja wao ashiriki kwenye bunge la katiba

Kanuni za Kuliongoza Bunge la Katiba Zakabidhiwa…! Share


Kanuni za Kuliongoza Bunge la Katiba Zakabidhiwa...! 
Na Magreth Kinabo- Maelezo, Dodoma
KAMATI ya Kumshauri Mwenyekiti wa muda wa Bunge Maalum kuhusu Kanuni za Bunge maalum imewasilisha taarifa katika semina iliyoandaliwa kwa wajumbe wa bunge hilo, ambapo imependekezwa mambo mbalimbali, likiwemo kuwepo kwa Siwa na wagombea uenyekiti na makamu mwenyekiti kutojitoa katika nafasi zao baada ya uteuzi wa wagombea.
Akiwasilisha taarifa hiyo Mwenyekiti wa kamati hiyo, Profesa Costa Mahalu wakati wa semina hiyo kwa wabunge hao, alisema kuwepo kwa Siwa mahsusi ambayo baada ya bunge hilo kukamilisha shughuli zake litatunzwa kama kielelezo cha kumbukumbu ya tukio hilo muhimu la kihistoria.
Alisema Siwa hilo litakuwa na urefu wa mita 1.2, uzito wa 4.5kgs, madini ya dhahabu na aluminium na muonekano wenye alama mbalimbali, ambazo ni kitabu, michoro ya watu wa makundi mbalimbali walioshiriki kutunga Katiba ya Tanzania kwa mujibu wa sheria, rangi, nembo, bendera ya taifa na kalamu inaounganisha kichwa na mkonga.
Profesa Mahalu aliongeza kuwa kamati hiyo imependekeza kuwepo kwa Siwa mbili ili moja iwekwe kama kumbukumbu kwa upande wa Tanzania Bara na nyingine Zanzibar. Alisema kamati hiyo imeongeza kanuni za uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum, ambapo imeweka fomu ya mgombea wa nafasi hizo na karatasi ya kupiga kura.
Mambo mengine yaliyopendekezwa katika rasimu hiyo ni watu wenye mahitaji maalum kuruhusiwa kutumia vifaa maalum ili waweze kuonekana kwa urahisi kwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum na kupewa nafasi ya kusema wakiwa katika ukumbi wa mikutano ya bunge hilo na wasaidizi wa wajumbe wenye mahitaji maalum waruhusiwe kuingia katika ukumbi huo ili wawasaidie wajumbe hao katika zoezi la kupiga kura na kupata usaidizi mwingine watakao uhitaji ukumbini.
Aidha alisema kamati hiyo imependekeza wakati Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba anapowasilisha Rasimu ya Katiba wajumbe wasiruhusiwe kuomba ufafanuzi, utaratibu au mwongozo wa Mwenyekiti.
Aliongeza kuwa kamati hiyo imependekeza katika uendeshaji wa shughuli za Bunge Maalum pale ambapo mjumbe hataridhika na uamuzi wa Mwenyekiti wa Bunge Maalum kuhusu sula linalohusu Kanuni za Bunge Maalum, mjumbe huyo atakata rufaa kwa Kamati ya Kanuni na Haki za Bunge, ambayo Mwenyekiti anayekatiwa rufaa hatakalia kiti, na pia rufani hiyo ifanyiwe kazi na taarifa yake itolewe katika bunge hilo ndani ya kipindi kisichozidi siku tano.

Pia imependekeza ili vikao wa bunge hilo vianze idadi ya wajumbe wa bunge hilo iwe nusu kwa nusu kutoka Tanzania Bara na Zanzibar, ambapo awali ilikuwa ni nusu ya wajumbe wote. Katika taarifa hiyo imependekezwa kuwa viongozi wa bunge hilo kwa kufuata misingi ya haki na bila upendeleo wowote wasiruhusiwe kuhudhuria vikao vyovyote ambavyo vinajadili na kuweka msimamo juu ya suala lolote linalojadiliwa au litakalojadiliwa na bunge hilo.

Profesa Mahalu alisema kamati hiyo inapendekeza kanuni mpya inayohusu Rais wa Jamhuri ya Muungano, Rais wa Zanzibar au Rais wa nchi nyingine kutambuliwa kama wageni rasmi wanaoweza kualikwa na Mwenyekiti wa bunge hilo na kulihutubia. Aidha alifafanua kwamba kamati hiyo inapendekeza kuainisha mavazi rasmi yanayoruhusiwa katika bunge hilo.

Serikali ‘Kuwasomesha’ Wanachuo 20 Mikoa ya Lindi na Mtwara


Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Eliakim Maswi akizungumza na viongozi wa dini kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara katika siku ya pili ya kongamano la viongozi hao kuhusiana na rasilimali zetu za gesi asilia, mafuta na madinikwa amani na maendeleo ya Tanzania. Kongamano ambalo lilifanyika leo katika ukumbi wa VETA, Mtwara.
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Eliakim Maswi akizungumza na viongozi wa dini kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara katika siku ya pili ya kongamano la viongozi hao kuhusiana na rasilimali zetu za gesi asilia, mafuta na madinikwa amani na maendeleo ya Tanzania. Kongamano ambalo lilifanyika leo katika ukumbi wa VETA, Mtwara.

Baadhi ya viongozi wa dini kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara wakiwa katika ukumbi wa VETA, Mtwara katika siku ya pili ya kongamano la viongozi hao kuhusiana na rasilimali zetu za gesi asilia, mafuta na madinikwa amani na maendeleo ya Tanzania.
Baadhi ya viongozi wa dini kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara wakiwa katika ukumbi wa VETA, Mtwara katika siku ya pili ya kongamano la viongozi hao kuhusiana na rasilimali zetu za gesi asilia, mafuta na madinikwa amani na maendeleo ya Tanzania.

Picha ya pamoja ya viongozi wa dini na Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini mara baada ya siku ya pili ya  kongamano lililohusu raslimali zetu za gesi asilia, mafuta na madini kwa amani na maendeleo ya Tanzania. Kongamano ambalo lilifanyika leo katika ukumbi wa VETA, Mtwara.  (Picha zote na Eleuteri Mangi- MAELEZO, Mtwara)
Picha ya pamoja ya viongozi wa dini na Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini mara baada ya siku ya pili ya kongamano lililohusu raslimali zetu za gesi asilia, mafuta na madini kwa amani na maendeleo ya Tanzania. Kongamano ambalo lilifanyika leo katika ukumbi wa VETA, Mtwara. (Picha zote na Eleuteri Mangi- MAELEZO, Mtwara)

Na Eleuteri Mangi- Maelezo, Mtwara
SERIKALI imeahidi kuangalia uwezekano wa kuwafadhili wanafunzi wapatao 20 kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara wanaosoma katika chuo kikuu kishiriki cha Stella Maris Mtwara (STEMUCO) ambao hawana uwezo wa kulipa ada ya masomo yao.
Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Eliakim Maswi alipokuwa akijibu ombi lililotolewa na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha STEMUCO, Padre Dk. Aidan Msafiri alipokuwa akiwasilisha mada yake ya Tunu na maadili katika rasilimali za gesi, mafuta na madini kwa amani na maendeleo ya Tanzania wakati wa siku ya pili ya kongamano la viongozi wa dini kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara. Katibu Mkuu Maswi alisema kuwa serikali ipo tayari kuhakikisha inawapatia elimu hiyo ili waweze kihudumia jamii ya wanaLindi na Mtwara katika kujiletea maendeleo yao wenyewe na taifa kwa ujumla.

Lengo kubwa la kongamano hili lilikuwa ni kutoa elimu zaidi kwa viongozi wa dini kuhusiana na rasilimali za gesi asilia, mafuta na madini kwa ajili ya maendeleo ya nchi nzima kwa ujumla. Elimu hiyo ililenga kuwaelimisha viongozi hao wa dini ambao wanaushawishi mkubwa kwa waumini wanaowaongoza ambapo mada mbalimbali zilitolewa ili kuwajengea uwezo wa kuwaelimisha waumini wao juu ya masuala ya gesi asilia, mafuta na madini.
Mada zilizowasilishwa katika kongamano hilo ili kufanikisha uelewa wa pamoja kwa viongozi wa dini ni pamoja na Mtazamo wa Kitheolojia/Kidini juu ya rasilimali za gesi asilia, mafuta na madini iliwasilishwa na Sheikh Abubakar Zuberi, Maelezo ya jumla ya Wizara ya Nishati na Madini kuhusu za gesi asilia, mafuta na madini iliwasilishwa na Katibu Mkuu wa wizara hiyo Eliakim Maswi, Tunu na maadili katika za gesi asilia, mafuta na madini iliwasilishwa na Padre Dkt. Aidan Msafiri, Ushuhuda wa mwakilishi aliyehudhuria mafunzou ushirikishaji mang’amuzi ya uchumi wa gesi nchini Thailand iliwasilishwa na Hssan Gobbosi.
Mada nyingine ni Mipango ya matumizi ya gesi asilia katika mikoa ya Lindi na Mtwara iliwasilishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Yona Killagane, Uzoefu wa ushiriki wa wazawa katika masuala ya gesi asilia iliwasilishwa na Sultan A. Sultan na Maelezo ya Wizara yaliyowasilishwa na Mwara Shoo na Ally Samaje.

Aidha, Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini imeridhia kuendelea kuwapeleka vijana wa mikoa hiyo kusoma VETA kwa muda wa miaka mitatu ili waweze kutumia fursa ya kugunduliwa kwa rasilimali mbalimbali katika mikoa hiyo. Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC Yona Killagane akiwasilisha mada juu ya mipango ya matumizi ya gesi asilia Lindi na Mtwara alisema kuwa zipo faida nyingi za mradi wa gesi kwa wananchi.
Killagane alizitaja faida hizo kuwa ni kujenga shule za chekechea, wanafunzi wanapata udhamini wa kusomeshwa shule za sekondari, kujengewa hospitali, kuwapatia maji safi, ajira na kupata umeme unaotokana na gesi aktika maeneo yao.
Kongamano hili la siku mbili la viongozi wa dini wa mikoa ya Lindi na Mtwara liliandaliwa na viongozi wa dini wa mikoa hiyo ikiwa ni muendelezo wa kongamano la kitaifa la viongozi hao lililofanyika mwezi Januari mwaka huu jijijni Dar es salaam.
Makonamano haya yote mawili yaliongozwa na kauli mbiu ya “Rasilimali zetu za gesi asilia, mafuta na madini kwa amanina maendeleo ya Tanzania.

Ahukumiwa Miaka 30 kwa Kumbaka Mwanafunzi Std II


Jaji Mkuu Tanzania, Chande Othuman
Jaji Mkuu Tanzania, Chande Othuman

Yohane Gervas, Rombo
MAHAKAMA ya Wilaya ya Rombo imemuhukumu Joseph Didas (39) mkazi wa Kijiji cha Ubaa Tarafa ya Mkuu Wilaya ya Rombo kutumikia kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na kosa la kumbaka mwanafunzi wa darasa la pili.
Awali mwendesha mashtaka Mkaguzi wa Polisi, Berndad Machibya amedai mahakani hapo kuwa Mshtakiwa mnamo mwezi Julai, 2013 kwa siku nne tofauti alimbaka mwanafunzi mwenye umri wa miaka nane ambaye anasoma darasa la pili katika Shule ya Msingi Ubaa.
Akisoma hukumu hiyo Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Rombo, Naomi Mwerinde alisema ameridhika na ushahidi wa pande zote mbili baada ya kusikiliza na kupitia kwa umakini na busara nyingi. Alisema amerithika pasipo na shaka kuwa mshtakiwa Joseph Didasi alifanya kitendo hicho kinyume na kifungu 130, 131 ya kanuni ya makosa ya adhabu.
Aidha Mwerinde alisema uchunguzi wa daktari unaonesha kuwa mlalamikaji alibakwa kwani baada ya madaktari kumfanyia uchunguzi walibaini kuwepo kwa michubuko sehemu za siri pamoja na rangi nyekundu katika sehemu hizo jambo ambalo si la kawaida.
Kabla ya Hakimu Mwerinde kutoa hukumu hiyo upande wa mashtaka ukiongozwa na mwendesha mashtaka wa polisi Mkaguzi, Bernad Machibya aliomba mahakama hiyo kutoa adhabu kali kwa mshtakiwa ili iwe fundisho kwake na wengine wote wenye matendo kama yake, kwani vitendo vya ubakaji kwa watoto wadogo wilayani Rombo vinaonekana kukithiri.
Akitoa hukumu hiyo hakimu Mwerinde alisema kuwa kitendo hicho ni cha kikatili na cha kusikitisha hivyo alistahili kifungo cha maisha lakini kutokana na mshtakiwa kuiomba mahakama na kujitetea kuwa ni mgonjwa imempunguzia adhabu. Hakimu Mwerinde alisema sasa atatumikia kifungo cha miaka 30 jela ili iwe fundisho kwake na kwa wengine wenye tabia kama hiyo.

Kilwa Kutumia Rasilimali Kuboresha Maisha ya Wananchi


Ramani ya hospitali ya kisasa yenye hadhi ya kimataifa itakayojengwa wilayani Kilwa kwa nguvu za halmashauri na wadau wa Maendeleo.
Ramani ya hospitali ya kisasa yenye hadhi ya kimataifa itakayojengwa wilayani Kilwa kwa nguvu za halmashauri na wadau wa Maendeleo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa, Adoh Mapunda (katikati) akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu namna wilaya hiyo inavyoendelea kuboresha huduma za jamii kwa kutumia rasilimali mbalimbali zilizo katika wilaya hiyo. Kushoto ni diwani wa kata ya Kikole Mwl. Haji Mulike na kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya hiyo Bw. Ali Mohamed Mtopa. Picha zote na Aron Msigwa - MAELEZO
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa, Adoh Mapunda (katikati) akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu namna wilaya hiyo inavyoendelea kuboresha huduma za jamii kwa kutumia rasilimali mbalimbali zilizo katika wilaya hiyo. Kushoto ni diwani wa kata ya Kikole Mwl. Haji Mulike na kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya hiyo Bw. Ali Mohamed Mtopa. Picha zote na Aron Msigwa – MAELEZO

Na Aron Msigwa – Maelezo, Dar es Salaam UONGOZI wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa umesema utahakikisha rasilimali zote zinazopatikana katika wilaya hiyo ikiwa ni pamoja na gesi asilia zinatumika kuleta maendeleo na kuboresha maisha ya wananchi.
Kauli hiyo imetolewa jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa, Adoh Mapunda wakati akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu uboreshaji wa huduma za jamii kwa kutumia rasilimali mbalimbali zilizo katika wilaya hiyo.
Akiwa ameambatana na baadhi ya viongozi wa wilaya hiyo akiwemo Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya hiyo, watendaji na baadhi ya Madiwani wanaohudhuria kikao kazi jijini Dar es Salaam, Mapunda alisema kuwa halmashauri hiyo imejipanga kupunguza utegemezi wa fedha toka serikali kuu kwa kupanua wigo wa mapato ya ndani kwa kubuni vyanzo vipya vya mapato.
Amevitaja vyanzo hivyo vipya ni pamoja na ushuru wa zao la Ufuta ambalo sasa mapato yake yamefikia milioni 595, mauzo ya viwanja na ushuru wa Gesi asilia inayozalishwa katika Kijiji cha Songosongo ambayo sasa inatoa asilimia 0.3 ikiwa ni ushuru wa tozo la huduma.
Akifafanua kuhusu mapato hayo, Mapunda alisema kuwa katika zao la ufuta asilimia 20 ya pato hilo inarudishwa vijijini na halmashauri hiyo na kuongeza kuwa mapato ya ushuru wa huduma unaolipwa kwa halmashauri kutokana na shughuli za gesi za kampuni ya PAN AFRICAN ENERGY katika eneo la Songosongo huchangia 20% kwa ajili ya maendeleo ya eneo hilo.
“Kuanzia mwezi Septemba 2012 Baraza la Madiwani lilipendekeza tuanze kupeleka asilimia 20 kwenye kijiji cha Songosongo kutokana na malipo ya kampuni ya PAN AFRICAN ENERGY kiasi cha shilingi milioni 811ambapo hadi sasa tumeshapeleka jumla ya shilingi milioni 139 na tunajiandaa kupeleka kiasi kingine kilichobaki cha shilingi 22,” alisema Mapunda.

Akitoa ufafanuzi kuhusu uboreshaji wa huduma za jamii mkurugenzi huyo alisema Wilaya ya Kilwa inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ikiwemo ya Maji Safi, Umeme, Elimu, mkakati wa kukuza ajira, kuimarisha ulinzi na usalama kwa kujenga kituo cha polisi cha kisasa kitakachogharimu shilingi milioni 625 na uboreshaji wa huduma za afya.

Aliongeza kuwa katika kuboresha huduma za afya wilaya hiyo imeshatenga eneo la hekari 30 kwa ajili ujenzi wa hospitali ya kisasa yenye hadhi ya kimataifa itakayotoa huduma ya afya kwa wakazi wa wilaya hiyo.

“Mradi huu wa hospitali ya kisasa utaanza haraka iwezekanavyo ndani ya mwaka huu hii ikiwa ni mchango wa rasilimali za eneo letu pia kwa kushirikiana na kampuni inayochimba gesi, pia tunajiandaa kwa ujenzi wa ukumbi wa kisasa wa kimataifa utakaogharimu kiasi cha shilingi bilioni 3.8,” alifafanua.

Aidha katika hatua nyingine, Mapunda ameeleza kuwa halmashauri ya Kilwa inaendelea na mikakati ya kuimarisha miundombinu ya barabara ili kuimarisha usafiri wa ndani wa wilaya hiyo, kufanya juhudi ya ukamilishaji wa miundombinu ya ulinzi na usalama ili kuimarisha hali ya ulinzi na usalama wa miundombinu iliyopo.

Rais Kikwete, Wanajumuiya UDSM Wauaga Mwili wa Balozi Kazaura

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitoa heshima zake za mwisho  kwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Marehemu Balozi Fulgence Kazaura katika ukumbi wa Nkrumah Chuoni hapo leo February 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitoa heshima zake za mwisho  kwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Marehemu Balozi Fulgence Kazaura katika ukumbi wa Nkrumah Chuoni hapo leo February 27, 2014.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini katika kitabu cha maombolezo wakati alipowasili kwenye hafla rasmi ya mazishi ya Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Marehemu Balozi Fulgence Kazaura katika ukumbi wa Nkrumah Chuoni February 27, 2014. Nyuma yake ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Dar es salaam Profesa Rwekaza Mukandara na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe saidi Meck Sadick.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini katika kitabu cha maombolezo wakati alipowasili kwenye hafla rasmi ya mazishi ya Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Marehemu Balozi Fulgence Kazaura katika ukumbi wa Nkrumah Chuoni February 27, 2014. Nyuma yake ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Dar es salaam Profesa Rwekaza Mukandara na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe saidi Meck Sadick.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na waombolezaji wengine  kwenye hafla rasmi ya mazishi ya Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Marehemu Balozi Fulgence Kazaura katika ukumbi wa Nkrumah Chuoni February 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na waombolezaji wengine  kwenye hafla rasmi ya mazishi ya Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Marehemu Balozi Fulgence Kazaura katika ukumbi wa Nkrumah Chuoni February 27, 2014.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifariji familia ya marehemu  kwenye hafla rasmi ya mazishi ya Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Marehemu Balozi Fulgence Kazaura katika ukumbi wa Nkrumah Chuoni February 27, 2014. PICHA NA IKULU
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifariji familia ya marehemu  kwenye hafla rasmi ya mazishi ya Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Marehemu Balozi Fulgence Kazaura katika ukumbi wa Nkrumah Chuoni February 27, 2014. PICHA NA IKULU
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, Februari 27, 2014, ameungana na mamia ya waombolezaji kuaga mwili wa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Balozi Fulgence Kazaura katika shughuli ya heshima za kuaga mwili iliyofanyika Ukumbi wa Nkrumah, Chuoni hapo.
Rais Kikwete aliwasili kwenye ukumbi huo kujiunga na Makamu wa Rais Dk. Mohamed Gharib Bilal, Waliokuwa Mawaziri Wakuu, Joseph Warioba na Frederick Sumaye, Makamu wa Chuo Kikuu hicho Profesa Rwekaza Mukandala, familia ya marehemu na waombolezaji wengine muda mchache klabla ya kuanza shughuli ya kuaga mwili.
Marehemu Kazaura ambaye alikuwa Mkuu wa UDSM kati ya mwaka 2005 hadi kifo chake, aliaga dunia Jumamosi iliyopita katika Kituo cha Ugonjwa wa Kansa mjini Chennai, India na mwili wake uliwasili nchini Jumanne wiki hii. Mazishi ya marehemu yamepangwa kufanyika keshokutwa Jumamosi, Machi Mosi, 2014, nyumbani kwao Bukoba.
Katika uhai wake alishikilia nafasi nyingi za utumishi ikiwa ni pamoja na kuwa RDD, Katibu Mkuu wa Wizara mbali mbali, Balozi wa Tanzania katika Umoja wa Ulaya na Ubelgiji, na Naibu Katibu Mkuu wa Jumuia ya Afrika Mashariki.

JK Azinduwa Mtambo wa Kuhakiki na Kusimamia Mawasiliano ya Simu

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akibofya kitufe kuzindua rasmi Mtambo wa Kuhakiki Takwimu za Mawasiliano (Telecommunication Traffic Monitoring System) February 27, 2014 katika jengo la Mawasiliano Towers jijini Dar es salaam.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akibofya kitufe kuzindua rasmi Mtambo wa Kuhakiki Takwimu za Mawasiliano (Telecommunication Traffic Monitoring System) February 27, 2014 katika jengo la Mawasiliano Towers jijini Dar es salaam.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kuzindua rasmi Mtambo wa Kuhakiki Takwimu za Mawasiliano (Telecommunication Traffic Monitoring System) February 27, 2014 katika jengo la Mawasiliano Towers jijini Dar es salaam. Kulia ni Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Prof. Makame Mnyaa Mbarawa, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk Fenella Mukangara, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Prof. John Nkoma, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Saidi Meck Sadick na wadau wengine wa tehama.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kuzindua rasmi Mtambo wa Kuhakiki Takwimu za Mawasiliano (Telecommunication Traffic Monitoring System) February 27, 2014 katika jengo la Mawasiliano Towers jijini Dar es salaam. Kulia ni Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Prof. Makame Mnyaa Mbarawa, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk Fenella Mukangara, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Prof. John Nkoma, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Saidi Meck Sadick na wadau wengine wa tehama.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo ya Mtambo wa Kuhakiki Takwimu za Mawasiliano (Telecommunication Traffic Monitoring System) aliouzindua leo February 27, 2014 katika jengo la Mawasiliano Towers jijini Dar es salaam. Kulia ni Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Prof. Makame Mnyaa Mbarawa, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk Fenella Mukangara, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Prof. John Nkoma, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Saidi Meck Sadick na wadau wengine wa tehama. PICHA ZOTE NA IKULU.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo ya Mtambo wa Kuhakiki Takwimu za Mawasiliano (Telecommunication Traffic Monitoring System) aliouzindua leo February 27, 2014 katika jengo la Mawasiliano Towers jijini Dar es salaam. Kulia ni Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Prof. Makame Mnyaa Mbarawa, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk Fenella Mukangara, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Prof. John Nkoma, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Saidi Meck Sadick na wadau wengine wa tehama. PICHA ZOTE NA IKULU.
Na Mwandishi Maalumu
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, Februari 27, 2014, amezindua Mtambo wa Kuhakiki na Kusimamia Mawasiliano ya Simu (Telecommunications Traffic Monitoring System –TTMS) katika sherehe fupi lakini ya kufana iliyofanyika Makao Makuu ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) mjini Dar Es Salaam.
Mtambo huo unalenga kuhakiki na kusimamia mawasiliano ya simu zinazoingia nchini kutoka nje ya nchi kwa kubaini jinsi matumizi ya simu yanavyofanyika, kubaini bei zinazotozwa na faida inayopatikana pamoja na kuihakikishia Serikali mapato yake stahiki.
TCRA imeupata mtambo huo wenye gharama ya dola za Marekani milioni 25 bila kuununua moja kwa moja. Mtambo huo umenunuliwa na kufungwa na Kampuni ya SGS ya Uswisi ikishirikiana na Kampuni ya JVG ya hapa nchini. Kampuni hiyo itausimamia na kuuendesha mtambo huo kwa miaka mitano chini ya utaratibu wa “Jenga, Endesha na Hamisha – Build, Operate and Transfer” kipindi ambako itaweza kurudisha gharama zake kabla ya kuukabidhi kwa TCRA.
Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Profesa John Nkoma amemwambia Rais Kikwete katika sherehe hizo kuwa ufungaji wa mtambo huo hautaongeza bei ya mawasiliano kwa watumiaji wa simu. Badala yake, amesema Profesa Nkoma, Serikali itanufaika kwa kupata kiasi cha dola za Marekani milioni moja kwa mwezi ikiwa ni gawio lake kutokana na faida itakayotokana na mtambo huo mpya.
Tayari TCRA imekwishakabidhi kwa Serikali dola milioni moja za mwezi uliopita na katika sherehe, Profesa Nkoma ameikabidhi Hazina mfano wa hundi yenye thamani ya sh. 1,684, 357. 283 (sawa na dola milioni moja) kwa mwezi wa Februari. Amesema kuwa fedha yake tayari imewekwa kwenye Akaunti ya Mfuko wa Hazina.
Akizungumza kwenye sherehe hiyo, Rais Kikwete ameeleza mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya mawasiliano katika miaka tisa iliyopita na jinsi gharama za mawasiliano zilivyopungua katika kipindi hicho kutokana na hatua mbali mbali zilizochukuliwa na serikali na hasa ujenzi wa Mkongo wa Mawasiliano wa Taifa.
Amesema kuwa matumizi ya simu yameongezeka kutoka laini za simu milioni 3.6 mwaka 2005 hadi kufikia laini milioni 28 mwishoni mwa mwezi uliopita wakati watumiaji wa Internet wameongezeka kutoka milioni 4.9 mwaka 2011 hadi kufikia milioni tisa wa sasa.
Kuhusu gharama za simu, Rais amesema kuwa gharama hizo zimepungua kwa asilimia 57 kati ya mwaka 2009 na 2013 kwa upande wa simu wakati punguzo hilo kwa upande wa internet.

Mkosaji na Mvunjifu Haki za Binadamu ni Serikali – Jaji mstaafu Mihayo


Pichani ni Baadhi ya Wakuu na Makamishina wa Jeshi la Polisi nchini wakiwa na viongozi wa asasi za kutetea Haki za Binadamu wakifurahia jambo wakati wa uwasilishwaji wa mada mbalimbali kwenye warsha ya siku moja iliyowakutanisha viongozi waandamizi wa Jeshi hilo na watetezi wa Haki za Binadamu nchini.
Pichani ni Baadhi ya Wakuu na Makamishina wa Jeshi la Polisi nchini wakiwa na viongozi wa asasi za kutetea Haki za Binadamu wakifurahia jambo wakati wa uwasilishwaji wa mada mbalimbali kwenye warsha ya siku moja iliyowakutanisha viongozi waandamizi wa Jeshi hilo na watetezi wa Haki za Binadamu nchini.
IMEELEZWA kuwa mkosaji na mvunjifu mkubwa wa haki za binadamu ni serikali kutokana na mazingira halisi ya utendaji na mfumo mzima wa utawala katika serikali nyingi duniani.
Akizungumza kwenye warsha ya siku moja iliyoandaliwa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu nchini, Tanzania Human Rights Defenders Coalition (THRDC) kwa wakuu na makamanda wa Jeshi la Polisi nchini, Jaji Mstaafu, Thomas Mihayo amesema kwa mfumo wa utawala katika nchi nyingi duniani mkosaji mkuu wa haki za binadamu ni serikali.
“dunia nzima inajua kwamba serikali ndio mkosaji mkuu wa haki za binadamu na maana halisi ya serikali ni dola na mahakama tu kwisha,” amesema Jaji Mihayo
Jaji Mihayo amesema kuwa kwa hali ya kawaida dola ikimkamata mtu au mhalifu lazima mpeleke katika mahakama ili sheria ichukue mkondo wake wa kawaida.
Kwa upande wake, Mjumbe wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu, Dkt Helen Kijo Bisimba akitoa neno la ufunguzi amesema warsha hiyo inatoa fursa nzuri kwa watetezi wa haki za binadamu na Jeshi la Polisi kuboresha kazi zao za utetezi wa haki za binadamu nchini.
Amesema kwa ujumla haki za binadamu hazipewi bali ni haki ya msingi ambayo mtu anazaliwa nayo ili zinaminywa aidha kupitia mtu kwa mtu au taasisi au mfumo wa utawala.
“Kazi za watetezi wa haki za binadamu na Jeshi la Polisi zinaendama na msingi ni utetezi wa haki za binadamu pamoja na mali zao,” alisisitiza
Naye, Mratibu wa kitaifa wa Mtandao huo, Onesmo Olengurumwa akiwasilisha mada yake ya (The Concept of Protection and Security Management for Human Rights Defenders and Social Organization) amesema kuwa taaluma inaweza kutumika kutetea haki za binadamu katika maeneo mengi hapa duniani.
Amesema pia kupitia mada hiyo kwamba jamii inadhani kwamba anayepaswa kutetewa ni mwananchi tu lakini pia hata polisi naye ni binadamu anapaswa kuwa na mtetezi pale ambapo haki yake ya msingi inapovunjwa.
“Mpaka sasa Tanzania haina sheria yeyote inayomlinda mtetezi wa haki za binadamu lakini tunaendelea na mchakato na ni matumaini yetu serikali itaridhia kuwa na sheria hiyo hapa nyumbani,” alilisitiza
Naibu Inspekta Jenerali wa Jeshi la Polisi nchini, Abdurahman Kaniki amesema kuwa jeshi la polisi nchini litaendelea kuimarisha mahusiano kati ya jeshi hilo na watetezi wa haki za binadamu nia ni kudumisha amani na utulivu nchini.
“majukumu ya jeshi la polisi na watetezi wa haki za binadamu nchini yanafanana kwa kila hali ni kulinda na kutetea haki za wananchi na mali zao,” amesema Naibu IGP Kaniki
Kamishina Kaniki alilisitiza kwamba ni muhimu wadau wote kuzingatia sheria za nchi, taratibu na kanuni katika kutafuta haki mbalimbali ili kudumisha amani na utulivu nchini.
“nachukua nafasi kuwakaribisha wadau wote wa haki za binadamu na makundi mengine kushirikiana na jeshi la polisi katika kulinda na kutetea haki za binadamu nchini,” alisisitiza.
Kamanda wa Polisi Arusha, RPC Liberatus Sabas amesema kwa muda mrefu watu wa utetezi wa haki za binadamu na makundi mengine huwa wanasahau kwamba polisi pia ni binadamu nao wanahitaji utetezi kutoka kwa watetezi hao wa haki za binadamu.
DSC_0316
Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Abdurahman Kaniki, akitoa hotuba yake ya ufunguzi kwa niaba ya IGP Ernest Mangu, kwenye warsha ya siku moja iliyowakutanisha viongozi waandamizi wa Jeshi hilo na watetezi wa Haki za Binadamu nchini.
DSC_0259
Mjumbe wa Bodi ya Mtandao wa watetezi wa Haki za Binadamu nchini (Tanzania Human Rights Defenders Coalition) Dk. Hellen Kijo Bisimba akitoa neno la ufunguzi wakati wa warsha ya siku moja iliyowakutanisha watetezi wa Haki za Binadamu nchini na Jeshi la Polisi jijini Dar.
DSC_0379
Jaji Mstaafu Thomas Mihayo akizungumza na Makamanda wa Jeshi la Polisi nchini, umuhimu wa kushirikiana kati ya Jeshi hilo na Asasi za kutetea Haki za Binadamu ili kuleta tija katika nyanja za kiuchumi, kijamii na kisiasa.
DSC_0325
Sehemu ya makamishina na makamanda wa mikoa na maafisa waandamizi wa Jeshi la Polisi nchini wakifuatilia mada mbalimbali kwenye warsha hiyo ya siku moja jijini Dar es Salaam.

DSC_0417
Naibu Inspekta General wa Jeshi la Polisi nchini, Abdurahman Kaniki (kushoto), Mratibu wa THRDC Taifa, Onesmo Olengurumwa (katikati) pamoja na  Mkurugenzi wa Mafunzo na Oparesheni, Kamishina Paul Chagonja wakifuatilia mbalimbali ilizokuwa ikitolewa na washiriki wa warsha hiyo.
DSC_0291
Mratibu wa THRDC Taifa, Onesmo Olengurumwa akiwasilisha mada yake juu ya Ulinzi na utawala wa haki za binadamu kwa mashirika ya watetezi wa Haki za Binadamu pamoja na Polisi.
DSC_0355
Pichani juu ni Meza kuu na chini ni Baadhi ya Wakuu na Makamishina wa Jeshi la Polisi nchini wakifurahia jambo wakati wa uwasilishwaji wa mada mbalimbali kwenye warsha ya siku moja iliyowakutanisha viongozi waandamizi wa Jeshi hilo na watetezi wa Haki za Binadamu nchini.
DSC_0362
DSC_0413
Kamishina wa kanda maalum ya Dar es Salaam, RPC, Sulemain Kova akichangia mada katika warsha ya siku moja kuhusu Haki za Binadamu na ushirikiano kati ya Jeshi la Polisi na watetezi wa Haki za Binadamu nchini.
DSC_0397
Kamanda wa Polisi, Arusha Liberatus Sabas akizungumza umuhimu wa kujali pia askari polisi kwa sababu na wao pia ni Binadamu wanahitaji utetezi kutoka kwa mashirika yasiyo ya kiserikali yanayotetea Haki za Binadamu nchini.
DSC_0390
Kamanda wa Polisi, Lindi, RPC Zeloithe Stephen akitoa nasaha kuhusu miiko na kanuni za Jeshi la Polisi jinsi zinavyotetea na kulinda Haki za Binadamu (Police General Order).
DSC_0438
Picha ya pamoja kati ya viongozi waandamizi wa Jeshi la Polisi nchini na mgeni rasmi Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi nchini.
DSC_0441
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP, Bi. Usu Malya (kulia) akiteta jambo na Kamishina wa kanda maalum ya Dar es Salaam, RPC, Sulemain Kova baada ya kupiga picha ya pamoja.

Uhaba wa chakula. Sababu? Wewe


Uharibifu wa chakula
Ni kiasi gani cha chakula unachokitupa ambacho pengine ungekila?
Basi Ripoti mpya kutoka benki ya dunia inasema kuwa robo ya chakula chote kinachokuzwa duniani hupotea ama kutupwa, na sasa inawataka raia kufikiri kwa makini kile kuhusu uharibifu huu wa chakula.
Inasema kuwa katika maeneo kama vile Marekani na Uchina ,watumiaji wa chakula ndio wa kulaumiwa pakubwa kwa kupoteza chakula hicho.
Lakini katika jangwa la Sahara chakula kingi hupotea wakati wa uzalishaji.
Benki ya dunia inasema kuwa kati ya asilimia 25 na 35 ya chakula chote kinachokuzwa duniani hutupwa.
katika mataifa yanye utajiri wa viwanda ,lawama kubwa zaidi huwaendea watumiaji wa chakula hicho ambao hukiwacha chakula kuoza katika jokovu.
Raia wa marekani kazkazini ni miongoni mwa wale walio na lawama kubwa kwa kuwa asilimia 61 ya chakula chao huharibika wakati wa matumizi.
Mwandishi wa ripoti hiyo Jose Cuesta anasema kuwa kile kinachohitajika ni kubadili tamaduni.
Lakini katika jangwa la Sahara chakula kingi huharibika wakati wa uzalishaji .
Benki kuu duniani inasema kuwa kiwango cha chakula kinachotupwa kinaweza kutofautisha kati ya chakula bora na uhaba wa chakula katika mataifa mengi.
Imeonya kuwa iwapo mbinu za uzalishaji hazitaimarishwa na tabia za kula kubadilishwa ,dunia huenda ikakumbwa na uhaba wa chakula kwa idadi kuu ya watu inayozidi kuongezeka.

Total Yazinduwa Awango Kukabili Tatizo la Umeme kwa Watu wa Kipato cha Chini Share


3. Kikundi cha burudani kikionyesha umahiri wa kutoa burudani kwa wageni waalikwa (hawapo pichani) huku wakiwa wameshika taa za nishati ya jua kuashiria uzinduzi rasmi wa AWANGO. AWANGO ni bidhaa zilizo chini ya Mradi wa ‘Total Access to Solar’ ulioanzishwa na kampuni ya TOTAL mwaka 2010 kusaidia kutatua tatizo la upungufu wa nishati kwa nchi zinazoendelea ukiwalenga watu wa kipato cha chini hasa wa vijijini na pembezoni mwa miji.
3. Kikundi cha burudani kikionyesha umahiri wa kutoa burudani kwa wageni waalikwa (hawapo pichani) huku wakiwa wameshika taa za nishati ya jua kuashiria uzinduzi rasmi wa AWANGO. AWANGO ni bidhaa zilizo chini ya Mradi wa ‘Total Access to Solar’ ulioanzishwa na kampuni ya TOTAL mwaka 2010 kusaidia kutatua tatizo la upungufu wa nishati kwa nchi zinazoendelea ukiwalenga watu wa kipato cha chini hasa wa vijijini na pembezoni mwa miji.
2. Waziri wa nishati na madini Prof. Sospeter Muhongo (kulia), mgeni rasmi katika hafla ya uzinduzi wa bidhaa zinazotumia nishati ya jua kuzalisha umeme zinazojulikana kama AWANGO, wa kwanza kushoto ni Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Mh. Marcel Escure pamoja na Mkurugenzi mkuu wa TOTAL nchini Tanzania Bw. Stephane Gay wakishuhudia matukio katika hafla hiyo.
2. Waziri wa nishati na madini Prof. Sospeter Muhongo (kulia), mgeni rasmi katika hafla ya uzinduzi wa bidhaa zinazotumia nishati ya jua kuzalisha umeme zinazojulikana kama AWANGO, wa kwanza kushoto ni Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Mh. Marcel Escure pamoja na Mkurugenzi mkuu wa TOTAL nchini Tanzania Bw. Stephane Gay wakishuhudia matukio katika hafla hiyo.
1. Mgeni rasmi, Waziri wa Nishati na Madini, Mh. Prof. Sospeter Muhongo akihutubia wageni waalikwa (hawapo pichani) waliohudhuria katika hafla ya uzinduzi wa bidhaa za AWANGO uliofanyika ndani ya hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam, usiku wa jana. Waziri Muhongo aliwapongeza TOTAL kwa juhudi wanazozifanya kusaidia jamii ya Watanzania kupata chanzo cha nishati kitakachowaletea maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Pembeni ni baadhi ya bidhaa hizo zinazotumia nishati ya jua
1. Mgeni rasmi, Waziri wa Nishati na Madini, Mh. Prof. Sospeter Muhongo akihutubia wageni waalikwa (hawapo pichani) waliohudhuria katika hafla ya uzinduzi wa bidhaa za AWANGO uliofanyika ndani ya hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam, usiku wa jana. Waziri Muhongo aliwapongeza TOTAL kwa juhudi wanazozifanya kusaidia jamii ya Watanzania kupata chanzo cha nishati kitakachowaletea maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Pembeni ni baadhi ya bidhaa hizo zinazotumia nishati ya jua
3. Kikundi cha burudani (Maendeleo Dance Crew) kikionyesha umahiri wake wa kucheza huku wakiwa na taa zinazotumia nishati ya jua za mradi wa AWANGO toka Kampuni ya Total mara baada ya uzinduzi wa bidhaa hiyo.
3. Kikundi cha burudani (Maendeleo Dance Crew) kikionyesha umahiri wake wa kucheza huku wakiwa na taa zinazotumia nishati ya jua za mradi wa AWANGO toka Kampuni ya Total mara baada ya uzinduzi wa bidhaa hiyo.
7. Baadhi ua wageni waalikwa wakifuatilia uzinduzi wa bidhaa za AWANGO zilizo chini ya mradi wa TOTAL unaojulikana kama ‘Total Access to Solar’ (TATS) wenye lengo la kutatua tatizo la ukosefu wa umeme nchini Tanzania kwa jamii ya watu wa kipato cha chini. Bi. Marsha alisema kuwa bidhaa hizo zitafika katika mikoa yote nchi nzima.
7. Baadhi ua wageni waalikwa wakifuatilia uzinduzi wa bidhaa za AWANGO zilizo chini ya mradi wa TOTAL unaojulikana kama ‘Total Access to Solar’ (TATS) wenye lengo la kutatua tatizo la ukosefu wa umeme nchini Tanzania kwa jamii ya watu wa kipato cha chini. Bi. Marsha alisema kuwa bidhaa hizo zitafika katika mikoa yote nchi nzima.
6. Meneja wa Maswala ya Kisheria na Ushirika wa kampuni ya TOTAL Tanzania Bi. Marsha Msuya akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi wa bidhaa za AWANGO zilizo chini ya mradi wa TOTAL unaojulikana kama ‘Total Access to Solar’ (TATS) wenye lengo la kutatua tatizo la ukosefu wa umeme nchini Tanzania kwa jamii ya watu wa kipato cha chini. Bi. Marsha alisema kuwa bidhaa hizo zitafika katika mikoa yote nchi nzima.
6. Meneja wa Maswala ya Kisheria na Ushirika wa kampuni ya TOTAL Tanzania Bi. Marsha Msuya akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi wa bidhaa za AWANGO zilizo chini ya mradi wa TOTAL unaojulikana kama ‘Total Access to Solar’ (TATS) wenye lengo la kutatua tatizo la ukosefu wa umeme nchini Tanzania kwa jamii ya watu wa kipato cha chini. Bi. Marsha alisema kuwa bidhaa hizo zitafika katika mikoa yote nchi nzima.
TATIZO la ukosefu wa nishati ya umeme kwa jamii ya watu wa kipato cha chini Tanzania linatarajiwa kufikia kikomo, baada ya TOTAL, moja ya kampuni inayoongoza katika biashara ya nishati duniani, kupitia mradi wa ‘Total Access to Solar (TATS)’ kutambulisha aina mpya ya bidhaa za taa pamoja na vifaa vya kuchajia simu vinavyotumia nishati ya jua vyenye kudumu na vinavyopatikana gharama nafuu nchini Tanzania.
Total Access to Solar (TATS) ni mradi ulioanzishwa na TOTAL mwaka 2010, ukiwa na shabaha ya kuhakikisha upatikanaji wa suluhisho la vifaa vya nishati mbadala katika soko la dunia kwa matumizi ya kijamii na kiuchumi ikilenga jamii ya kipato cha chini. Mradi wa TATS unaendana na mlengo wa kibiashara wa TOTAL ambao ni “Kuwajibika katika upatikanaji wa nishati kwa watu wengi zaidi kadri inavyowezekana, na kupambana na mahitaji ya dunia,”
Miradi ya TATS yote inalenga katika kuleta mabadiliko ya kimaendeleo katika shughuli za kijamii na kiuchumi kwa kutumia nishati itokanayo na vyanzo vya uhakika vikiwemo Jua, Gesi, Mafuta na mabaki ya plastiki. Kwa kugundua mahitaji makubwa ya nishati mbadala kwa Watanzania, TOTAL Tanzania kupitia TATS imezindua rasmi bidhaa mpya zilizo chini ya mradi wa AWANGO, zikiwa ni maalum kwa ajili ya jamii ya Kitanzania.
AWANGO ni mradi unaoleta bidhaa zinazotumia nishati ya jua kuweza kuzalisha umeme. Lengo kuu ni kuwezesha matumizi ya nishati ya jua kama suluhu itakayowezesha upatikanaji wa umeme wa uhakika na nafuu kwa jamii ya watu wa kipato cha chini wanaoishi vijijini na pembezoni mwa miji.
Kabla ya kuzinduliwa Tanzania, mradi wa AWANGO ulishaanza kufanya kazi katika nchi nne duniani huku ukifanyiwa majaribio kwa zaidi ya mwaka mmoja. Baada ya mafanikio katika nchi za Cameroon, Indonesia, Kenya na Jamhuri ya Kongo, zaidi ya taa 125,000 na vifaa vya Jua viliuzwa, baadae mradi huu ulikua na kufikia nchi nyingine nane.
Akihutubia wakati wa uzinduzi wa AWANGO, mgeni rasmi Mhe. Prof. Sospeter Muhongo, ambae ni Waziri wa Nishati na Madini aliwapongeza TOTAL kwa kusaidia kutatua kero ya upatikanaji wa nishati ya uhakika nchini, “kwa niaba ya Serikali, nawapongeza TOTAL kwa kwenda mbali zaidi na kuona uhitaji wa wananchi wetu juu ya mabadiliko na kupiga hatua ya kutatua tatizo upatikanaji wa nishati”.
“TOTAL Wameweza kugundua njia bora ya kuisaidia jamii kwa kuleta vifaa ambavyo vitawasaidia kwenye shughuli za kijamii na kiuchumi. Kama wizara husika tunatambua mchango wa TOTAL kwenye hili na tunawahimiza kuendelea na juhudi zao za kutoa nishati ya gharama nafuu itayopatikana kwa urahisi kwa umma wa Watanzania.” Alisema Prof. Muhongo.
Kwa kuzingatia mahitaji makubwa ya umeme yanayoongezeka kila siku, bidhaa za AWANGO zimetengenezwa kukabiliana na ongezeko hili. Ufanisi, unafuu na kudumu kwa muda mrefu ndio sababu kubwa zinazofanya ya vifaa vya AWANGO kuwa tofauti na vifaa vingine vilivyozoeleka kutumika na jamii ya kipato cha chini.
Akizungumza juu ya upatikanaji wa bidhaa hizo, Mkurugenzi Mtendaji wa TOTAL Tanzania Bw. Stephane Gay alisema kwamba bidhaa hizi zitapatikana katika vituo vyote vya mafuta vya TOTAL vilivyopo takribani mikoa yote ya Tanzania, lakini pia kampuni hiyo itashirikiana na wadau wa maendeleo zikiwema asasi za kijamii katika usambazaji, ikiwa ni Dhamira ya kupeleka bidhaa za AWANGO nchi nzima.
Ikiwa kama bidhaa ya kibiashara inayosaidia jamii, AWANGO imejidhatiti katika kutoa huduma bora na ufanisi mkubwa kama ilivyo TOTAL. Mradi huu unatazamiwa kuwa na matokeo matatu katika njia tofauti za Kiuchumi, kijamii na kulinda mazingira. Shabaha kubwa ni kumpa Mwananchi wa kipato cha chini nguvu ya kujikwamia kimaendeleo kijamii na kiuchumi.
TOTAL Tanzania Ltd ni kampuni inayojishughulisha na usambazaji wa bidhaa za nishati ya petroli na mafuta ghafi. Kampuni hiyo ilianzishwa mwaka 1969 ikiwa na makao makuu yake Dar Es Salaam, Tanzania.

TFF yasitisha mkataba wa kocha wake


Timu ya Taifa ya Tanzania
Hatimaye Shirikisho la Kabumbu nchini Tanzania TFF limetangaza kuvunja mkataba wake na Kocha mkuu wa Timu ya taifa ya soka ya Tanzania Taifa Stars Kim Poulsen kwa kile kilichoelezwa maafikiano ya pamoja baina ya kocha huyo,TFF, na Serikali.
Jamal Malinzi ambaye ni Rais wa Shirikisho la soka Tanzania amesema kuwa huo ni utaratibu wa kawaida hasa baada ya wadau mbali mbali kuona kuwa huu ni wakati wa kufanya mabadiliko ya lazima katika benchi la ufundi la Taifa Stars ambayo inajiandaa kwa mechi za kufuzu kwa Fainali za kombe la mataifa Afrika hapo mwakani zitakazofanyika nchini Morocco.
Kuhusu gharama za kuvunja mkataba na Kocha huyo Bwana Malinzi amesema serikali haitagharamia uvunjaji huo wa mkataba na kocha huyo na badala yake wapo wadau waliojitokeza kugharamia kutokana na kuona umuhimu wa kufanya mabadiliko katika kipindi hiki kwa faida ya soka la Tanzania.
Kwa Upande wake Kocha Kim Poulsen amesema na rekodi yake inaonyesha kuimarika kwa soka la Tanzania katika kipindi cha takriban miaka miwili aliyokuwa akikinoa kikosi cha Taifa Stars lakini kusitishwa mkataba ni jambo la kawaida kwa kocha yeyote baada ya kipindi fulani kutoka sehemu moja na kwenda sehemu nyingine na ndiyo sehemu ya maisha.
“Kama kocha unapoona ndiyo umefanya kazi yako,unapaswa kuangalia mbele zaidi baada ya kufanya kazi yako si lazima uendelee kuwa hapo, mnakaa na kujadiliana na kuachana kwa amani kisha unapaswa kusonga mbele,ninaondoka nikiwa najivunia kipindi nilichofundisha soka hapa,na ninawatakia kila la kheri Tanzania na Taifa Stars kwa ujumla.”alisema Poulsen.
Kuhusu Kocha mpya wa Taifa Stars Jamal Malinzi ambaye ni Rais wa TFF amesema hadi sasa wapo makocha watatu raia wa Uholanzi ni wawili na Mjerumani mmoja wanaosailiwa kwa ajili ya kumrithi Kim Poulsen,lakini moja ya vigezo Malinzi amesema kuwa ni lazima kocha huyo awe amewahi kuipeleka kwenye fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika moja ya nchi zilizoko kusini mwa jangwa la Sahara.
Katika hatua nyingine kocha Salum Madadi ameteuliwa kukaimu nafasi iliyoachwa wazi na Kim Poulsen ambapo kocha huyo akisaidiwa na Hafidh Badru kutoka Zanzibar watasimamia Taifa Stars kwenye mechi ya kirafiki dhidi ya Namibia iliyoko kwenye kalenda ya FIFA baadaye mwezi ujao

Benki ya Dunia 'yabana' msaada kwa UG

Wafadhili wakatiza misaada Uganda
Benki ya dunia imebana msaada wa dola milioni 90 kwa Uganda , siku chache tu baada ya Rais Yoweri Museveni kuishinisha sheriua mpya dhidi ya mapenzi ya jinsia moja.
Benki hiyo imesema kuwa inataka kufanya tathmini yake kuhakikisha kuwa malengo yake ya maendeleo nchini Uganda katika sekta ya afya, ambayo msaada huo ulikuwa unanuiwa, hayataathirika .
Sheria iliyoidhinishwa na Rais Yoweri Museveni, ilitiwa saini Jumatatu na inatoa adhabu kali kwa watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja.
Wafadhili wengine tayari wameanza kusitisha misaada Uganda. Wahisani kama Denmark na Norway wamesema kuwa wataanza kufadhili mashirika moja kwa moja badala ya serikali.
Aslimia 20% ya bajeti ya Uganda inategemea michango ya wafadhili.
Mpaka sasa nchi tatu za Ulaya zimeamua kukata misaada yao kwa mamilioni ya dola.
Wizara ya fedha ya Uganda imesema inasubiri mawasiliano rasmi ya nchi husika, na iko tayari kukabiliana na athari za hatua hiyo.
Hadi kufikia sasa Waziri wa Fedha Wa Sweden, akiwa mjini Kampala, alisema waekezaji kutoka nchi yake watakuwa na wakati mgumu kuweka pesa zao nchini Uganda kwa sababu watakuwa na hofu kuwa sheria yo yote inaweza kupitishwa kuwadhulumu watu.
Jana serikali ya Uholanzi ilisema itazuia kwa muda misaada kwa Serikali ya Uganda. Norway na Denmark pia zimetangaza kupunguza au kusimamisha kwa muda misaada yake kwa Uganda.