Monday, October 21, 2013

Wahalifu wa DRC hawakupelekwa mahakamani

Wanajeshi wa serikali ya Congo
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Demokrasi ya Congo unasema unasikitika kuwa watu waliofanya ukatili katika mji wa Minova mwaka jana hawakufikishwa mahakamani.
Umoja wa Mataifa unasema una ushahidi wa kesi 135 za ubakaji pamoja na mauaji na wizi wa ngawira uliofanywa katika eneo la Minova mwezi Novemba mwaka jana.
Ulilishutumu jeshi la Congo kufanya uhalifu huo.
Inaarifiwa maafisa 12 wa jeshi la Congo walisimamishwa kazi kwa muda, lakini Umoja wa Mataifa unasema hakuna aliyefikishwa mahakamani.Wanajeshi wa serikali ya Congo

No comments:

Post a Comment