Saturday, August 24, 2013

PICHA ZA UCHI ZA MPENZI WA DIAMOND ZAVUJA....

Mwanamziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amegeuka gumzo nchini Kenya baada ya mrembo mmoja aliyejipatia jina kupitia Runinga ya KTN, Angel Maggy kutangaza penzi lao upya kwa mara nyingine.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari za burudani vya Kenya, mara baada ya Diamond kufanya shoo mbili katika Miji ya Nairobi na Mombasa nchini humo, alipogeuza kisogo kurejea Bongo ndipo ukaibuka mlipuko wa habari zilizomhusu na mrembo huyo.


Habari hizo zilieleza kuwa mara tu baada ya kutua nchini humo, Diamond alipokelewa kwa bashasha na mrembo huyo akiwa na wenzake wanne.

Ilisemekana kuwa alipokuwa akifanya shoo kwenye Ukumbi wa KICC, Nairobi siku ya kwanza, Diamond aliimba wimbo wake wa Ukimuona maalum (dedication) kwa ajili ya Angel, jambo lililomfanya mrembo huyo kuonekana ‘spesho’ miongoni mwa maelfu waliohudhuria onesho hilo.

Imeripotiwa kuwa baada ya shoo hiyo kumalizika  USIKU, Angel alionekana ‘beneti’ na Diamond wakielekea katika hoteli aliyofikia staa huyo Nairobi. 

Katika  jitihada  za  kulikoleza  penzi  lao, Angel  anadaiwa  kujipiga  akiwa  uchi  wa  mnyama  kwa  lengo  la  kumtumia  Diamond......

Bahati  nzuri  au  mbaya, picha  hizo  zimevuja  na  mtandao  huu  umefanikiwa  kuzinasa....

MSANII MANAIKI ATIWA MBARONI NA POLISI BAADA YA KUPIGA PICHA ZA UCHI NA WAREMBO MBALI MBALI NA KUZISAMBAZA



 
 Jeshi la polisi kanda ya Dar es Salaam linadaiwa kumtia mbaroni msanii anaetuhumiwa kupiga picha chafu na wanawake mchanganyiko wakiwema mamiss maarufu na baadae kusambaza kwenye mitandao yote ya kijamii pamoja na kuripotiwa kwenye magazeti mbalimbali
 

Mwandishi wetu amefanikwa  kuzinasa  picha  za  Manaiki  akiwa chini ya ulinzi wa  polisi huku akiwa amevishwa pingu na kurukishwa kichurachura.
 
Habari za uhakika zilizonaswa  zinasema kuwa msanii huyo alikamatwa siku chache baada kuvuja kwa picha zake za aibu zikimuonesha akiwa na wanawake tofauti tofauti

HATARIIII!!! VIUNGO VYA MAITI VYAUZWA MOCHWARI,MAJI YA KUOSHEA NA SANDA NAVYO DILI.


Kiganja cha binadamu.

OPARESHENI Fichua Maovu ‘OFM’ ya Global Publishers bado iko mitaani ikiibua mambo, wiki hii ilitia timu Wilaya ya Kibaha, Mkoa wa Pwani kilomita chache kutoka jijini Dar es Salaam.


Safari hiyo ilifanywa baada ya kupokea ‘mashitaka’ kwamba, wafanyakazi wa mochwari moja katika hospitali kubwa mjini Kibaha wamekuwa wakiuza viungo vya binadamu.


VIUNGO VINAVYOUZWA 
Kwa mujibu wa chanzo, viungo vinavyouzwa katika mochwari hiyo ni sehemu za siri za jinsi zote, viganja, ndimi na miguu.


WALIOKUFA KWA AJALI DILI ZAIDI
Kwa mujibu wa mtoa habari huyo, viungo vya maiti za watu waliokufa kwa ajali vina dili zaidi kwa sababu havijadhoofika kama wale waliokufa kwa kuugua.
“Tena nawaambia OFM, viungo vya watu waliokufa kwa ajali ni mali sana, wanasema viungo vyao ni imara kuliko wale waliokufa kwa kuugua,” kilisema chanzo.

VINAPATIKANAJE, WATEJA WAO AKINA NANI?
Sosi akaendelea kuweka wazi kwamba, watu wanaofanya kazi mochwari huvikata viungo hivyo wakati wa kuosha miili ya marehemu na kuhifadhi kwa ajili ya wateja wao ambapo wengi ni waganga wa kienyeji.


DILI LINGINE
Mbali na ‘bidhaa’ hizo, maji yaliyooshewa maiti na sanda navyo vilitajwa kuwa ni dili kubwa kwa wafanyakazi wa mochwari.
“Halafu yale maji yanayooshewa maiti na sanda au shuka ambalo hutumika kufunikwa maiti pia ni dili kubwa sana, waganga wanachukua kwa ajili ya kwenda kufunikia kesi mbaya za watu,” alisema mtoa habari.

MAITI ZA WAKRISTO ‘ZINAONEWA’ ZAIDI

Mtoa habari akasema maiti za Wakristo ndiyo huongoza kwa kufanyiwa mchezo huo kwa vile ndugu zao huwapa kazi ya kuosha wafanyakazi na wao kusubiri nje.

Akasema kwa Waislamu ni ngumu kidogo kwani wao wakati wa maiti wao kuoshwa ndugu wawili watatu huingia kusaidia ili kwenda sawa na kanuni za uoshaji wa imani hiyo.

Mtoa habari huyo alizidi kudai kwamba, maiti nyingi za Wakristo huagwa na ndugu kwenda kaburini zikiwa na upungufu wa viungo ila kwa sababu hakuna utamaduni wa kukagua hakuna anayejua. Inatisha sana!

OFM WAINGIA MZIGONI

Baada ya kupata taarifa hizo, hivi karibuni mapaparazi makini walitia timu kwenye hospitali hiyo ambayo hupokea maiti nyingi za watu waliopata ajali katika Barabara ya Morogoro Dar es Salaam.

Walipata bahati ya kupokelewa na mfanyakazi wa mochwari ambapo baada ya salamu walijitambulisha kwa majina ya bandia, Paschal na Fanuel

Walisema  wao ni wafanyabiashara wa samaki tokea Mwanza na wanataka viungo vya wanadamu vilivyopo mochwari hapo.

Mfanyakazi huyo aliweka bayana kwamba, kuna mikono na sehemu za siri za kiume, kama wako tayari wanaweza kuuziwa. Bei ni shilingi milioni moja (1,000,000) mpaka laki mbili (200,000) kutegemea na ukubwa wa kiungo chenyewe.

Ili kudhihirisha hilo, mfanyakazi huyo alikwenda kutoa ‘sampo’ ya viungo hivyo na kuambiwa kama wapo tayari watoe mkwanja biashara ifanyike mara moja.

MAPAPARAZI WATOA AHADI, WASHTUKIWA

HATA hivyo, mapaparazi walimwambia mfanyakazi huyo kwamba kwa muda huo hawana fedha, wangerudi tena jioni na fedha ili kumaliza biashara.

Jibu hilo lilimshtua jamaa huyo na kuwaweka chini ya ulinzi huku akimnyang’anya simu mmoja wa mapaparazi hao.

Aliikagua simu hiyo na kugundua alikuwa akirekodiwa sauti hivyo akafuta sauti hiyo. Pia aliikagua simu hiyo na kubaini meseji za paparazi huyo kumtumia meseji mhariri wake akimwambia upelelezi unakwenda vizuri.

Mfanyakazi huyo alikwenda mbele zaidi kwa kuangalia namba zilizopigwa kwenye simu hiyo na kuona moja ambayo jina la aliyepigiwa lilimaliziwa na paparazi, mfano; Paschal Paparazi, jamaa akashtuka zaidi.

Kama vile haitoshi, jamaa huku presha ikiwa juu, aliingiza mkono kwenye mifuko ya suruali ya mapaparazi na kukutana na vitambulisho vyenye nembo ya Global Publishers & General Enterprises.

“Sikieni, mimi sitaki maneno na nyinyi, nawaomba muondoke eneo hili haraka sana, mmenifanya mimi ni mtoto siyo?” alisema mfanyakazi huyo. OFM iliondoka kwa mafanikio makubwa kwani ilithibitika biashara hiyo ipo.

MIJIMAMA: WANAUME WANATUPENDA SISI MABONGE




Na Waandishi Wetu
MAKUBWA! Madogo yana nafuu! Wanawake wenye maumbile makubwa wanaofanya biashara haramu ya kuuza miili yao jijini Dar, wamefunguka kwamba wanaume wamekuwa wakiwapenda kwa sababu ya ubonge wao

Mijimama hiyo ilitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita wakati ikizungumza na paparazi wetu aliyekuwa katika oparesheni maalum ya kuhojiana nao ili kujua kinachowafanya wajihusishe na biashara hiyo inayohatarisha maisha yao.

Akizungumza na mwandishi wetu, mmoja wa wanawake hao aliyejitambulisha kwa jina moja la Zainabu anayefanya biashara hiyo maeneo ya Sinza Afrika Sana, alisema umbo lake limekuwa likiwadatisha wanaume kibao.

“Kaka si unaiona hii shepu yangu, hapa kuna mwanaume anayeweza kunipita na kwenda kwa wale vimbaumbau,” alisema Zainabu huku akimuonesha paparazi wetu wasichana wembamba waliokuwa mbele yao



Mwanamke mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Sara Mashauzi, aliyekuwa katika mawindo ya wanaume wakware na Zainabu alisema: “Mimi nilianza haya mambo baada ya kuachana na mume wangu, sasa kila ninakopita wanaume wakiniona tu huanza kunipigia miluzi na wengine kuniita, sista… sista… hongera…, nikaamua kujiuza ili nipate kipato kwani maisha yalibana sana.”
Sara aliongeza kuwa, wanaume wengi anaotoka nao wamekuwa wakimsifia kwa umbo lake ‘pana’ na kudai kwa siku huwa hakosi shilingi 50,000 na siku nyingine anapata hadi 80,000.

Karibu wanawake wote mabonge waliozungumza na paparazi wetu maeneo ya Kinondoni, Buguruni, Manzese na Oysterbay ambako biashara hiyo imeshamiri walidai maumbo yao yamekuwa yakipendwa sana na wanaume hususan waume za watu.
Paparazi wetu alipomuuliza Sara, Zainabu na mwenzao aliyejitambulisha kwa jina la Sikitu kwamba hawaoni kama wanaharibu soko la wenzao wembamba, kama vile waliambiana jibu wakasema watajiju!



Baadhi ya madadapoa wembamba waliozungumza na paparazi wetu, waliwafungukia majimama hao na kudai wamewaharibia soko lao na kusababisha wajiuze kwa promosheni.

Gazeti hili linakemea tabia hiyo chafu na isiyofaa katika jamii na kuviomba vyombo husika kupambana na kuwasambaratisha wasichana hao. Mhariri.

TUHUMA NZITO:MAGUFULI, MWAKYEMBE, LUKUVI KUFIKISHWA KWENYE KAMATI YA MAADILI YA BUNGE



Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge.

Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012.

Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni.

“Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. Tunajua kwamba fedha hizi zilipunguzwa kiasi cha Sh95 bilioni na kupelekwa Wizara ya Uchukuzi, zilibakia Sh252.975bilioni katika kifungu hicho lakini kuna bilioni 100 zimetumika visivyo,” alisema Zitto, ambaye pia ni Mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini (Chadema).

Alisema katika majumuisho ya Bajeti ya wizara hiyo, Dk Magufuli na Dk Mwakyembe wakati huo akiwa Naibu Waziri wa Ujenzi na Lukuvi walitoa maelezo yasiyo ya kweli bungeni kuhusu fedha.

Alikariri maneno yaliyorekodiwa kwenye Hansard ya Bunge yaliyosemwa na viongozi hao watatu.

“Tunaomba fedha Sh252 bilioni kwa ajili ya kuanzia kazi za ujenzi wa barabara,” Zitto alisema akikariri maneno ya Dk Magufuli wakati anawasilisha bajeti.

“Fedha hizi zitachangia miradi ya wafadhili,” haya yalikuwa maneno ya Dk Mwakyembe wakati akifanya majumuisho.

“Hizi ni fedha kwa ajili ya counterpart fund,” alimkariri Lukuvi wakati akichangia hotuba ya wizara hiyo.

Zitto alisema CAG alihoji mwaka huu kuhusu matumizi ya fedha hizo na alitoa taarifa akidai kuwa fedha hizo zilikuwa miradi hewa na kasma kivuli.

Zitto alisema kuwa Dk Magufuli na Katibu Mkuu wake walipohojiwa walidai kutumia fedha hizo kulipa madeni.

“Kwa nini mlidanganya Bunge? Mliomba fedha za kuanza miradi maalumu. Hamkuomba fedha za madeni. Kwa nini mliunda kasma kivuli na kuifuta baada ya pesa kulipwa?” Zitto alimhoji Balozi Mrango.

Katika majibu yake, Balozi Mrango alisema kwa nia njema, fedha hizo zilitumika kuwalipa makandarasi waliokuwa wamechachamaa, huku baadhi yao wakisisitiza kusitisha kuendelea na miradi. Hivyo wakalazimika kuomba fedha kwa njia hiyo ili miradi kuendelea katika maeneo mbalimbali ya nchi.

Zitto hakuridhishwa na majibu hayo akisema hapakuwa na haja ya kutumia fedha hizo kuwalipa makandarasi wakati kulikuwa na kasma yao ya awali. Alisema kama kulikuwa na haja hiyo, wizara isingeita mradi rasmi.

“Jambo hili siyo sahihi hata kidogo kulidanganya Bunge na hadi sasa wewe na waziri wako hamuonyeshi kukubali kosa hili, hata Waziri Lukuvi naye alisisitiza bungeni kwamba fedha hizo zinaombwa ili kutekeleza mradi maalumu lakini sasa imebainika sivyo, kwa mujibu wa Kanuni za Bunge tutawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ili wahojiwe nao wajieleze kwa kulidanganya,” alisema Zitto.

Pia kamati hiyo imeitaka wizara hiyo kutoa ufafanuzi wa kina kuhusu matumizi ya Sh100 bilioni zilizotumika kinyume na maombi yaliyowasilishwa kwenye Bajeti ya mwaka huo wa fedha.

CAG ameshauri madeni yote ambayo Wizara ya Ujenzi inadaiwa yaorodheshwe ili yawe wazi kuepuka migongano katika matumizi ya fedha.

Alipoulizwa kuhusu madai hayo, Lukuvi alisema haelewi chochote na kusisitiza kuwa akipata taarifa rasmi za Kamati ya PAC, atatoa ufafanuzi.



Halmashauri zinavyotafuna mabilioni

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAACc), imeeleza namna mamilioni ya fedha za Serikali zinavyoibwa kutoka Hazina kupitia halmashauri za wilaya huku Ilala ikitajwa kuongoza kwa ufisadi huo.

Mwenyekiti wa LAAC, Rajab Mbarouk Mohammed aliwaambia waandishi wa habari jana kwamba Hazina imekuwa ikipeleka fedha kwenye halmashauri zikiwa zimezidi na kwamba kiasi kinachozidi hakirudishwi badala yake huliwa.

Alisema kamati hiyo imefanya uchunguzi kwenye halmashauri 43 na kubaini kwamba mtindo huo ndiyo unaotumika kuiba fedha za Serikali.

“Mwaka 2011/12 kiasi cha Sh1.5 bilioni zilipelekwa zikiwa zimezidi kwenye halmashauri hizo lakini hazikurudishwa Hazina kama inavyoonyesha kwenye ripoti ya CAG.

Alisema kati ya kiasi hicho, Halmashauri ya Manispaa ya Ilala ilipewa ziada ya Sh213 milioni ikifuatiwa na Geita iliyopewa Sh129 milioni.

“Fedha hizo za mishahara zilipelekwa kwenye halmashauri hizo na Hazina kimakosa zikiwa zimezidi lakini watendaji wa hawakuzirudisha kama wanavyotakiwa kisheria badala yake zikayeyuka,” alisema.

Mwenyekiti huyo alisema kuwa uchunguzi huo pia ulibaini kwamba katika halmashauri hizo 43 kiasi cha Sh693 milioni hulipwa mishahara hewa ambayo wafanyakazi wake walishakufa na wengine kustaafu.

Alisema Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema ililipa mishahara hewa yenye thamani ya Sh79.4 milioni ikifuatiwa na Ukerewe iliyolipa Sh57.5 milioni.

Kwa upande wa fedha za miradi ya maendeleo, mwaka 2011/12, Hazina ilipeleka katika Halmashauri ya Mbarali, Mbeya Sh724 milioni kwa ajili ya Mradi wa Maendeleo ya Elimu Sekondari wakati mradi huo ulikuwa ukihitaji Sh70 milioni tu.

“Kiasi cha Sh654 milioni zilipelekwa kimakosa na Hazina lakini badala ya kurudishwa zilitumiwa katika mazingira ya kutatanisha,” alisema.

Alisema Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe ilipelekewa ziada ya Sh500 milioni na Mvomero ilipewa Sh85 milioni. “Kuna mtandao mkubwa wa Hazina na halmashauri ambao ukiachwa utaendelea kupoteza fedha nyingi za walipakodi,” alisema.

Wednesday, August 21, 2013

Serikali yakanusha kuwa Mama Salma Kikwete si Mnyarwanda na wala Kikwete si shemeji yao



Msemaji Mkuu wa Serikali ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO Assah Mwambene leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara hiyo amekanusha taarifa zilizoandikwa kwenye mtandao wa News for Rwanda na  wanyarwanda kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ni shemeji wa aliyekuwa Rais wa Rwanda Juvenal Havyarimana.

“Taarifa hizi haina ukweli wowote na zinalenga kumpaka matope Rais Jakaya Mrisho Kikwete,” amesema Mwambene na kufafanua kuwa lengo la mitandao ya kijamii ni kuhabarisha na kuelimisha umma wala siyo kupotosha jamii kwa kuandika habari zisizo na ukweli wowote.


Madai  hayo  yaliandikwa  jana  na  mitandao  ya  Rwanda  wakidai  kuwa  mama  Salma  Kikwete  ni  Mnyarwanda  na  ni  binamu  wa  aliyekuwa  rais  wa  zamani  wa  Rwanda.

Mtandao wa Kagame wadai kuwa Mama Salma Kikwete ni Mnyarwanda

 
 Mtandao  wa  News  of  Rwanda  umeendelea  kutuchokonoa  watanzania  ili  kuupima  msimamo  wetu.....

Baada  ya  kukurupa  na  madai  kwamba  Rais  Kikwete  si  mtanzania  halisi  na  kwamba  ni  mtu  mwenye  asili  ya  Burundi, mtandao  huo  umekuja  na  kioja  kipya....

Taarifa  iliyotolewa  jana  tarehe  19/08/2013  na  mtandao  huo  inadai  kwamba  mke  wa  Rais  Kikwete  aitwaye  Mama  Salma  Kikiwete  ni   mnyarwanda   wa  kabila  la  wahutu ( mhutu )..


Katika  maelezo  yake, mtandao  huo  umeenda  mbali  na  kudai  kuwa  Mama  Salma  Kikwete  ni  binamu  wa  rais  wa zamani wa Rwanda, Juvenal Habyarimana  na  ndo  maana  rais Kikwete  alitoa  ushauri  wa   mazungumzo  ya  amani  kati  ya  Kagame  na  waasi....
.............................................................
HII  NDO  POST  YAO  WALIYOTOA
---------------------------------------------
New details obtained by News of Rwanda may give insight into why Tanzania’s President Jakaya Kikwete came out as the sole global leader sympathetic to Rwandan FDLR rebels based in DR Congo jungles since 1994.


According to secret US State Department cables published by whistle-blowing site Wikileaks, President Jakaya Kikwete’s wife fondly known in Tanzania as “Mama Salma Kikwete” is a cousin of former Rwanda leader Juvenal Habyarimana. The shocking details are contained in a cable sent to Washington on Thursday May 5th, 2005, by Shabyna Stillman, a senior diplomat at the US embassy in Dar es Salaam.


The US embassy was giving update on the selection of Mr Jakaya Kikwete to be the CCM flag-bearer in the presidential election late that year. “For years, observers of the Great Lakes conflicts have considered Kikwete to be virulently pro-Hutu,” reads the cable, in part.


“Kikwete’s marriage to a cousin of former Rwandan President Juvenal Habyarimana may have fueled these rumors, which are now fading as the Burundi conflict winds down,” adds the cable, signed by Stillman.


According to the US embassy, Mr Kikwete’s love affair with “Hutus” could be seen in his spirited support for Burundian rebels at the time fighting former President Pierre Buyoya.


Since 1995, up until 2005 when Mr. Kikwete was foreign affairs minister of Tanzania, rumours have swelled around him suggesting he sided massively with the ethnic extremist establishment. It is this system that planned and executed the genocide against Tutsis in 1994, and fled across to Zaire and other parts of the world.


It is alleged, around 1996, Mr Kikwete suggested publicly that “Hutus” need to be armed to fight off the government in Kigali at the time. A book published by virulent critic of President Paul Kagame and historian GĂ©rard PRUNIER writes that Tanzania did offer to train troops for Seth Sendashonga.


A former leader of the Rwanda Patriotic Front (RPF), for whom he was a minister in the government set up after the rebel movement’s victory over the army and the militias responsible for the genocide in 1994, Mr. Sendashonga was murdered in Nairobi, Kenya, on 16 May 1998 by, according to PRUNIER, “unknown assailants.”


Fast forward to May 26, 2013, President Jakaya Kikwete goes public with a suggestion that the government of President Kagame in Rwanda negotiates with rebels of the Democratic Forces for the Liberation of Rwanda (FDLR). The group was formed in May 2000, but its members had been roaming DRC forests ever since they lost power in Kigali.


The suggestion by a head of state of Tanzania, a country that had long been considered a friendly nation to Rwanda, caught many by surprise. Since then, the two countries are embroiled in a bitter war of words.


The ex-Rwandan Juvenal Habyarimana died on the evening of April 6th, 1994, after his plane was shot down by extremist members of inner circle who did not want the peace talks with the RPF rebels. In the same plane was Burundian counterpart Cyprien Ntaryamira and French pilots.


The death of the French crew has been the centre of legal battles in France and the United States. A French judicial inquiry did confirm that the plane was brought down by a missile fired from a military camp next to Habyarimana’s home near the airport.
 ---------------

Basi la Turu lachomwa moto na wanakijiji....Abiria 60 wamenusurika

 
Abiria wapatao 60 waliokuwa wanasafiri na basi la Turu linalofanya safari zake kati ya mkoa wa Singida na Haidom mkoani Manyara, wamelazimishwa kuteremka toka ndani ya basi hilo na wananchi zaidi ya mia mbili ( 200 ) wa vijiji vitatu, na kisha kulichoma moto basi hilo.

Taarifa toka eneo la tukio zinasema wananchi hao ni wa vijiji vya Singa, Idabagadu na Nkungi mkoani Singida, ambao baada ya kuhakikisha abiria wote wameshuka, walilichoma moto basi hilo ambalo limetekea sehemu kubwa.

Sababu ya wananchi hao kuchukua uamuzi huo ni kutokana na basi hilo kumgonga mwanakijiji mmoja na kufa wiki tatu zilizopita

Kilichomfanya mbuge Wenje atiwe mbaroni ni Uchochezi

SIKU moja baada ya Jeshi la Polisi mkoani hapa kulazimika kutumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya wananchi na wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), waliokuwa wakiandamana kutoka Uwanja wa Furahisha kuelekea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, mbunge wa Nyamagana jijini Mwanza, Ezekiel Wenje (CHADEMA), amekamatwa akituhumiwa kutenda makosa mawili.
 
Wenje alishikiliwa jana majira ya saa 5 asubuhi kwa mahojiano na Jeshi la Polisi yaliyodumu takribani saa nne.
 
Mbunge huyo aliitwa polisi kwa ajili ya mahojiano kuhusiana na tuhuma za kuchochea maandamano na yeye kuandamana bila kibali, jambo lililosababisha ghasia na uvunjifu wa amani.
 
Inadaiwa na polisi kwamba mbunge huyo juzi aliongoza maandamano ya wafuasi wa CHADEMA na wananchi kutoka Uwanja wa Furahisha kuelekea ofisi ya mkuu wa mkoa, yalikokuwa yakifanyika mazungumzo baina ya Mkuu wa Mkoa Evarist Ndikilo na ujumbe ulioongozwa na mbunge wa Ilemela, Highness Kiwia kuhusu hatima ya meya, naibu wake, na madiwani watatu waliofukuzwa kinyume cha sheria.
 
Wenje aliyeongozana na mwanasheria wake, Charles Kiteja, baadhi ya madiwani wa Nyamagana na Ilemela na viongozi wa CHADEMA Kanda ya Ziwa Magharibi, alifika katika ofisi ya Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Mwanza (RCO), majira ya saa 5 asubuhi.

Akiwa huko, RCO Joseph Konyo na baadhi ya maofisa wengine wa jeshi hilo, walitumia takribani dakika 45 wakimhoji mbunge huyo kuhusiana na tuhuma hizo dhidi yake.
 
Wenje ambaye anasifika kwa msimamo na ushawishi mkubwa kwa wananchi ndani na nje ya jimbo lake la Nyamagana, aliliambia gazeti hili kwamba: “Polisi wanadai nimewaambia wananchi kwamba Ndikilo na Matata ni adui wa wananchi, na wakiwaona wawazomee.
 
“Wananituhumu pia kuongoza waandamanaji kutoka viwanja hivyo vya Furahisha kisha kuelekea ofisi za mkuu wa mkoa, pamoja na kusababisha barabara ya Nera-Makongoro Mission kuzibwa kutokana na ghasia zilizoibuka.”
 
Alipoulizwa kuhusiana na kushikiliwa kwa mbunge huyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, na Naibu Kamishna wa jeshi hilo, Ernest Mangu alikiri Wenje kushikiliwa.
 
“Kweli mheshimiwa Wenje tumemshikilia kwa mahojiano. Anatuhumiwa mambo mawili ya kuchochea maandamano na yeye kuandamana bila kibali cha polisi.
 
“Tunataka mheshimiwa Wenje atueleze alipata wapi idhini ya kuandamana bila kibali, na aliandamana na akina nani. 

Asipotutajia alioandamana nao tutamng’ang’ania yeye hadi kieleweke,” alisema RPC Mangu.

Juzi majira ya alasiri, ziliibuka ghasia baada ya Jeshi la Polisi kulazimika kutumia mabomu ya machozi, kuwatawanya wafuasi wa CHADEMA.
 
Ghasia hizo zilitokea wakati wa maandamano ya chama hicho yaliyolenga kupinga uchaguzi ‘batili’ wa Meya wa Manispaa ya Ilemela, Henry Matata na Naibu wake, Swila Dede, pamoja na kupinga kufukuzwa madiwani watatu wa chama hicho kinyume cha taratibu, kanuni na sheria za nchi.
 
Madiwani waliofukuzwa na Matata kinyume cha sheria na kata zao kwenye mabano ni Abubakar Kapera (Nyamanoro), Malietha Chenyenge (Ilemela), na Dany Kahungu (Kirumba).

Godbless Lema augua ghafla, kesi yake yaahirishwa


MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Arusha jana imeshindwa kuanza kusikiliza kesi ya uchochezi inayomkabili Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, dhidi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, kutokana na mbunge huyo kuwa mgonjwa.
Wakili wa Lema, Method Kimomogoro, aliieleza mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi, Hawa Mguruta, anayesikiliza shauri hilo kuwa Lema anaumwa na alikuwa amelazwa katika Hospitali ya AICC tangu Agosti 14 hadi 19, mwaka huu aliporuhusiwa kutoka hospitali, hivyo ametakiwa apumzike kwa muda wa siku 10 kuanzia Agosti 19, mwaka huu.
 
Wakili Kimomogoro aliomba shauri hilo liahirishwe hadi siku nyingine, ombi lililokubaliwa na hakimu aliahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 1 na 2 mwaka huu, ambapo mashahidi tisa wanatarajiwa kutoa ushahidi wao.
Wakili wa Serikali, Elizabeth Swai, anayesaidiana na Mary Lucas, alikubaliana na ombi hilo na kuongeza kuwa mashahidi wanne miongoni mwa tisa walikuwapo mahakamani hapo kutoa ushahidi wao jana ambao ni Mkuu wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Arusha (OCD) Gilles Mroto, Naibu Mkuu wa Chuo cha IAA, Faraji Kasidi, Mhadhiri wa chuo hicho, John Nanyaro na maofisa wa Polisi, Jane Chiguga na Bernard Nyambalya.
 
Mashahidi wengine wanaotarajiwa kuletwa mahakamani hapo na upande wa serikali ni pamoja na maofisa wa Jeshi la Polisi,  PC Godfrey, Joachim Mahanyu  na wengine  kutoka Chuo cha Uhasibu, ambao ni  Benjamin Simkanga na Naibu Hamidu.
Awali ilidaiwa mahakamani hapo kuwa  mnamo Aprili 24, mwaka huu, mshitakiwa Lema akiwa eneo la Freedom Square ndani ya Chuo cha Uhasibu, alitoa maneno ya uchochezi yaliyosababisha uvunjifu wa amani.
 
Maneno hayo ni  kinyume cha kifungu cha 390 sura ya 35 cha sheria ya kanuni ya adhabu marejeo ya mwaka 2002 .
“RC anakuja (Chuo cha Uhasibu) kama anaenda kwenye sendoff, hajui chuo kilipo, wala mauaji ya mwanafunzi wa chuo hicho ….. (RC), ameshindwa hata kuwapa (wanafunzi) pole kwa kufiwa na amesema hawezi kuongea na wanafunzi wasio na nidhamu,” yalinukuliwa baadhi ya maneno aliyodai kuwa yalitamkwa na Lema siku hiyo.
Kauli hizo zinadaiwa zilipandisha hasira za wanafunzi ambao walianza kumrushia mawe na chupa Mkuu wa Mkoa, Mulongo, alipokuwa akiwahutubia kuhusiana na tukio la kifo cha mwanafunzi, Henry Koga, kilichotokea Aprili 23, mwaka huu.

MAMBO 100 USIYOYAJUA KUHUSU CHOKOCHOKO ZA RWANDA KWA TANZANIA.....


Historia ya Rwanda ni ndefu iliyojaa misukosuko ya kisiasa, kupinduana, vita na mauaji ya wenyewe kwa wenye yaliyosababishwa na ubaguzi wa kikabila.
 

Rwanda imekuwa ikipita katika vipindi vigumu na vya hatari. Vipindi hivi hufuatana na mauaji ya raia wa nchi hiyo, sio tu kutokana na sababu za ukabila bali pia uongozi mbaya wa kisiasa.
 

Mwaka 1959, mtawala wa Kitutsi aliyekuwa akiitawala nchi hiyo na kulalamikiwa kuwa utawala wake ulikuwa ukiwaneemesha zaidi Watutsi walio wachache, uliangushwa na Wanyarwanda wa Kabila la Kihutu.
 

Mabadiliko haya yalifuatiwa na mauaji ya takriban Watutsi 150,000. Walioponea chupuchupu walikimbilia nchi mbalimbali jirani na Rwanda. 
 
Ni wakati huu wazazi wa Rais wa sasa wa Rwanda, Paul Kagame walikimbilia nchi jirani, Uganda yeye akiwa na umri wa miaka miwili.


Baada ya hapo, Wahutu wakaunda Chama cha PARMEHUTU, kikiongozwa na Gregoire Kayibanda, ambaye baadaye alikuwa Rais wa Rwanda.
 

Mtu angedhani wakati huo kuwa kwa sababu uongozi wa nchi hiyo ulichukuliwa na kudhibitiwa na mtu kutoka kabila la Wahutu waliokuwa asilimia 88 ya Wanyarwanda wakati ule, (Watutsi wakiwa asilimia 11 na asilimia moja Watwa), kusingekuwa na chokochoko tena. Utawala ungekuwa wa amani, wapi?
 

Mapinduzi ya kijeshi

Kinyume na matarajio, Julai 5, 1973 Serikali hii nayo ilipinduliwa. Mapinduzi haya yalifanywa na jeshi la Wahutu wakiongozwa na Meja Jenerali Juvenal Habyarimana, ambaye naye alikuwa Mhutu.
 

Cha ajabu, licha ya tofauti hizo za kikabila, mapinduzi hayo yalifanywa na Wahutu walio wengi wakishirikiana na Watutsi wachache. Hii ilitokana na malalamiko kuwa Rais Kayibanda alikuwa akiendesha nchi kama familia yake, akipitisha uamuzi bila kushirikiana na viongozi wengine.
 

Baada ya mapinduzi hayo, kiongozi huyo mpya alibadilisha mambo mengi ikiwa ni pamoja na kusambaratisha chama kilichokuwa kikiongozwa na Kayibanda, PARMEHUTU, badala yake akaunda Chama cha National Revolutionary Movement for Development MRND.
 

Miaka takriban 17 baadaye kutokana na kile kilichoonekana kama utawala wa kikandamizaji, Watutsi waliokuwa nje ya nchi walishirikiana na Wahutu wa ndani kuanza harakati za kuiangusha Serikali ya Habyarimana.
 

Harakati hizi ndizo zilizomwingiza madarakani Rais wa sasa, Paul Kagame. Malalamiko kama yale yaliyosababisha mapinduzi dhidi ya mtangulizi wa Habyarimana yakajitokeza tena.

Mtu anayeangalia na kuchambua hali ya mambo ilivyo hivi sasa hachelewi kung’amua kuwa hali kama ile iliyozikumba tawala za tangu utawala wa kifalme wa Watutsi na tawala za Kihutu zinajitokeza tena.
 
Na hii inaifanya hali iwe tete kuliko wakati wowote. Wengi wanaamini kama yatatokea mapigano au mabadiliko katika Serikali ya Kigali pengine hali inaweza kuwa mbaya kuliko ilivyowahi kushuhudiwa.
 
Hivi sasa Wanyarwanda hasa kutoka Kabila la Kitutsi na ambao walikuwa bega kwa bega na Rais Kagame, baadhi ya wasomi na maofisa wa juu kutoka jeshi la RPF wameikimbia Rwanda na tayari kuna kampeni za chini kwa chini kutoka makabila yote mawili kuupinga utawala wa Kagame.
 
Mbaya zaidi kuna kundi kubwa la vijana waliozaliwa baada ya mauaji ya Rwanda. Hili ni kundi kubwa na mtu yeyote ambaye amekuwa akitembelea kambi za wakimbizi kwa miaka mingi anaelewa ninachoelezea hapa.
 
Mwaka 1997 nikiwa na waandishi wenzangu tulitembelea kambi za wakimbizi kutoka Rwanda. Kulikuwa na idadi kubwa ya watoto. Mmoja wetu alimuuliza mmoja wa wakimbizi kwa utani “nyinyi mpo kwenye matatizo mbona mnazaa watoto wengi hivi, hamuoni ikiwa mnajiongezea mizigo”?
 “Hawa ndio watakuja kuikomboa Rwanda,” alijibu kiongozi wa wakimbizi huku akipigiwa makofi na kundi la vijana waliokuwa pembeni kusikiliza mahojiano, katika kambi ya Mbuba wilayani.
 
Nadharia hii imekuwa ikiendelea kwa miaka mingi. Hata tulipotembelea kambi nyingine tukiandamana na Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia wakimbizi Ulimwenguni (UNHCR), Antonio Guateres karibu waandishi wengi hawakuficha hisia zao za kushangazwa na kasi ya kuzaana katika kambi za wakimbizi.
 
Fikiria kwa utaratibu huu watoto waliozaliwa tangu mwaka 1994 ni watu wazima. Kama ni wanajeshi ni jeshi kubwa tena lenye hamasa kubwa ya kurudi katika nchi yao Rwanda katika wakati ambapo wanaona kikwazo ni Kagame na Serikali yake.
 
Hivi Kagame anajua kuwa kundi hili halibanwi na tuhuma za mauaji ya halaiki ya Rwanda ya mwaka 1994?  Hata wale wanaotafutwa sio tena kitisho dhidi ya Serikali ya Kigali sababu ni wazee sasa, wa kuogopa ni jeshi hili kubwa la vijana. 
 
Hawa Kagame anawabana na sheria gani? Isipokuwa kwamba wanajiandaa kupigana na Serikali yake kama yeye alivyofanya kuipindua Serikali ya Habyarimana akitokea Uganda?
 
Kibaya zaidi ni kuwa makundi haya katika ukanda wa Maziwa Makuu, wana mawasiliano na kwa nyakati fulani yanasaidiana.
 
Ushauri wa Rais Kikwete

Ninaamini hiki ndicho kilichomsukuma Rais Kikwete kutoa ushauri kwa marais hawa majirani zetu kuwa wasifanye kosa wazungumze na waasi. Heri kupatana nao kwa sasa kuliko baadaye wakisharidhika kuwa wamejiandaa vizuri na wakaanza mapigano rasmi.
 
Kila mwenye macho ya kuona mbali hachelewi kumshauri Kagame chonde chonde ongea na waasi hawa, badala ya kujiridhisha kuwa ni watuhumiwa wa mauaji ya halaiki, wakati wengine mauaji hayo yalitokea wakiwa na umri wa miaka sita na kurudi chini, hawa ni jeshi kubwa lenye uwezo wa muda mrefu wa kukaa msituni, ni hatari.
 
Yapo maswali kadhaa ya kujiuliza, hivi kwa nini Rais Kagame hakioni hiki tunachokiona sisi? Kwa nini hakioni hiki ambacho amekiona Rais mwenzake Kikwete?
 
Ninaamini Rais Kikwete hakukurupuka, ana vyombo vya kiintelijensia vinavyomfahamisha kinachoendelea sio tu Tanzania, lakini hata katika mapori makubwa na Misitu ya DRC.
 
Kagame anapaswa kusoma alama za nyakati, asikimbilie kusema “watuache Rwanda tumalize matatizo yetu,” kwani baada ya mauaji ya mwaka 1994 nchi hiyo ililaumu jumuia ya kimataifakuwa  haikuisaidia Rwanda kuepuka mauaji hayo.
Kama walivyosema Wahaya kuwa “ajuna akanyonyi ajuna akakyahalala” maana ukitaka kumsaidia ndege msaidie akiwa bado ana uwezo wake wa kupaa.
 
Badala yake ametoa lugha za matusi kashfa hadi kutoa vitisho dhidi ya Tanzania, ati kwa ushauri aliopewa na Rais Kikwete, kuwa azungumze na waasi wa Democratic Forces for The Liberation of Rwanda (FDLR).
 
Kikwete alitoa ushauri huo kwenye Kamisheni ya Ulinzi na Usalama ya Umoja wa Afrika wakati wa Mkutano wa wakuu wa nchi za umoja huo uliofanyika mwanzoni mwa Juni mwaka huu, mjini Addis Ababa, nchini Ethiopia.
 
Ushauri huo umegeuka mwiba na kitanzi dhidi ya uhusiano uliokuwepo kati ya Tanzania na Rwanda, ingawa wengine tunajua uhusiano huo haukuwa barabara tangu awali kwani kiongozi huyo wa Rwanda mara kwa mara amekuwa akiisimanga Tanzania hata kabla ya ushauri huo kutolewa. 


Imekuwa kama vile jirani yetu huyu amepata turufu muhimu ya kuitishia Tanzania.
 
Kinachoshuhudiwa sasa ni vita ya maneno baina ya nchi hizi mbili yaani Tanzania na Rwanda.Vita ya maneno na majibizano ya namna hii mataifa hujikuta katika vita kamili.
 
Kwa upande mwingine wengi walishangaa kwa nini Kagame aonekane kukerwa sana wakati ushauri huo haukumhusu yeye peke yake?
 
Wakati Paul Kagame akikabiliwa na kundi linaloinyemelea nchi yake la FDLR, Joseph Kabila, wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) anapambana na waasi wa sasa wa M23,  na Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda akitishiwa na makundi mawili.  Allied Democratic Force (ADF) na Lord’s Resistance Army (LRA).


Hata hivyo, si Tanzania pekee ambayo imeona hatari inayoinyemelea Rwanda bali hata moja ya makanisa nchini Rwanda.

Kanisa hilo lilipeleka ujumbe hivi majuzi hadi Ikulu ya Kagame likitabiri kuwa Rwanda inakabiliwa na matatizo makubwa na kuwa inaweza tena kudidimia katika mgogoro mkubwa. Watumishi hao wa Mungu wameishia kukamatwa na kuambiwa wanataka kuvuruga amani kuleta mgororo wa kikabila.
 
Uasi zaidi
Kila kukicha wanajeshi wa Rwanda wanazidi kulikimbia jeshi lao na nchi yao, siku zilizopita walikuwa wakikimbilia Uganda siku hizi baada ya kuzidishwa ulinzi katika mpaka wa nchi hizo mbili sasa wanakimbilia Afrika Kusini, nchi ambayo inajua kwa hakika kitu gani kinaendelea nchini Rwanda. Inawapa hifadhi ya ukimbizi wa kisiasa.
 
Miongoni mwao ni aliyekuwa Mkuu wa Usalama katika Jeshi la RPF, Luteni Jenerali Faustin Kayumba Nyamwasa. Huyu alianza kutofautiana mapema na Kagame, baadaye akamsogeza mbali na nchi hiyo. Akamteua kuwa Balozi wa Rwanda nchini India.
 
Bado Kagame aliendelea kumwona ofisa huyo tishio, hivyo akamtuhumu kuwa alihusika na milipuko ya mabomu February 2010 mjini Kigali.  Wakati Kagame akiandaa utaratibu wa kumkamata habari zikavuja, ofisa huyo akatoroka kutoka India hadi Afrika Kusini anapoishi sasa.
 
Inafahamika kuwa maofisa wenye uwezo kama wa Nyamwasa wakipata ushirikiano na wanamgambo wa Kihutu walio sehemu mbalimbali nje ya Rwanda ni rahisi kuishambulia Rwanda, ndio maana inasemekana wametumwa makachero kumuua Nyamwasa kule kule Afrika Kusini lakini ‘wakachemka’ na kuishia kwenye mikono ya polisi ambapo walikiri kutumwa na Serikali ya Kigali, kumuua Nyamwasa.
 
Mwezi Juni 2010, Kiongozi wa Timu ya mpira wa miguu wa Rwanda Brigedia Jenerali Jean Bosco Kazura, alikwenda Afrika Kusini kuangalia mashindano ya kombe la dunia, lakini aliporejea Rwanda akakamatwa kwa tuhuma kuwa akiwa huko alifanya mawasiliano na Nyamwasa na kwa maana hiyo akaingizwa katika kundi la wanaotaka kuiangusha Serikali ya Kagame.
 
Jean-LĂ©onard Rugambage, mwandishi wa habari ameuawa na makachero ikisemekana kuwa alikuwa akitumiwa na Nyamwasa.


Maofisa wa Serikali ya Rwanda wanapotetea msimamo wa Rais Kagame wa kuikejeli Tanzania wanadai kilichomkasirisha bosi wao ni kushauriwa akae meza moja na wale anaowaona kama wauaji wa halaiki wa mwaka 1994, na kuwa ushauri huo ni sawa na kucheza juu ya makaburi ya Wanyarwanda waliopoteza maisha katika mauaji hayo.
 
Hata kama ingekuwa hivyo, basi angewachukia waasi wale lakini sio Tanzania kwa sababu baada ya mauaji ya Rwanda, iwe Kagame au waasi wenyewe hakuna upande wowote uliowahi kuituhumu Tanzania kuhusika kwa namna yoyote katika mauaji hayo, kwa sababu wanajua kuwa nchi hii ilikuwa ikijua kila kilichokuwa kikiendelea na kikifanywa na kila upande kabla na baada ya mauaji hayo.
 
Na hapo ndipo lilipo ‘fumbo la imani’ kwa nini Kagame amechukia sana kwa ushauri ule.
 
Sababu nyuma ya pazia
Udhaifu wa sababu ya chuki za Kagame unaashiria  kwamba kilichoikasirisha Rwanda ni uamuzi wa Tanzania kupeleka jeshi lake lishiriki kulinda amani DRC, na sio ushauri ule.

Alijua kuwa sasa mengi  yatafumuka, ambayo tayari Tanzania inayafahamu ikichanganya na yale itakayoyagundua DRC. 

Nina mifano mingi na ushahidi wa kimazingira hebu nitaje mmoja na kumalizia makala yangu.
 
Yaliyotokea 1994
Rwanda inajua, Kagame anajua, na dunia nzima inajua kuwa mauaji ya kimbali ya Rwanda yalikolezwa zaidi ya kutunguliwa ndege ya aliyekuwa Rais wa nchi hiyo wakati huo, Habyarimana.
 
Habyarimana na mwenzake wa Burundi, Syprian Ntaryamirwa walikuwa wakitoka Arusha nchini Tanzania katika mojawapo ya mikutano yenye lengo la kuangalia namna ya kugawana madaraka baina ya Serikali ya Kigali ya wakati ule na kundi la waasi siku zile RPF.
 
Kikundi hiki cha RPF kikiwa na Watutsi wengi kilikuwa kimeanzisha mapigano dhidi ya Serikali ya Habyarimana miaka miwili kabla wakipigana kutokea nchini Uganda wakitaka Serikali itoe nafasi  kwa Watutsi karibu lakini tano waliokuwa wakiishi nje ya Rwanda.
 
Licha ya Serikali ya Habyarimana kusaini makubaliano ya kuwaingiza waasi wa RPF katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa, Wahutu ambao ndio walio wengi walikuwa hawakubaliani na jambo hili.Kwa hiyo, fikiria inakuja kufahamika kuwa Watutsi wale walioanzisha mashambulizi kutokea nchini Uganda, wametungua ndege ya Rais wa kabila lao na kumuua pamoja na makamanda wa ngazi za juu wa jeshi la Rwanda la wakati ule.
 
Ndio maana baada ya kutunguliwa ndege hiyo Aprili 1994 mauaji ya kutisha yaliyodumu kwa siku mia moja yaliendelea na kugharimu maisha ya Wanyarwanda laki  nane, wengi wao wakiwa Watutsi na Wahutu wenye msimamo wa wastani.

-Imeandikwa  na  Christopher Buke   wa  gazeti  la  mwananch