Tuesday, June 18, 2013

A.Magharibi yapiku Somalia kwa uharamia

 
Uharamia wapungua Somalia kuliko Kanda ya Afrika Magharibi
Visa vya Uharamia pwani mwa Afrika Magharibi, vimekuwa juu zaidi ikilinganishwa na vile vinavyotokea nchini Somalia. Hii ni kwa mujibu wa shirika la kimataifa linalohusika na safari za baharini.
Shirika hilo linasema kuwa mabaharia 966 walishambuliwa kanda ya Afrika Magharibi mwaka 2012, ikilinganishwa na visa 851 vilivyorokea pwani ya Somalia.
Maharamia katika kanda hiyo zaidi huiba mafuta na mali ya wasafiri na hata wakati mwingine kutumia mabavu katika kutekeleza wizi.
Watano kati ya mateka 206 waliokamatwa mwaka jana katika kanda hiyo waliuawa.
Ripoti hiyo yenye mada athari za kimaisha kwa uharamia mwaka 2012, ilitolewa na shirika la kimataifa la safari za majini , shirika la Oceans Beyond Piracy pamoja na mashirika mengine.
Yanasema kuwa licha ya kuongezeka kwa visa vya uharamia katika ghuba ya kanda ya Afrika Magharibi nchini Guinea, eneo hilo halijaweza kupewa ulinzi kama pwani ya Somalia.
Maharamia hulenga kushambulia meli zenye kubeba mafuta na kuyauza kwa masoko yasiyo rasmi.
''Nchini Nigeria,pesa hutolewa kwa haraka katika biashara hiyo haramu ikilinganbishwa na Somalia,'' alisema afisaa mmoja anayehusiika na maswala ya usafari wa baharini.
"pia Somalia inaweza kuchukua miezi kadhaa kabla ya kuuza mafuta hayo lakini nchini Nigeria maharamia huchukua mafuta na pesa za wafanyakazi wa meli hizo. Inaweza kuchukua wiki kadhaa tu na waweze kupata pesa kwa haraka. ''
Aidha ripoti hiyo inasema kuwa kukabiliana na uharamia Afrika Magharibi na Somalia inahitaji ushirikiano kati ya juhudi zinazofanywa baharini na zile za ardhini kuweka usalama na kutoa nafasi za ajira kwa watu wanaoweza kufanya kazi ya uharamia.
Wakati huohuo, ripoti inasema kuwa visa vya uharamia vilishuka kwa 78% nchini Somalia mwaka jana ikilinganishwa na visa vilivyoripotiwa mmwaka jana 2011.

No comments:

Post a Comment