Sunday, March 2, 2014

Obama aionya Urusi kuhusu Ukrain

Rais Obama aongea na rais wa Urusi Vladmir Putni katika simu

Rais Obama amesema kuwa Urusi inakiuka sheria ya kimataifa kufuatia hatua yake ya kuingiza vikosi vyake nchini Ukrain na sasa ametoa wito kwa rais Vladmir Putin kuvirudisha vikosi hivyo katika kambi zake za jimbo la Crimea.
katika mazungumzo ya simu yaliochukua takriban dakika 90,rais Putni amemwambia Obama kwamba Urusi ina haki ya kutetea maslahi yake iwapo ghasia zaidi zitaelekea mashariki kwa Ukrain pamoja na jimbo la Crimea.
Rais Obama aongea na rais wa Urusi Vladmir Putni katika simu
Lakini rais Obama ameonya kwamba Urusi huenda ikatengwa kisiasa na kiuchumi iwapo uvamizi huo utaendelea.
Amemwambia rais Putni kwamba wasiwasi wowote wa Urusi kuhusu hali ya raia wa Urusi wanaoishi nchini Ukrain unafaa kujadiliwa ana kwa ana na serikali ya Ukrain.
Kaimu rais wa Ukrain, Oleksandr Turchynov,ameviweka vikosi vyake vya kijeshi nchini humo katika hali ya tahadhari.
Hatua hiyo inajiri baada ya bunge la Urusi kumruhusu Rais Vladimir Putni kutuma wanejeshi nchini Ukrain.
Wakati huohuo kaimu waziri mkuu Arseniy Yatsunuk amevitaka vikosi vya kijeshi vya urusi vinavyopiga doria katika eneo la Cremia kurudi kambini.
Ameonya kuwa iwapo mzozo huo utaendelea,Urusi ipo hatarini ya kukabiliwa kijeshi mbali na kumaliza uhusiano wake na Ukrain.

No comments:

Post a Comment