Tuesday, May 14, 2013

Reginald Mengi Kutoa Milioni Moja Kwa Atake Mwandikia Tweet Nzuri Kila Mwezi

Reginald Mengi '1m price for a nice tweet"

    Upo kwenye Twitter? Kama haupo fanya haraka

    ujiunge sababu kuna ulaji huko!! Mwenyekiti mtendaji wa makampuni ya
    IPP, Reginald Mengi amesema kuanzia mwezi huu, atakuwa akitoa shilingi milioni 1 kwa kila tweet itakayomfurashia.

    Not to fast
    though…… Sio tweet zile za ‘I’m having fun being single, #TeamSingle, tupa
    kuleee!

    Mengi anataka ulikune
    jicho lake kwa tweet yenye akili ambayo inaweza kuchangia kwa namna moja ama
    nyingine kupunguza umaskini uliokithiri nchini.

    “Umaskini umekuwa sugu. Kwa mwaka 1 anzia Mei ntatoa sh 1m
    kila mwezi kwa tweet nitakayochagua kuwa bora kushinda vita na umaskini,”
    ametweet leo.

    Ameongeza kuwa Tweet hiyo iende kwake, yaani mtu
    akiandika tweet afanye kummention ili aione.

No comments:

Post a Comment