Sunday, February 23, 2014

Bunge la Ukraine kujadili Serikali mpya

 
Waziri Mkuu wa zamani wa Ukraine Yulia Tymoshenko ametaka upinzani kuendelea na maandamano
Maelfu ya waandamanaji wameendelea na maandamano katikati ya mji wa Kiev wakati Wabunge wakikutana kujadili kuhusu uundwaji wa Serikali mpya nchini Ukraine.
Hali katika viwanja vya uhuru imetulia, ikiwa ni siku moja baada ya Bunge kupiga kura kumuondoa Rais wa nchi hiyo, Viktor Yanukovych,hatua ambayo amedai kuwa ni mapinduzi huku mpaka sasa akiwa hajulikani alipo.
Mpinzani wake mkuu, Waziri mkuu wa zamani Yulia Tymoshenko, pia aliachiwa huru toka kifungoni , hatua hii imekuja baada ya maandamano dhidi ya Serikali ya nchi hiyo yaliyodumu kwa miezi kadhaa.
Yulia tymoshenko alihukumiwa kifungo cha miaka saba jela akishutumiwa kutumia vibaya madaraka yake, na kuachiwa kwake yalikua madai ya msingi ya waandamanaji nchini humo.
Wabunge wa upinzani wameiambia Televisheni ya taifa kuwa Bunge litajadili kuhusu uundwaji wa Baraza jipya la mawaziri na uteuzi wa Waziri mkuu.

No comments:

Post a Comment