Tuesday, June 25, 2013

MAMA ASIYE NA HURUMA AMTUPA MTOTO KISIMANI BAADA YA KUJIFUNGUA


Sources state they saw the little unlucky child later and when they came for his rescue he was already swollen and floating lifelessly on the surface of the the dim water. Some women don't deserve to be called mothers.

Tears poured from neighbours, especially a young woman who has been trying to give birth for four years to no avail, as the police came to fetch out the baby from the well.

After a quick search by the police the mother's blood and placenta was seen on the ground a couple of meter's away from the scene of the crime.

The main suspect is already on her heels as she was warned by her close friends that the police have been involved.

The picture above was given by a citizen journalist.

MAREKANI YATOA ONYO KALI KWA MSAFARA WA RAIS OBAMA TANZANIA


Dar es Salaam. Licha ya ujumbe wa Rais wa Marekani, Barrack Obama kutarajiwa kufikia katika hoteli kubwa zenye hadhi wakati kiongozi huyo atakapowasili nchini Julai Mosi mwaka huu, Ikulu ya Marekani imetoa tahadhari ya vyakula ambavyo hawatakiwi kuvigusa wakiwa nchini ikiwa ni pamoja na kutumia maji ya bomba.
Mbali na tahadhari hiyo, ziara hiyo ya Obama itakuwa na ulinzi mkubwa ambao pengine haujawahi kutokea katika historia ya viongozi wa nje wanaotembelea Tanzania kwani utahusisha idadi kubwa ya magari, ndege za kijeshi na meli kubwa ya kivita ambazo zitakuwa zikifanya doria karibu na pwani ya Tanzania.
Tahadhari za matumizi ya chakula, maji na nyinginezo zimetolewa katika nchi zote tatu za Afrika ambazo Obama atatembelea, kila moja kwa jinsi Wamarekani hao wanavyoitathmini.
Rais Obama atatembelea nchi za Tanzania, Senegal na Afrika Kusini.
Ulinzi
Vyombo vya usalama vya Marekani vimejipanga kuhakikisha ziara ya kiongozi huyo haivurugwi kwa namna yoyote ile. Tayari ndege za jeshi zilizobeba magari ya akiba 56, yakiwemo 14 aina ya ‘Cadillac One’ maalumu kwa ajili ya kiongozi huyo, yamewasili katika nchi hizo tatu za Afrika atakazotembelea.
Kwa mujibu wa gazeti la Washington Post la Marekani, ndege hizo pia zimebeba malori matatu ambayo yamesheheni karatasi maalumu za kuzuia risasi kupenya kwenye vioo, zitakazobandikwa kwenye madirisha ya hoteli ambazo Rais Obama na ujumbe wake watafikia.
Kwa mujibu wa gazeti hilo, mamia ya mashushushu wa Marekani tayari wako katika nchi hizo. Meli maalumu za kubeba ndege za kivita, maarufu kwa jina la ‘amphibious ship,’ ikiwa na hospitali maalumu na yenye vifaa vyote itaweka nanga baharini, jirani na nchi atakayokuwa Rais Obama, tayari kukabiliana na dharura yoyote itakayotokea. Gazeti hilo liliandika kuwa ndege za kivita za Marekani zitakuwa zikipeana zamu kufanya doria kwa saa 24, katika anga la nchi ambayo Rais Obama atakuwepo, iwapo ndege za ‘adui’ zitakaribia eneo linaloitwa ‘anga ya rais.’ Kwa mujibu wa gazeti hilo, ziara ya Rais Obama aliyoifanya hivi karibuni katika nchi za Ujerumani na Ireland Kaskazini, japo kulikuwa na gharama kwa walinzi, lakini safari za nchi za Afrika zimeelezwa kuwa na gharama kubwa zaidi.
Tahadhari
Kwa mujibu wa taarifa ya maelekezo ya Ikulu ya Marekani, ambayo Mwananchi imepata nakala yake, watu watakaokuwa kwenye msafara wa Obama wametakiwa kutotumia kachumbari. Pia imewataka kutumia maji ya chupa zaidi.
“Kutokana na mfumo wa maji uliopo, tunashauri watu wetu kutumia maji ya chupa zaidi kwa kunywa na hata kwa kupiga mswaki,” ilisema taarifa hiyo.
Kwa kuelewa fika tatizo la ugonjwa wa malaria nchini, ujumbe wa Obama umeshauriwa kutumia dawa ya mbu ya kupaka na kupuliza inayoitwa Deet.

Deet ni dawa maarufu huko Marekani na ikiwa katika aina tofauti ikiwamo ya kupaka na kupuliza na imekuwa ikitumiwa na jeshi la Marekani kwenye vita mbalimbali tangu miaka ya 1940 kabla ya kuanza kutumiwa na raia mwaka 1957.
ATM nazo noma
Pia watu watakaokuwa kwenye msafara wa Rais Obama wametakiwa kuhakikisha wanatumia mashine za kutolea fedha (ATM) zilizoko karibu na hoteli watakazofikia.
“Kuna tatizo la uhalifu kwa hiyo siyo vizuri kutumia ATM ambazo ziko katika sehemu zisizo salama. Pia katika kipindi watakachokuwa Tanzania watu wanapaswa kutumia teksi ambazo zimeidhinishwa na hoteli.
“Pia siyo vizuri kuacha kompyuta ya fedha kwenye vyumba mtakavyolala. Pia kina mama wanapaswa kuchukua tahadhari ya mabegi yao watakapokuwa wanapita mitaani,” ilitahadharisha taarifa hiyo.

Monday, June 24, 2013

HALI YA MANDELA NI TETE...ASHINDWA KUFUMBUA MACHO KWA SIKU KADHAA


Mzee Nelson Mandela ameendelea kuwa katika hali mbaya hospitalini jana baada ya kubainika kwamba gari la wagonjwa lililombeba Rais huyo wa zamani wa Afrika Kusini kwenda hospitali limeharibika.

Gari hilo la wagonjwa mahututi liliharibika wiki mbili zilizopita wakati Mandela alipokuwa akikimbizwa kwenye hospitali moja mjini Pretoria, na kumwacha 'njiapanda' kwa dakika 40.


Rais huyo wa zamani wa Afrika Kusini alihamishiwa kwenye gari jingine la wagonjwa la hospitali ya kijeshi kumalizia safari iliyobaki ya dakika 50 kati ya Johannesburg na Hospitali ya Moyo ya Medi-Clinic.

Msemaji wa Rais Mac Maharaj alisema: "Tahadhari zote zimechukuliwa kuhakikisha kwamba hali ya kiafya ya rais wa zamani Mandela haiathiriki na tukio hilo."


Madaktari wanaomtibu Mandela waliridhika kwamba hakupata maumivu yoyote katika kipindi hiki, aliongeza Maharaj.

Taarifa ya jana kuhusu afya ya Mandela inaonesha kwamba kuna mabadiliko kidogo katika hali ya shujaa huyo wa kupinga ubaguzi wa rangi tangu alipopokelewa hospitalini hapo.
 
Mandela, ambaye alikuwa rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini mwaka 1994, alikimbizwa hospitali moja ya Pretoria mapema Juni 8 kufuatia maambukizi kwenye mapafu.
Ilidaiwa jana kwamba Mandela hajitingishi na familia yake sasa inajadili uwezekano wa kusitisha matibabu.

Amekuwa hospitalini kwa wiki mbili akipambana na maambukizi hayo, lakini taarifa zilizopita zimeashiria kwamba afya ya Mandela inaimarika.

Kwa mujibu wa vyanzo vipya, ufanyaji kazi wa ini na figo za Mandela umeshuka hadi asilimia 50 na hakufungua macho yake kwa siku kadhaa.
 
Pia alitakiwa kufanyiwa oparesheni mbili hivi karibuni, moja kutibu vidomda vya tumbo zilivyokuwa vikichuruzika damu na nyingine kuchomeka mpira mwilini mwake, imeripotiwa.
Taarifa hizi zinaashiria kwamba suala la Mandela ni kubwa kuliko inavyoripotiwa na mamlaka za Afrika Kusini.

Historia ya matatizo ya mapafu ya Mandela ilianzia tangu alipokuwa kwenye gereza la Kisiwa cha Robben karibu na Cape Town. Aliachiwa huru mwaka 1990 baada ya miaka 27 na akaendelea kutumikia nchi kama Rais kuanzia mwaka 1994 hadi 1999.

Kulazwa kwake hospitalini ni mara ya nne tangu Desemba, mwaka jana.

MAAJABU: MTOTO AZALIWA NA MAKALIO MATATU, MAMA YAKE ALIA AKIOMBA MSAADA

Maajabu  ya  uumbaji  yamemfanya  mama  mzazi  wa  Xiao Wei  ambaye  ni  mchina amwage  machozi  akiomba  msaada  wa  kunusuru  maisha  ya  mwanae   mwenye  umri  wa  miezi  7 aliyezaliwa  na  makalio matatu...
Kalio  la  tatu  lipo  kama  mkia  mfupi, wenye  urefu  wa   sentimita  8  ( 8 cm ), katikati  ya  makalio  mengine  mawili.
Akiongea   kwa  uchungu, mama  mzazi  wa  mtoto  huyo  amedai  kuwa  kwa  muda  mrefu  amekuwa  akiwaomba  madaktari  wafanye  upasuaji  wa  tako  hilo  lakini  wao  wamekuwa  wakimjibu   kuwa  hiyo  si  kazi  nyepesi  kama  anavyodhani....
"Tukilikata  litaota  tena, hivyo  hatutakiwi  kukurupuka  na  badala  yake  tutakiwa  kupata  muda  wa  kupitia  vitu  vingi  ukiwemo  mrija  wa  uti  wa  mgongo  ambapo  kalio  hilo  limejiegesha"...Alisema  daktari  mmoja  akimjibu  mama  huyo

SUGU AGOMA KUOMBA RADHI BAADA YA KUDAI KUWA WAZIRI MKUU NI MPUMBAVU

Juzi, mbunge  wa  mbeya  mjini  alitoa  tusi  zito  kwa  waziri  mkuu  wa  Tanzania  na  kudai  kuwa  Tanzania  haijawahi  kuwa  na  waziri  mkuu  mpumbuvu  kama  yeye...

Kupitia  account  yake  ya facebook, Sugu, ambaye  ni  mbunge  wa  mbeya  amezidi  kusisitiza  kuwa  hawezi  kuomba  msamaha wala  kuifuta  kauli  yake....

Hii   ni  post  yake  facebook:
"...naskia kuwa watu wanasema kwamba eti nimefuta kauli yangu kuhusu waziri mkuu na amri yake kwa polisi kupiga wananchi?!...

Sina sababu ya kufuta wala kuomba radhi, na nasimamia kauli yangu to the end...kwanza 'upumbavu' sio tusi,upumbavu kwa kiingereza ni stupidity-which is lack of knowledge and understanding...
So hata uwe na cheo gani kama ukishindwa kuwa na 'understanding' juu ya madhara ya kauli zako kwa taifa then u r 'stupid'...ambapo kwa kiswahili ndio 'mpumbavu'..."

KWA KAULI YA PINDA , TUTAPONA KWELI KWA HAWA JAMAAAA

Wanajeshi wakitoa kichapo  huku mwingine akiwa ameninginizwa kama swala na wawindaji porini..
Angalizo....picha hii nimeikuta mtandaoni inawezekana sio ya Tanzania......mmh mwenzangu nisije ninginizwa na mimi...

NGONO KINYUME NA MAUMBILE ZAONGEZEKA TANZANIA.

Taasisi ya Kupambana na Ukimwi Nchini (Tacaids) imesema tafiti mbalimbali zinaonyesha kuwa vitendo vya ngono kinyume na maumbile vinazidi kuongezeka.

Hayo yalisemwa jana na Dk. William Kafura, katika mkutano wa sita wa Chama cha Wabunge cha Kupambana na Ukimwi (Tapac).

Alisema hiyo inatokana na imani za kishirikina kwamba wakifanya vitendo hivyo watapata bahati kwa kupandishwa vyeo.

“Lazima tukubali tatizo lipo na tulitafutie suluhisho, utafiti upo umefanywa na Muhimbili, umefanywa na chuo kikuu cha Dar es Salaam, umefanywa na Tasisi ya Utafiti ya Ifakara,”alisema.

Alisema pia wafanyabiashara wanaamini kwa kufanya vitendo hivyo watajirika wakati wanawake wanaamini kuwa watazidi kupendwa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa TACAIDS, Dk. Fatuma Mrisho, alisema utafiti uliofanyika nchini unabainisha kuwa wanawake hawana uelewa wa kutosha juu ya kujikinga na maambukizi ya ukimwi.

Akizungumzia suala la kujikinga na ugonjwa wa Ukimwi Dk. Mrisho alisema kuwa wanaume wana uelewa mkubwa zaidi kuhusu ugonjwa huo kuliko wanawake.Hata hivyo, alisema kwa sasa ipo kazi kubwa ya kutoa elimu kwa wananchi na hivyo kuwataka wabunge na viongozi mbalimbali kutoa elimu juu ya kujikinga na gonjwa hatari la ukimwi.

Aidha Mrisho alisema kuwa kwa sasa Mkoa wa Njombe unaongoza kwa maambukizi ya Virusi vya ukimwi kwa asilimia 14.8 ambapo Unguja Kaskazini inamaambukizi madogo kwa asilimia 0.1.

Hata hivyo alisema kuwa kuna changamoto mbalimbali ambazo wanakumbana nazo ni pamoja na rasilimali za ukimwi kwa serikali, mashirika ya Dini na sekta binafsi kuwa pungufu kuliko mahitaji.

Alisema pamoja na kuwepo kwa changamoto lakini nia ni kufikia sifuri tatu ifikapo mwaka 2015 na hiyo hipo katika ulimwenguni, Afrika hapa hapa Tanzania.

NAFASI MPYA ZA KAZI LEO 24 JUNE 2013


CLICK HERE TO SEE ALL AVAILABLE VACANCIES

KIJIJI CHA NGONO CHAFICHULIWA HUKO SINZA,MAKAHABA WAAHIDI KUTOACHA KAZI HIYO



NI hakika ‘mtaa wa ngono’ umefumuliwa! Sakata hilo lilijiri saa tisa usiku, Ijumaa iliyopita, Barabara ya Shekilango, kuanzia Bamaga hadi Sinza Mori jijini Dar eneo ambalo makahaba wameligeuza chumbani
Kwa mujibu wa takwimu za kiserikali, eneo hilo
(kuanzia Bamaga hadi Sinza Mori) limekubuhu kwa wasichana kujiuza nyakati za usiku huku makao yao makuu yakiwa eneo la Afrika Sana hasa pembezoni mwa Corner Bar.

Mmoja wa viongozi wa serikali ya mtaa ya eneo hilo ambaye aliomba jina lake lisiandikwe , alisema:
 “Tumejitahidi sana kushirikiana na polisi ili kutokomeza ukahaba eneo hilo lakini wapi! Hawa mabinti ni wabishi, mbaya zaidi wamelifanya eneo hili kuwa la ngono.
“Watoto wetu wanapita usiku pale wanawaona wanavyofanya, wanatuharibia kizazi kijacho, kama wao wamejishindwa wasiwaambukize wengine.”
Siku ya tukio, saa tisa usiku,  askari wa ulinzi shirikishi walijipanga kwa ajili ya kuufumua mtaa huo huku wakiwa na tahadhari kufuatia habari za kiintelijensia kudai kuwa, makahaba hao walipanga kuua mtu punde watakapovamiwa.

Askari hao wakiwa kwenye doria ya kila usiku, waliwavamia makahaba hao eneo lenye majani madogo katikati ya Afrika Sana na Mapambano upande wa yadi ya Mwanamboka wakiwa na wateja wao wakifanya ngono hadharani.
Katika hali iliyoonesha makahaba wamejiimarisha kwa ulinzi siku hizi, wakati wa zoezi hilo, machangu hao sanjari na vibaka  wanaowaunga mkono wakisemekana ni ‘walinzi’ wao, waliokota mawe na kuwarushia askari hao hali iliyozua tafrani zaidi.
Ndipo piga nikupige ilipozuka ambapo askari walionesha umahiri wao wa kupambana na wahalifu kwa kuwadhibiti kwa vichapo vya hapa na pale na kufanikiwa kuwaweka wengi chini ya ulinzi.
Kuona hivyo, baadhi ya makahaba na wateja wao walifanikiwa kuwachoropoka askari bila nguo na kutokomea gizani hivyo kulifanya eneo hilo kuwa jeupe.
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, baadhi ya makahaba waliokimbia walijikuta wakiacha kwenye majani nguo zao za ndani na kuzua maswali kwamba ni kwa nini hawakuwa wamezivaa!


“Jamani hizi si nguo zao za ndani? Ina maana wakiwa kazini hawavai siyo? Wanakuwa tayaritayari kwa kazi? Jamani!” alisema kwa mshangao mkubwa mmoja wa askari hao.

Licha ya kuwa chini ya ulinzi mkali, baadhi ya makahaba walionaswa walikuwa wakiwalalamikia askari hao kwamba wanawafuatafuata wakati kila mtu siku hizi anaangalia atakulaje!

“Mnatuonea bure, nyie mnakula kivyenu na sisi mngetuacha tule kivyetu, hao watoto wenu mnaosema tunawaharibu usiku huu wao wanatokea wapi na wanakwenda wapi?” alisikika akisema kahaba mmoja aliyekuwa mtata kuwekwa chini ya ulinzi.


Mwingine akadakia: "Kama mnataka tuwape uroda si mseme, mnatukamata kila siku kwani tunawatibulia nini majumbani mwenu? Lini tumekuja kuwaghasi wakati mmelala na wake zenu?”

Uchunguzi wa kawaida ulibaini kuwa muda rasmi wa
makahaba hao kuwasili eneo la Corner Bar ili kuanza ‘kazi’ ni saa mbili usiku japokuwa wapo wanaoripoti mapema na kufanya biashara hiyo kwa wizi kulingana na wateja wenye ‘kiu’ nyakati hizo.

Licha ya kuwa chini ya ulinzi, makahaba hao waliahidi endapo watapelekwa polisi na kutoka watarejea eneo hilo kujiuza kwani ndiyo ajira inayowafanya waendelee kuishi katika Jiji la Dar es Salaam, kusomesha watoto vijijini kwao na kuwasaidia wazazi wao mahitaji mbalimbali.

“Hata kama mtatupeleka polisi, tutarudi tu hapa, sisi tunasomesha watoto, tunasaidia wazazi wetu vijijini, pia tunaishi Dar kwa sababu ya kipato hiki cha kuuza miili yetu, acheni hizo,” mmoja wa makahaba hao alisema bila kumung’unya maneno.

Saturday, June 22, 2013

NCHI IMEVAMIWA


Stori:Mwandishi wetu

Taifa linapepesuka, linayumbishwa na adui asiyeonekana, anayesababisha kizaazaa kisha yeye kukaa pembeni akiwaacha Watanzania wao kwa wao wakinyoosheana vidole kutuhumiana kuhusika.


IGP Saidi Mwema
Adui huyo ameivamia Tanzania na ndiye inafaa awe mtuhumiwa nambari moja wa bomu lililolipuliwa Soweto, Arusha, katika mkutano wa hadhara wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wakati wa ufungaji wa kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani, Jumamosi ya wiki iliyopita.

Jinsi nchi…

Stori:Mwandishi wetu
Taifa linapepesuka, linayumbishwa na adui asiyeonekana, anayesababisha kizaazaa kisha yeye kukaa pembeni akiwaacha Watanzania wao kwa wao wakinyoosheana vidole kutuhumiana kuhusika.


IGP Saidi Mwema
Adui huyo ameivamia Tanzania na ndiye inafaa awe mtuhumiwa nambari moja wa bomu lililolipuliwa Soweto, Arusha, katika mkutano wa hadhara wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wakati wa ufungaji wa kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani, Jumamosi ya wiki iliyopita.
Jinsi nchi inavyopepesuka kwa sasa, ni ishara ya mafanikio ya adui huyo ambaye lengo la uvamizi wake na harakati zake za kutibua amani ya nchi kuona Watanzania wao kwa wao wanashikana mashati, badala ya kuzingatia masuala muhimu yanayohitaji mshikamano wa kitaifa.

Namna Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chadema, vinavyotuhumiana kuhusika na ulipuaji wa bomu hilo ambalo imeshaelezwa kusababisha vifo vya watu wanne, ni ushindi kwa adui huyo mwenye shabaha ya kutenda tukio kiuchochezi na kuzigeuza fikra za watu kutuhumu wasiohusika.
“Tuache kufikiria haya mambo kisiasa, tuyatafakari katika sura yenye hoja mahususi, utaona kwamba siyo CCM wala Chadema wanaohusika na ulipuaji wa bomu Arusha,” alisema Job Ngarano, mkazi wa Arusha, aliyejitambulisha kuwa msomi wa shahada ya kwanza ya Diplomasia na Uhusiano wa Kimataifa.

NANI KALIPUA BOMU?
Ripoti ya uchunguzi wa gazeti hili, iliyokusanya taarifa za eneo la tukio na mambo mengine ya pembeni kuhusiana na bomu la Arusha, imebaini kuwa siyo Chadema wala CCM, mwenye uhakika na tuhuma dhidi ya mwenzake.
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alishatoa kauli yenye kudai kuwa anao mkanda wa video unaoonesha namna tukio lilivyotendeka na akasisitiza kuwa mlipuaji ni askari polisi aliyekuwa amevalia sare za kikosi cha kutuliza ghasia (FFU).
Upande mwingine, Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alirusha kombora kwamba Chadema ndiyo wahusika wa bomu hilo.
Tuhuma za Nape, zinaendana na dhana kuwa Chadema walijilipua wenyewe kwa lengo la kutafuta huruma ya wapiga kura ili wakichague chenyewe katika uchaguzi mdogo wa udiwani, uliofanyika Juni 16, mwaka huu.
Uchunguzi unapingana na dhana hiyo kwa hoja kwamba Chadema kilikuwa na nafasi kubwa ya kuibuka mshindi katika uchaguzi huo bila hata kusaka huruma ya wapiga kura, kutokana na jinsi kilivyokuwa kinakubalika.
 Macho yanayoona mbali aliyonayo Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia, January Makamba, ndiyo yaliyomuongoza pale alipowataka wanasiasa kukaa kimya na kuacha mamlaka zinazohusika kufanya kazi yake.
“Natoa rambirambi zangu na kulaani. Naamini katika mambo haya ni vyema wanasiasa tukafunga midomo yetu hadi ukweli ujulikane,” January, aliandika ujumbe huo kuhusiana na tukio la Arusha, kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter.
Wakati January akiwataka watu kutulia na kuacha kusemasema, Noel Kyaro ambaye ni mwongozaji wa watalii (tour guider) Arusha, alisema kuwa kama Chadema na CCM, watakaa pamoja na kuacha kutuhumiana, wanaweza kumpata kwa urahisi mhusika wa mabomu.
“Kuna changamoto nzito hapa, inabidi pia tuangalie uhusiano wa nchi yetu na mataifa mengine. Tanzania inaonewa wivu sana kutokana na uimara wake wa vivutio vya utalii,” alisema Kyaro na kuongeza:
“Hivi karibuni Rais wa Rwanda, Paul Kagame, alitoa kauli chafu sana dhidi ya Rais Jakaya Kikwete. Sasa haishindikani Rwanda kufanya huo ugaidi kwa sababu wameonesha waziwazi kupitia kwa rais wao kuwa hawatupendi.”
Rwanda inapotajwa, moja kwa moja kikundi cha waasi cha chini DRC cha M23, kinaingizwa katika skendo hiyo kwa sababu haijapita muda mrefu tangu nacho kiutangazie ulimwengu kuwa kitapambana na Tanzania.
Mei 5, mwaka huu (Jumapili), saa 4:30 asubuhi, bomu lilirushwa kwenye Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasiti, Arusha na kusababisha vifo vya watu watatu na majeruhi zaidi ya 40.
Siku moja kabla, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, alitoa tamko la serikali kuwa Tanzania lazima ipeleke majeshi DRC kupigania amani na haitishwi na vitisho vya waasi wa M23.
Kauli ya Membe, ilifuatia waraka wa M23 ambao waliutuma nchini, wakieleza kuwa ni ujumbe kutoka kwa Mungu, wakiionya Tanzania kutopeleka majeshi DRC, vinginevyo itakiona cha moto.
Baada ya kauli hiyo ya Membe, M23 walihamishia mashambulizi yao kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter, wakiitishia Tanzania.
Baadhi ya ‘twiti’ za M23, siku moja kabla ya bomu la kanisani Arusha, mojawapo ilisema: “Membe usiwadanganye watu, mnakuja DRC kuweka petroli kwenye moto, hamji kutafuta amani.”
Twiti nyingine inasomeka: “Hatutishwi na scout (askari chipukizi), Tanzania leteni majeshi yenu halafu mtaona.”
Hatari kubwa zaidi ni kwamba M23, walitishia kuingia nchini na kufanya mashambulizi, wakitamba wana uwezo mkubwa sana wa kufanya hivyo.
Kutokana na hatari hiyo, Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, ‘alitwiti’, akionya kwamba M23 walikuwa ‘wanatwiti’ wakiwa Dar es Salaam, hivyo ni dhahiri kuwa kundi hilo lilikuwa limeshaingia nchini.
Kauli hiyo ya Zitto, ilikuwa inaweka wazi namna taifa letu lilivyo hatarini, kwani maadui wanaweza kuingia nchini na kupanga mashambulizi dhidi yetu bila sisi wenyewe kujua.
“Kabla ya kurushiana makombora na kutuhumiana bila ushahidi ni bora tukaangalia uhusiano wa nchi yetu na mataifa mengine. Nchi majirani zetu hazitupendi, wanatuonea wivu, hawashindwi kupanga njama za kutuchonganisha sisi kwa sisi,” alisema Matilda Urio wa Kijenge Chini, Arusha na kuongeza:
“Hatutamjua adui, hatutapata ufumbuzi wa haya matatizo mpaka tutakapoacha kutuhumiana sisi kwa sisi. Chadema waache kuwalaumu CCM kuwa wanahusika, vilevile CCM wasiituhumu Chadema. Tuhuma hizo zinapoteza uelekeo wa kumjua adui.”
Mtumiaji wa Twitter mwenye akaunti yenye jina @iAlen, aliandika ujumbe wake kwa Lugha ya Kiingereza; This Chadema CCM blame game isn’t going to help anyone. People have lost their lives here folks (Huu mchezo wa kulaumiana CCM na Chadema hautamsaidia yeyote. Watu wamepoteza maisha).

KWA NINI
NI WATU WA NJE?
Kwa mujibu wa watu waliozungumza na gazeti hili ambao wanalitazama tukio la Arusha kwa jicho la mbali zaidi ni kwamba sura ya nchi kiutalii ndiyo inayosababisha jiji hilo likumbwe na misukosuko ya milipuko ya mabomu.
“Unalengwa utalii wetu, majirani wanataka Tanzania ionekane ina machafuko ili watalii wawe wanaenda kwenye nchi zao,” alisema Rachel Komba ambaye ni Meneja Uhusiano wa Taasisi Isiyo ya Kiserikali ya OTSG.
Rachel alisema: “Jinsi tunavyogombana ni sawa na mgonjwa wa kifafa halafu arogwe ugonjwa wa malaria ya kichwa, akianguka, kila mtu atajua kifafa ndicho kimemfanya aanguke.
“Tanzania kuna udini, kuna mvutano mkubwa wa kisiasa kati ya CCM na Chadema. Bomu likitupwa kanisani, haraka sana Wakristo wanawatuhumu Waislamu, vilevile bomu likitupwa kwenye mkutano wa Chadema, wafuasi wa Chadema watawatuhumu CCM.
“Tuliona jinsi bomu la kanisani Arusha lilivyoleta sintofahamu, vilevile hili la mkutano wa Chadema, linavyowagombanisha CCM na Chadema. Kuna adui wa nje anayewachonganisha Watanzania.
“Anafanya makusudi kwa kutumia udhaifu wetu. Anajua tuna udini, anapiga upande mmoja halafu Waislamu na Wakristo wanakamatana, amepiga mkutano wa Chadema, tunaona hali ilivyo.”
Rachel aliongeza: “Inakuwa vigumu kuwajua hawa maadui kwa sababu wanatupiga kwa kutuchonganisha. Kama wangelipua reli au bandari, moja kwa moja tungejua ni wavamizi kutoka nje. Tatizo wanapiga makanisa, misikiti na mikutano ya vyama vya siasa ndiyo maana inatuchukua wepesi kutuhumiana sisi kwa sisi.”
Elibariki Munishi wa Unga Limited, Arusha, alikumbusha tukio la bomu ambalo alipigwa Katibu wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata), Mkoa wa Arusha, Sheikh Abdulkarim Jonjo, akiwa nyumbani kwake na kumjeruhi vibaya.
“Inawezekana kabisa, watu waliomrushia bomu Sheikh Abdulkarim ndiyo haohao waliolishambulia kanisa na ni haohao waliorusha kwenye mkutano wa Chadema. Inabidi tuwe makini sana.
“Tukidanganyika, tunaweza kupigana sisi kwa sisi. Hakuna Muislamu Mtanzania anayeweza kumdhuru Mkristo, vilevile Mkristo hawezi kumdhuru Muislamu kutokana na asili yetu na tunavyojijua,” Elibariki.

LENGO LA NINI?
John Sebless wa Ngarenaro, alisema kuwa lengo la adui ni kuvuruga sura ya utalii wa nchi, hivyo kuyafaidisha mataifa ya kigeni.
“Haya machafuko malengo ya wachafuaji ni kuifanya nchi yetu ionekane siyo salama kwa kupokea watalii. Halafu jiulize kwa nini Arusha ambayo ndiyo mji ambao unaoongoza kwa utalii nchini?
“Tunatakiwa kuacha kulumbana na kusimamia utaifa wetu. Adui kutoka nje anatugawa, tuache kuzingatia mambo ya msingi na matokeo yake tubaki tunalumbana wenyewe. CCM hakiwezi kulipua bomu Chadema kwa sababu viongozi wake wana akili na wanajua kufanya hivyo, wao watakuwa watuhumiwa nambari moja.
“Vilevile haiingii akilini Chadema kujilipua wenyewe. Tuache kulumbana, Wakristo kwa Waislamu, Chadema, CCM na vyama vingine vyote, tunatakiwa tutambue kwamba tumevamiwa kisha tuanze kupambana na adui huyo wa nje anayetaka kuvuruga sifa njema ya nchi yetu kiutalii,” alisema Sebless.
Hata Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, mapema wiki hii, alithubutu kulinyooshea kidole jeshi la polisi, akalitaka kuacha kutumia mabomu kutuliza machafuko, akafafanua kwamba kufanya hivyo kunazidi kuuweka utalii wa nchi katika hali mbaya.

KUTOKA KWA MHARIRI
Tunapaswa kulinda amani yetu ambayo inavutia watalii na wawekezaji wengi kuja nchini. Tuamke sasa na kupambana na adui anayetaka kuivuruga nchi yetu. Bila umoja na mshikamano hatutashinda. Tusikubali kuchochewa kupigana sisi kwa sisi. MHARIRI.

ZIARA YA KAKOBE CANADA NI MAAJABU




ULE mpango wa Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship, Zachary Kakobe kwenda kuhubiri jijini Toronto nchini Canada umekamilika, juzi alianza kuonesha maajabu kwa Watasha hao.

Askofu Kakobe
Katika mtandao wake wa Facebook, Askofu Kakobe amethibitisha kufanya safari hiyo akisema amefikia Marriot Hotel yenye ubora wa hali ya juu.

Amesema mkutano wake wa kihistoria unafanyika kwa siku tatu, Juni 20 hadi 23 mwaka huu katika Kiwanja cha Rexall Centre ambacho huchukua watu 14,000 kwenye matamasha.…


ULE mpango wa Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship, Zachary Kakobe kwenda kuhubiri jijini Toronto nchini Canada umekamilika, juzi alianza kuonesha maajabu kwa Watasha hao.

Askofu Kakobe
Katika mtandao wake wa Facebook, Askofu Kakobe amethibitisha kufanya safari hiyo akisema amefikia Marriot Hotel yenye ubora wa hali ya juu.
Amesema mkutano wake wa kihistoria unafanyika kwa siku tatu, Juni 20 hadi 23 mwaka huu katika Kiwanja cha Rexall Centre ambacho huchukua watu 14,000 kwenye matamasha.

Martha Munizii
Uongozi wa hoteli aliyofikia umesema siku zote ambazo Askofu Kakobe atakuwepo, wateja wote watapunguziwa kodi ya kulala hotelini hapo.
Kitanda anacholalia ni cha bei mbaya na ameandaliwa chumba maalum (presidential room) .
Askofu Kakobe pia anasaidiwa kutoa Neno na mhubiri maarufu wa Marekani, Don Moen ambaye anatajwa kuwa ana uwezo mkubwa wa kuonesha ‘laivu’ miujiza ya Mungu.

Uwanja
Wenyeji wake Kakobe wamempanga nyota wa nyimbo za Injili nchini Marekani, Martha Munizzi ambaye amewahi kushinda Tuzo za Billboard ya Stellar Awards kutumbuiza kabla Kakobe hajaanza mkutano.
Kakobe pia ametengewa siku moja, Juni 24 mwaka huu kukutana na wanandoa na atakula nao chakula cha usiku kisha atawafanyia sala maalum ili ndoa zao zidumu.

Jijini Dar, waumini wa Kakobe katika kanisa hilo lililopo Barabara ya Sam Nujoma wamekuwa wakikesha kumuombea kiongozi wao huyo ili apambane na maovu hasa mashoga wanaotajwa kuwa wanapinga mkutano wake wa kiroho katika Jiji la Toronto.
Katika Jiji la Toronto,  mabango kuhusiana na ziara ya Askofu Kakobe yamewekwa katika mitaa mbalimbali na yameandikwa Toronto Miracle Healing Crusade hali inayofanya kufika kwake huko kuwa na msisimko wa kipekee.

MCHUNGAJI AZAA NA HAUSIGELI


 
HAYA ni madai mazito! Mchungaji wa Kanisa la Kiroho la Kijito cha Utakaso au Healing Centre International lililopo Kimara-Mwisho, Dar, Thomas Mariki anadaiwa kuvuliwa kofia ya uchungaji baada ya kutuhumiwa kuzaa na ‘hausigeli’ wake, Sessy Mwambashi.

Akizungumza na Risasi Jumamosi kwa masikitiko, mke wa ndoa wa Mariki, Joyce Thomas Mariki alidai kuwa yeye na mchungaji huyo walioana mwaka 2004 katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Lungai Mwika, Moshi.

Alisema walijaliwa kupata watoto watatu lakini mmoja hakuwa bahati.…


HAYA ni madai mazito! Mchungaji wa Kanisa la Kiroho la Kijito cha Utakaso au Healing Centre International lililopo Kimara-Mwisho, Dar, Thomas Mariki anadaiwa kuvuliwa kofia ya uchungaji baada ya kutuhumiwa kuzaa na ‘hausigeli’ wake, Sessy Mwambashi.

Akizungumza na Risasi Jumamosi kwa masikitiko, mke wa ndoa wa Mariki, Joyce Thomas Mariki alidai kuwa yeye na mchungaji huyo walioana mwaka 2004 katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Lungai Mwika, Moshi.
Alisema walijaliwa kupata watoto watatu lakini mmoja hakuwa bahati.
MATESO YAANZA
Mwanamke huyo alidai amani katika ndoa yake ilipotea baada ya kujifungua mtoto wa pili (marehemu), mumewe alianza kumtuhumu kuwa alitoka nje ya ndoa na huyo mtoto hakuwa wake.
Aliendelea kudai kuwa, mtoto alipofikisha mwaka mmoja na miezi nane, walishauriana watafute hausigeli ili mama huyo afanye biashara ya kuwaongezea kipato.
Mama mchungaji alisema alimpata Sessy akiwa na miaka 15, mkazi wa Mbozi, Mkoa wa Mbeya.
Alisema yeye alianza biashara ya genge maeneo ya Kimara-Mwisho ambapo alikuwa akiwahi sokoni saa 11:00 alfajiri na kumwacha msichana huyo akiendelea na kazi za nyumbani.

VISA VYAANZA
Mama mchungaji aliendelea kudai: Baada ya miezi michache, mchungaji alibadilika tabia, alikuwa mkali, wakati mwingine alinifuata sokoni na kunipiga akinishutumu nina uhusiano na wanaume ndiyo maana nachelewa kurudi nyumbani.

MUMEWE AMFICHULIA SIRI
Akadai: “Siku moja mchungaji alinifichulia siri kuwa hausigeli wetu ni mjamzito na mimba ilikuwa yake hivyo akataka iwe siri kati yetu watatu.”
Mama Mariki alisema alikubaliana na mumewe ambapo alivumilia kwa kipindi kirefu lakini uzalendo ulimshinda baada ya msichana huyo kuwa na tabia ya kuwatesa watoto huku akisema aachwe kwani ni mjamzito.

MKE NAYE AFICHUA SIRI
Alisema kuwa baada ya kuona mumewe anamjali zaidi hausigeli kuliko yeye na watoto aliamua kwenda kutoa siri kwa wasimamizi wa ndoa, wakaitwa na kusuluhishwa ambapo waliamua kuwa msichana huyo arudishwe nyumbani kwao Mbeya jambo ambalo mtumishi huyo wa Mungu alilitekeleza, yeye mwenyewe alimrudisha msichana huyo kwao.

NDOA YATIBUKA
Mwanamke huyo alidai mumewe huyo aliporudi Dar, alianza visa akisema kuwa hausigeli alikuwa akimpa ‘mambo’ kuliko yeye ambaye amezeeka huku vitisho na vipigo vikiongezeka maradufu!
“Wasimamizi wa ndoa walituita kwa mara nyingine wakatusuluhisha lakini tulipofika nyumbani, mateso yakawa palepale ndipo wasimamizi waliponiambia nirudi kwa wazazi wangu kwani ni aibu kubwa kwa mtumishi wa Mungu kufanya vile,” alisema na kuongeza:
“Kweli nilirudi kwetu Moshi, wazazi wangu walimpigia simu mume wangu kuhusu matatizo yetu, lakini aliwajibu hanitaki na ataniletea talaka nyumbani.”
Alisema miezi mitatu baadaye, wasimamizi wa ndoa walimtaka arudi Dar kwa ajili ya kujua hatima ya ndoa yake.
Aliambatana na kaka yake hadi nyumbani kwa mumewe, cha ajabu walimkuta hausigeli akiwa na mtoto mchanga. Aliwazuia kuingia ndani akidai hawakuwa na mamlaka hayo.
Alisema kaka yake alimtaka hausigeli ampigie simu mchungaji amwambie shemeji yake anamhitaji, alifanya hivyo na mchungaji alifika lakini alipowaona alitoka nduki.

WAZEE WA KANISA WAINGILIA KATI
Aliendelea kudai kuwa ulifika wakati wazee wa kanisa waliingilia kati, wakamuweka mchungaji kikao na kumuuliza kulikoni hawamuoni mke nyumbani badala yake  msichana wa kazi tena akiwa na kichanga.
“Cha kushangaza mchungaji alipandwa na hasira, akawafanyia fujo wazee hao, alimpiga na kiti mzee mmoja ambaye alikuwa msaidizi wake anayeitwa Kisaka na kumjeruhi,” alisema mama mchungaji.
Alisema sakata la kujeruhiwa kwa Kisaka liliripotiwa katika Kituo cha Polisi Mbezi Kwayusuf na kufunguliwa jalada namba KMR/RB/2125/2013- SHAMBULIO LA KUDHURU MWILI.

AVULIWA UCHUNGAJI
Alisema katika kikao hicho, wazee hao walifikia uamuzi wa kumvua rasmi uchungaji kwa kumwandikia barua na kumkabidhi.
Mchungaji aliipokea barua hiyo lakini hadi sasa anaendelea na huduma kwani wapo waumini wachache walio upande wake huku wengine wakidaiwa kulikimbia kanisa hilo.

BOFYA HAPA UMSIKIE MCHUNGAJI
Baada ya kuzinyaka habari hizo, Juni 18, mwaka huu, mapaparazi wetu walimtafuta Mchungaji Mariki na kufanikiwa kumkuta nyumbani kwake Kimara-Mwisho ambapo alikuwa na haya ya kusema:
“Siwezi kuzungumzia lolote kuhusu habari alizosema mke wangu kwa sababu suala hili lipo kwenye Baraza la Usuluhishi wa Ndoa na lipo kwa maandishi, naweza kuwaambia kuwa kuna watu wanataka kunipindua, wanapanga hila na njama ili walichukue kanisa na ndiyo wanamtumia mke wangu lakini hawawezi, wameshindwa.
“Kuhusu kuzaa na hausigeli wangu ni kweli na mtoto ana miezi saba sasa, lakini hizo shutuma kwamba alikuwa na miaka 15 siyo kweli, alikuwa na miaka 17 na sasa ana miaka hiyohiyo.”

HAUSIGELI VIPI?
Risasi Jumamosi lilizungumza pia na hausigeli ambaye anaishi na mchungaji huyo kwa sasa kama mke ambapo alikuwa na haya ya kusema:
“Anayesema nilikuwa na miaka 15 ana ushahidi? Wanaoweza kujua umri wangu ni wazazi wangu na ukweli ni kwamba mwezi wa kumi mwaka huu natimiza miaka kumi na nane.
“Kuhusu kwamba nilikuja kufanya nini Dar, nilikuja kwa mume wangu mwenye ushahidi kuwa nilimfukukuza mke wake alipokuja nyumbani aniletee.”
Hata hivyo, Risasi Jumamosi linaendelea kufuatilia sakata hili ili kukujuza ni
ni hatima yake.

VIDEO YA WANAWAKE WAWILI WALIOVULIWA NGUO NA KUTEMBEZWA UCHI KWA MADAI YA WIZI


Kulikuwa na kizaazaa katika eneo la transami huko embakasi hapa jijini baada ya wanawake wawili kuvuliwa nguo na kusazwa uchi wa mnyama. 


Kisa na maana walikamatwa kwa madai ya walitaka kumuibia mwanamume mmoja, ambaye waliandamana naye nyumbani kwake jana usiku kwa starehe.

 Inadaiwa walimtilia dawa- bwana huyo akalaa fofofo...aliamkia purukushani nyumbani kwake.makinika na malimwengu haya .

HUYU NDIYE MWANAFUNZI WA UDSM ALIYEPIGWA RISASI YA TUMBO NA MAJAMBAZI USIKU WA KUAMKIA JANA

ALEX ROBERT AKIWA KATIKA POZI WAKATI WA MAPUMZIKO.




WANAFUNZI WA CHUO HICHO MWAKA WA NNE PAMOJA NA MKUU WA KITOVO CHA SHERIA PROFESA BONAVENTURE RUTINWA WAKIMWOMBEA MWENZAO AENDELEE KUWA SALAMA NA UPASUAJI HUO UFANYIKE VIZURI KATIKA HOSPITALI YA MUHIMBILI DAR ES SALAAM JUNI 21.


WANAFUNZI WA CHUO HICHO MWAKA WA NNE WAKIONESHA MSHIKAMANO WAKISUBIRI MWENZAO ALEX ROBERT AKIWA THIETA WAKATI WA OPERESHENI KATIKA HOSPITAL YA TAIFA MUHIMBILI  


ALEX ROBERT KULIA AKIWA NA RAFIKI ZAKE

SOMA ALICHOKIANDIKA ZITTO KABWE KUHUSU KAULI YA PINDA KURUHUSU POLISI KUPIGA WANANCHI


Baada ya mh.waziri mkuu mizengo pinda kutoa ruhurusa kwa polisi kupiga wananchi..Mh mbunge zitto kabwe nae atoa lake juu ya mh.waziri mkuu...Kupiitia tweet yake Zitto alisema "Viongozi wa kisiasa lazima wajue kuwka akiba ya maneno yao .kuropoka hovyo hovyo wakati kama huu wenye taharuki ni hatarii sana"..Aliongezea "Ni lazima viongozi wawajibishwe kwa maneno wanayotamka.Mh. Pinda anahamasisha ukiukwaji wa katiba na sheria Asipowajibishwa.!"

HIZI NDIZO TWEET ZA MH.ZITTO KABWE

Friday, June 21, 2013

KIGALI HIYOOO YAWADIA WAI NAFASI YAKO SASA


MABONDIA WANNE WA TANZANIA WAFUNGWA JELA MIAKA 15 BAADA YA KUNASWA NA MADAWA YA KULEVYA NCHINI MAURITIUS


Mabondia wanne wa Tanzania wafungwa miaka 15 jela nchini Mauritius kwa makosa ya kuingiza dawa za kulevya aina ya heroin.

Mabondia hao ni Case Ramadhani Fills, Nathanael Elia Charles, Ally Rajabu Msengwa na Petro Charles Mtagwa.

Wakati kesi hiyo ilipoanza kusikilizwa, wote walikiri makosa ya kuingiza mihadarati hiyo nchini Mauritius wakati walipokwenda kushiriki mashindano ya ndondi barani Afrika mwaka 2008.

Wakiwa mbele ya Jaji, waliiambia mahakama kuwa walilazimika kuingia katika biashara hiyo haramu kutokana na hali zao za maisha kuwa maskini.
 

"Tunaomba radhi kwa taifa la Mauritius", waliiambia mahakama.
 

"Tu watu maskini na tunategemewa na familia, watoto na wazee wetu wanaotugemea. "Kwa dawa hizi tungepata kiasi cha Pauni £4,000". walisema

Jaji Benjamin Marie Joseph alisema katika kutoa adhabu hiyo yote hayo ameyafikiria, kwani walitoa ushirikiano mzuri wakati wote wa uchunguzi wa kesi hiyo, kulikowezesha hata wafanyabiashara hiyo, raia wa Mauritius kukamatwa.

Wamekuwa mahabusu kwa siku 1,722, sawa na miaka miatano, hivyo watatumikia miaka kumi iliyobakia jela. Pia watatakiwa kulipa faini ya pauni £1,600 na gharama nyingine za uendeshaji wa kesi hiyo.

Kwa mujibu wa mwandishi wa habari wa BBC nchini Mauritius Yasine Mohabuth in Mauritius, Jaji aliwashutumu kwa kuukosea umma wa Mauritius kwa kuingiza dawa hizo za kulevya aina ya heroin.

Mabondia hao waliwasili Mauritius tarehe 10 Juni 2008 na kuweza kupita uwanja wa ndege bila kunaswa hadi walipokamatwa katika hoteli waliyofikia ya Quatre Bornes.

Kwa pamoja walimeza gram 4639.04 za heroin zikiwa katika vifuko 358 vijulikavyo kama pipi.

MWANAFUNZI APIGWA RISASI TUMBONI CHUO KIKUU CHA UDSM USIKU WA KUAMKIA LEO


Taarifa zilizotufikia katika chumba cha habari zinaeleza kuwa wanafunzi wanne wa chuo kikuu cha Dar es salaam maarufu kwa jina la Chuo cha Mlimani wamevamiwa na majambazi usiku wa kuamkia leo maeneo ya Yombo chuoni hapo.
Wanafunzi hao wanaosemekana kuwa ni wa mwaka wa nne na wa mwisho wa masomo walikuwa wanajisomea na kuandaa “Disertation” zao na kujikuta wakivamiwa na watu wanne na kuamuriwa watoe komputa zao na pochi za fedha. Kwa mujibu wa chanzo cha habari hii kutoka chuoni hapo, wanafunzi hao walikubali kuwapa komputa hizo na pochi za fedha,  na majambazi kuanza safari yao.
Baadaye wanafunzi hao wakawaomba wapate hata nakala (Soft Copy) ya vitu vyao, na ndipo mmoja wao akaamua kuwafuata na kukumbana na risasi tumboni. Mwanafunzi huyo baada ya kupigwa risasi alianguka chini na kugaagaa chini huku akikosa msaada wa kupelekwa Hospitalini.
Chanzo kimeendelea kusema kuwa wanafunzi wa Chuo hicho waliwasiliana na uongozi ili kupata gari ili wamkimbize mwenzao Hospitalini, lakini ilipita takribani nusu saa hakuna majibu na ndipo walipoamua kujikusanya na kuamua kuwafuata viongozi. Kwa sasa mwanafunzi huyo amekimbizwa Hospitalini kupata matibabu zaidi na mpaka sasa hakuna taarifa yoyote iliyotoka, ingawa FULLSHANGWE inajitahidi kufuatilia suala hilo ili kupta taarifa zaidi na picha za tukio hilo.
Tukio hilo limelaaniwa vikali na UMMA wa chuo kikuu cha Dar es salaam na kuitaka serikali kufuatiliwa na kudhibiti vitendo hivyo vya kikatili chuoni hapo. Endelea kufuatilia katika mtandao huu amboa umefunga safari ya kuelekea Chuo kikuu cha Mlimani kuangalia nini kinaendelea.
Mbali na tukio hilo, pia kumekuwepo na wizi wa hadharani katika shule za Chuo hicho ambapo hivi karibuni wanafunzi wamekuwa wakiporwa komputa zao mchana kweupe maeneo ya Mikocheni wakitoke shule kuu ya uandishi wa Habari na Mawasilinao ya Umma (SJMC).
Suala hizi limepoteza amani kwa wanafunzi na kuwafanya washindwe kusoma kwa amani.

KIONGOZI WA CHADEMA ALIYEUAWA KWA BOMU AZIKWA MAKABURI YA SOKONI 1 JIJINI ARUSHA


Baadhi ya viongozi wa CHADEMA wakimpumzisha Judith katika nyumba yake ya milele, Judith William Moshi alikuwa ni katibu wa CHADEMA kata ya Sokon 1 jijini Arusha na aliuawa katika shambulio la bomu lililotokea katika mkutano wa kufunga kampeni za uchaguzi mdogo wa madiwani, Soweto Arusha.
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman…
Baadhi ya viongozi wa CHADEMA wakimpumzisha Judith katika nyumba yake ya milele, Judith William Moshi alikuwa ni katibu wa CHADEMA kata ya Sokon 1 jijini Arusha na aliuawa katika shambulio la bomu lililotokea katika mkutano wa kufunga kampeni za uchaguzi mdogo wa madiwani, Soweto Arusha.
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na Mbunge wa Mbeya Mjini, Mhe. Joseph Mbilinyi (SUGU) wakiweka udongo katika kaburi la Marehemu Judith William Moshi aliyekuwa katibu wa CHADEMA kata ya Sokon 1 jijini Arusha,Judith aliuawa katika shambulio la bomu liliotokea katika mkutano wa kufunga kampeni za uchaguzi mdogo wa madiwani, Soweto Arusha.
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe akiweka shada la maua katika kaburi la Marehemu Judith William Moshi aliyekuwa katibu wa CHADEMA kata ya Sokon 1 jijini Arusha, Judith aliuawa katika shambulio la bomu liliotokea katika mkutano wa kufunga kampeni za uchaguzi mdogo wa madiwani, Soweto Arusha.
Baadhi ya Viongozi wa Chadema na wakazi wa Arusha wakiwa katika mazishi ya marehemu Judith William Moshi aliyekuwa kiongozi wa CHADEMA kata ya Sokon 1, Judith aliuawa katika shambulio la bomu lililotokea katika mkutano wa kufunga kampeni za uchaguzi mdogo wa madiwani, Soweto Arusha.
Baadhi ya Wabunge ,Viongozi wa Chadema na wakazi wa Arusha wakiwa katika ibada ya mazishi ya marehemu Judith William Moshi aliyekuwa kiongozi wa CHADEMA kata ya Sokon 1 jijini Arusha, ibada ya mazishi ilifanyika katika kanisa la KKKT Usharika wa Sokoni 1 na kuzikwa katika makaburi ya Sokon 1. Judith aliuawa katika shambulio la bomu lililotokea katika mkutano wa kufunga kampeni za uchaguzi mdogo wa madiwani, Soweto Arusha.
Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema (kulia) na Mbunge Grace Kiwelu (viti maalumu Moshi) wakiwa mstari wa mbele na wabunge wengine wakiongoza kubeba jeneza la Marehemu Judith William Moshi aliyekuwa kiongozi wa CHADEMA kata ya Sokon 1 jijini Arusha, ibada ya mazishi ilifanyika katika kanisa la KKKT Usharika wa Sokoni 1, Judith aliuawa katika shambulio la bomu lililotokea katikamkutano wa kufunga kampeni za uchaguzi mdogo wa madiwani, Soweto Arusha

MABOMU ARUSHA; LEMA NUSURA ATUMBUKIE KWENYE MAFUTA YA KITIMOTO



KUFUATIA mapambano ya raia na Jeshi la Polisi mjini hapa, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema), Jumanne wiki hii alilazimika kukimbilia kwa wachoma nyama ya nguruwe karibu na eneo hilo ambapo alidaiwa kunusurika kutumbukia kwenye mafuta ya kiti moto.
Lema aliyenusurika kupigwa na bomu lililoharibu gari lake, alikuwa akijaribu kuwatuliza wananchi walioanza kukusanyika katika vikundi, wakijadili amri ya serikali ya kukataza miili ya watu waliofariki dunia katika shambulio la bomu, isiagwe kwenye Viwanja vya Soweto, mjini hapa.

Kabla ya kupigwa mabomu na kukimbilia kwa wachoma nyama ya nguruwe hao, Lema alikuwa akiwataka wananchi kuwa wavumilivu…

Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.
Na Mwandishi Wetu, ARUSHA
KUFUATIA mapambano ya raia na Jeshi la Polisi mjini hapa, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema), Jumanne wiki hii alilazimika kukimbilia kwa wachoma nyama ya nguruwe karibu na eneo hilo ambapo alidaiwa kunusurika kutumbukia kwenye mafuta ya kiti moto.

Lema aliyenusurika kupigwa na bomu lililoharibu gari lake, alikuwa akijaribu kuwatuliza wananchi walioanza kukusanyika katika vikundi, wakijadili amri ya serikali ya kukataza miili ya watu waliofariki dunia katika shambulio la bomu, isiagwe kwenye Viwanja vya Soweto, mjini hapa.
Kabla ya kupigwa mabomu na kukimbilia kwa wachoma nyama ya nguruwe hao, Lema alikuwa akiwataka wananchi kuwa wavumilivu kwani walikuwa wanawasiliana na serikali ya mkoa ili kupata kibali cha kuaga miili ya wapendwa wao.
Ghafla polisi walifika na kutangaza amri ya watu kutawanyika katika viwanja hivyo ili kuweka hali ya usalama ambapo walisema pasingekuwa na suala la kuaga miili ya watu hao katika eneo hilo. Zoezi hilo lilikwama baada ya mabomu kurindima kwa mara nyingine.