Monday, February 3, 2014

RAIS KIKWETE:MBOWE ANAKOSA UWEZO, JAMBO LA WENGI HALITAAMULIWA KWA NGUMI


Rais Kikwete: Mbowe anakosa uwezo, jambo la wengi halitaamuliwa kwa ngumi
Rais Jakaya Kikwete katika maadhimisho ya miaka 37 ya CCM alimwambia Mheshimiwa Mbowe kuwa nashanganzwa na kauli yake kwamba isipopatikana Serikali tatu atapambana kwa ngumi na mateke mpaka ipatikane.

“uliona wapi jambo la wengi likiamuliwa kwa ngumi?” aliendelea Kikwete kwa kusema “hakuna katiba ya nchi dunia iliyopatikana kwa kutumia ngumi na hata Mbowe akiamua kupigana sina hakika kama atamshinda John Komba au Mheshimiwa Mnyika kumpiga Mheshimiwa Missanga”.

Bunge la katiba ndilo litakalopitisha aina ya katiba tunayoitaka kwa niaba yetu na lina uwezo wa hata kuja na rasimu ya katika yao tofauti kabisa na ya sasa na ikawa halali.

Alimalizia kwa kusema “katiba mpya ikikwama tutaendelea na katiba ya sasa”

No comments:

Post a Comment