Friday, May 10, 2013

Bomu Arusha: Waarabu ni innocent kwa mujibu wa ndugu zao


Taarifa za kuaminika toka kwa mwanasheria

Jambo hilli limefanyiwa fabrications kadhaa, kwa uchache tu;

Ndg. zetu hawa sio kweli kama ilivyoripotiwa kwamba:
1). Walifika jumamosi na kesho yake jumapili litakatokea tukio hilo,
2). Na si kweli eti kuwa baada ya tukio eti wakaanza kuondoka kupitia Nairobi road na hivyo kukamatwa wakiwa njiani wanaondoka kuelekea Kenya kupitia Namanga.

UKWELI ULIVYO KWA MAELEZO YA NDUGU ZAO:

WENZETU HAWA WASAUDI WAWILI WALIKUJA SIKU TATU KABLA YA TUKIO HUSIKA KWA MATEMBEZI YAO BINAFSI AMBAYO MARA KWA MARA HUWA WANAYAFANYA KUJA KUWATEMBELEA NDG. ZAO HAPA TZ ARUSHA KAMA MTU MWINGINE ANGEWEZA KUFANYA KIMATEMBEZI.

WALIPOFIKA WALIKUWA WAKILALA KATIKA HOTELI MOJA "B" (JINA NALISITIRI) ILIYOPO ENEO LA KITUO KIKUU CHA MABASI YAENDAYO MIKOANI HAPA ARUSHA AMBAYO INAMILIKIWA NA MCHAGGA MMOJA MKRISTO, SIKU YA TUKIO BAADA YA KUTOKEA, MMILIKI HUYO WA HOTELI HIYO ALIPIGA SIMU POLISI AKIELEZA KWAMBA HOTELINI KWAKE WAMEFIKIA WATEJA AMBAO ANA SHAKA NAO HIVYO POLISI WALIFIKA NA KUWAKAMATA HAO WAWILI HAPO HAPO HOTELINI NA KUWATAFUTA WENYEJI WAO WAWILI "X" NA "Y" NA WOTE KUKAMATWA NA KUPELEKWA KITUO KIKUU CHA POLISI HADI LEO.

My take:
Suala hili linageuzwageuzwa na watu humu ndani pamoja na mtaani ili mradi kuonekana tu waarabu hawa wanakosa. Ni kwanini watu tunashindwa kumuelewa hata kiongozi mkuu wa katoliki Tanzania ndg Kadinali Pengo ambae kwa maneno yake ameseme lisihusishwe na dini bali ni mgogoro wa ndani ya 'KANISA LENYEWE'

Kwanini hatuwabebeshi mzigo huu waswahili wenzetu ambao dalili zaonyesha wazi kuwa wametenda kosa hilo mfano Victor Ambrose?
Ni wazi bado tunaelement za chuki dhidi ya hawa waarabu na dini yao pia. Ni vyema tungojee mwisho wa uchunguzi polisi watasemaje kuliko kulijadili suala hili kwa kuegemea upande mmoja(bias).

No comments:

Post a Comment