Tuesday, October 29, 2013

MWIGAMBA AANZA KUIANIKA CHADEMA..AWAONYA WANAO MWITA MSALITI


*Awaonya wanaomwita msaliti
*Dk. Slaa aibua mapya
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba, aliyesimamishwa uongozi asema atakichafua chama hicho kama ataendelea kuitwa msaliti.

Hatua hiyo, imekuja baada ya Mwigamba kukiri hadharani kusambaza waraka unaowatuhumu viongozi wa chama hicho katika mtandao wa Jamii Forum (JF), akitumia jina la Maskini Mkulima. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Arusha jana, Mwigamba aliwaonya viongozi wa Chadema wanaomwita msaliti. Alisema kama wanataka awe msaliti, yupo tayari kumwaga mambo yote hadharani, tena kwa ushahidi usio na shaka hata kidogo. 

Mwigamba, aliyejiunga na Chadema mwaka 2004, akiwa mwanachama wa kawaida, alisema akiwa makao makuu mjini Dar es Salaam kama mhasibu mkuu wa chama, ndipo alipoanza kutambua udhaifu mkubwa wa kiuongozi ndani ya chama chake.

“Niliondoka pale makao makuu kwa mizengwe, kiongozi mmoja mkubwa kabisa alinifukuza kazi kwa kunipigia simu, tena baada ya kuwasiliana na Mkurugenzi wa Fedha,Anthony Komu akiwa nje ya Dar es Salaam na kumwagiza anifukuze,” alisema Mwigamba.

Alisema kwa bahati mbaya, udhaifu huo umeshindwa kushughulikiwa na vikao rasmi vya chama, kwani yeyote anayejaribu kukosoa ama kuhoji iwe ndani ya vikao rasmi ama nje, hutangazwa kuwa ni msaliti.

Alisema kutokana na hali hiyo, ni wajumbe wachache ndani ya Chadema, hasa kwenye Kamati Kuu, ambao wanaweza kusimama kidete na kukosoa uongozi.

Aliwataja wajumbe hao, kuwa ni Dk. Kitila Mkumbo, Profesa Mwesiga Baregu, Mzee Shilungushela na marehemu Magadula Sherembi kabla hajafariki dunia.

Hata baada ya kuondolewa Aprili, mwaka jana, alirejea Arusha na hakuwahi kujitokeza kwenye vyombo vya habari ama mitandao kuzungumzia tatizo la viongozi na uongozi ndani ya chama.

“Matatizo yaliyomo ndani ya chama ambayo wanachama wa kawaida wanaokiamini chama na viongozi wake wangeyasikia, hakika wangeweza kukata tamaa.


“Nimefanya hivyo kwa mapenzi na kwa maslahi ya chama changu, sasa kama viongozi wenzangu wanataka niwe msaliti basi waniambie hata leo nimwage ambayo yote hadharani, tena kwa ushahidi usio na shaka hata kidogo.

MCHEZAJI WA MPIRA AUMBUKA BAADA YA MZIGO WAKE KUVIMBA AKIWA UWANJANI



Huyu  ni  staa  wa  mpira  aitwaye Zlatan Ibrahimovic  akiwa  katika  wakati  mgumu  baada  ya  mzigo  wake  kuvimba  akiwa  uwanjani…


Taarifa  zinaarifu  kuwa, mzigo  huo  ulivimba  baada  ya  mchezaji  mwenzake  kumkumbatia  kwa  nyuma..

UWEZI AMINI TANZANIA IMETEGWA TENA KATIKA MKUTANO WA EAC


NCHI za Tanzania na Burundi, kwa mara nyingine zimetengwa na wenzao wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), baada ya marais wa Kenya, Uganda na Rwanda kukutana mjini Kigali jana. Marais hao walitarajia kujadili namna ya kuimarisha Jumuiya ya Afrika Mashariki kupitia uimarishwaji wa miundombinu, uchumi, biashara pamoja na kuweka mikakati ya shirikisho la kisiasa.

Kitendo cha kuziacha Tanzania na Burundi ambazo ni wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, kinazidi kutia shaka mtangamano wa jumuiya hiyo.

Nchi hizo mbili zimeshaeleza kusikitishwa na muungano wa nchi hizo tatu, ambao zimesema unakwenda kinyume cha makubaliano na mkataba wa EAC.

Katika mkutano huo, marais hao, Paul Kagame wa Rwanda, Yoweri Museveni wa Uganda na Uhuru Kenyatta wa Kenya, pamoja na mambo mengine, walitarajia kusaini makubaliano ya kuanzisha kituo kimoja cha kukusanya ushuru kinachotarajia kurahisisha uchukuzi wa bidhaa kutoka Mombasa nchini Kenya, Uganda hadi Rwanda.

Aidha Sudan Kusini ilialikwa ikiidhinishwa kama mshirika katika kikao hicho.

Mkutano huo unakuja baada ya ule uliofanyika mjini Kampala, Uganda, Juni mwaka huu na mwingine uliofanyika Mombasa, Agosti, ambako viongozi hao watatu walipendekeza kupanuliwa kwa Bandari ya Mombasa, ili kuwezesha uharaka wa bidhaa kupitishwa katika kuhudumia kanda nzima.

Mkutano mwingine wa marais wa nchi 15 za Afrika, ikiwamo Tanzania, utafanyika leo nchini hapa, katika kongamano la siku nne ambalo linatarajiwa kuweka kipaumbele kwa uimarishwaji wa huduma za internet katika mataifa hayo.


Kwa mujibu ya waandaaji, zaidi ya wajumbe 1,500 watahudhuria mkutano huo, chini ya uenyeji wa Rais Paul Kagame na Dk. Hamadoun I. Toure, Katibu Mkuu wa Muungano wa Kimataifa wa Mawasiliano ya Kiteknolojia (ITU).
-Mtanzania

MGANGA AKUTWA NA KIGANJA CHA BINADAMU AKIMUUZIA MTEJA WAKE KWA MILIONI 100 HUKO MWANZA.


Mtu mmoja jijini Mwanza anadaiwa kukamatwa na kiganja cha mtu akiwa anajiandaa kumuuzia mteja kwa sh million 100.

Washukiwa walikamatwa  jana  karibia na uwanja wa ndege wa Mwanza  wakifanya  biashara  hiyo  haramu.... 
 Baada  ya  upekuzi  wa  kina, mteja  alikuwa  ana  milioni  100  na mganga alikutwa  na   kiganja cha  binadamu  ambacho kilikuwa  kibichi kikitoa damu.


Kiganja  hicho  kilikuwa  kimevishwa  tunguri  na nywele za binadamu.

Saturday, October 26, 2013

POLISI 56 WAFUKUZWA KAZI KWA MAKOSA YA KUOMBA NA KUPOKEA RUSHWA

 

JESHI la Polisi nchini limewafukuza kazi askari wake 56 katika kipindi cha mwaka mmoja, kutokana na makosa ya kuomba na kupokea rushwa pamoja na utovu wa nidhamu.
  
Kamishna msaidizi wa jeshi hilo, Patrick Byatao, alisema hayo jana alipokuwa akitoa ufafanuzi juu ya mambo mbalimbali hususan masuala ya nidhamu kwa askari wake katika warsha ya siku maalumu ya polisi iliyofanyika mjini Bukoba.
  
Alisema kuwa askari waliofukuzwa ni kutoka katika mikoa mbalimbali nchini ambao wamekutwa na tuhuma za utovu wa nidhamu ikiwemo kuomba rushwa kwa wananchi. Kwa kipindi cha mwaka 2012, waliwafukuza askari 35 na mwaka huu 21.
  
Kwa mujibu wa Byatao, wapo baadhi ya askari ambao wamekuwa wakitoa visingizio vya kuomba rushwa kwa sababu mishahara yao ni midogo na haitoshelezi mahitaji yao.
  
Alisema ni heri askari wa aina hiyo wakaacha jeshi, vinginevyo wataendelea kuchukuliwa hatua kama hawatafuata masharti ya kazi yao.

Akitoa mada juu ya kuimarisha maadili ndani ya jeshi hilo, Mrakibu Msaidizi wa Polisi kutoka makao makuu, Andrew Makungu, alisema wameanzisha mkakakati wa kudhibiti vitendo vya ukiukwaji maadili kwa askari wake ikiwemo rushwa.
  
Alitaja maeneo lengwa kuwa ni chumba cha kupokea taarifa za mashitaka, usalama barabarani na upelelezi wa makosa ya jinai. Bado juhudi zinaendelea ili kuboresha maeneo mengine.
  
Makungu alisema ubia wa kiutendaji wa jeshi hilo umekuwa ukiimarika kila siku baada ya sehemu kubwa ya jamii kutambua nafasi yao katika jukumu hilo. 
  
Alisema mambo hayo yanaonekana kutokana na wananchi kufanya ulinzi wa maeneo yao, kuchangia rasilimali kwa jeshi, kutoa taarifa sahihi za uhalifu, kujenga vituo vya polisi na kuanzisha vikundi vya ulinzi shirikishi. Hadi sasa viko vikundi 5,344 nchi nzima huku Mkoa wa Kagera ukiwa na 431.
  

Naye mgeni rasmi katika warsha hiyo, Meya wa Manispaa ya Bukoba, Anatory Amani, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali mstaafu Fabian Massawe, alisema kuwa Jeshi la Polisi limekuja na mkakati wa polisi jamii/ulinzi shirikishi unaoelekeza kuwapo kwa mashauriano, majadiliano ya kiutendaji yanayosisitiza uwepo wa maadili katika kazi, ikiwemo mapambano dhidi ya rushwa ndani ya jamii.

RAIS WA USWISI AIFUNDA TANZANIA JINSI YA KUPATA FEDHA ZA KIFISADI


Katika mahojiano maalumu na timu ya waandishi wa Mwananchi na The Citizen jana, Graf alisema kuwa Serikali ya Tanzania inapaswa kusaini mkataba wa kimataifa wa kubadilishana taarifa za masuala ya usimamizi wa fedha na kodi ili kuweza kujua ni kina nani wameweka fedha nchini kwake na kunufaika na kodi.

Graf, ambaye alikuwa katika ziara ya kikazi nchini, alisema kuwa hivi karibuni Serikali ya Uswisi ilisaini mkataba wa kimataifa wa kubadilishana taarifa kuhusu masuala ya fedha, ambao unajulikana kwa lugha ya Kiingereza kama `Convention on Mutual Administrative Assistance in Tax Matters’.

Alisema ikisaini mkataba huo ina maana itasaidiwa na Serikali ya Uswisi kupata fedha zilizofichwa na Watanzania.

“Serikali ya Tanzania inatakiwa kuweka mkakati wa kisheria utakaotengeneza mazingira ya kubadilishana taarifa za fedha na mataifa mengine. Kwa jambo hilo hata Serikali ya Uswisi inaweza kusaidia katika kupatikana kwa fedha zilizofichwa,” alisema Graf, ambaye anaongoza Serikali ya Uswisi kwani kwa kawaida Rais wa Bunge ndiye pia kiongozi wa taifa hilo.

Graf alisema kwa sasa itakuwa ngumu kwa Tanzania kupata fedha hizo kwani haijasaini mkataba wa kimataifa wa kubadilishana taarifa za fedha na mataifa mengine.

Alieleza pia katika miaka ya karibuni Serikali ya Uswisi imeandaa muswada wa sheria wa kubana fedha zilizopatikana kwa njia za kifisadi na kufichwa katika benki za Uswisi. Graf alisema sheria hiyo ikipita itaruhusu Serikali ya nchi hiyo kutaifisha fedha ambazo zimepatikana kwa njia haramu na kufichwa katika benki za huko.

Muswada huo unaoitwa kwa lugha ya Kiingereza `Freezing and Restitution of Assets of Politically Exposed Persons obtained by Unlawful Means Bill’ ulisomwa kwa mara ya kwanza kwenye Bunge la nchi hiyo mwezi Mei, mwaka huu.

Graf alisema faida nyingine ya Tanzania kusaini mkataba huo ni kuwa, itaweza kuwatoza kodi Watanzania hao walioweka fedha huko.

Alifafanua kuwa siyo fedha zote zinazowekwa kwenye benki za Uswisi kuwa ni haramu kwani kuna nyingine zimepatikana kihalali, lakini zinaweza kutozwa kodi.

“Tanzania inakosa kodi kutokana na fedha zilizohifadhiwa na Watanzania wenye akaunti kwenye benki za Uswisi,” aliongeza Graf, ambaye alichaguliwa kuwa Rais wa nchi hiyo Novemba 26, 2012 na kutakiwa kukaa madarakani kwa mwaka mmoja.

Graf alisema pia fedha za kodi zingeisaidia Tanzania kugharimia sekta mbalimbali za maendeleo.


Zito aitupia lawama Serikali

Naye Waziri Kivuli wa Fedha, Zitto Kabwe, ambaye yuko nchini Uswisi akifuatilia masuala ya utoroshaji fedha na kufichwa kwenye benki za huko, alisema kuwa wakati shinikizo la dunia sasa limeelekea kumaliza tatizo la ukwepaji kodi na utoroshaji wa fedha kutoka nchi za Afrika, lakini Serikali ya Tanzania inasuasua juu ya kupambana na jambo hilo.

Zitto alisema katika taarifa yake kwa vyombo vya habari kuwa moja ya njia ya Serikali za nchi maskini kupata taarifa za kampuni kubwa za kimataifa yanayokwepa kodi ni mfumo wa kupashana taarifa unaoitwa kwa lugha ya Kiingereza `automatic exchange of tax information’.

“Kutokana na shinikizo la nchi mbalimbali, hivi sasa nchi zinazoitwa `tax havens’ (nchi zinazohifadhi fedha kwa siri) fedha zimeanza kuweka sahihi makubaliano ya kutoa taarifa,” alisema Zitto, ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema).

Alisema kuwa Tanzania mpaka sasa haijaweka saini na Serikali haijatoa taarifa yoyote kwa umma juu ya sababu ya kutokufanya hivyo. “Ghana, Afrika Kusini na Nigeria nchi zinazotegemea sana rasilimali kama Tanzania zimeweka saini mkataba huu tayari,” aliongeza Zitto.Alisema asilimia 44 ya fedha za kigeni inazopata Serikali ya Tanzania zinatokana na mauzo ya madini nje. Kampuni za madini ndizo zinazoongoza kukwepa kodi.

Alisema Tanzania inapoteza jumla ya Dola 500 milioni (Sh783 milioni) na Dola 1.25 bilioni (Sh2 trilioni) kwa mwaka kutokana na kampuni kubwa za kimataifa kukwepa kodi.

“Hii ni sawa na kusema Tanzania inapoteza Dola2 milioni (Sh3.1 bilioni) kila siku kwa uporaji huu,” alisema Zitto.

Zitto alisema Serikali lazima ichukue hatua mara moja kuhakikisha Tanzania inaingia makubaliano ya kupashana taarifa za kikodi.

Jaji Werema agoma kujibu

Alipoulizwa juu ya Tanzania kutokusaini mikataba ya kimataifa ya kubadilishana taarifa za utoroshaji fedha na mambo au kodi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema alisema hawezi kujibu suala hilo.

“Muulize huyo aliyekwambia kuwa Tanzania haijasaini mikataba ya kubadilishana taarifa za utoroshaji fedha na masuala ya kodi. Naomba uniache nifanye kazi zangu,” alijibu Jaji Werema kwa mkato na kukata simu.

Mahojiano kamili na Rais wa Uswisi, soma Mwananchi Jumapili.

CCM WASUTANA DODOMA-WANYOOSHEANA VIDEOLE MATUMIZI YA PESA


*Mada ya rushwa yaibua malumbano Dodoma
*Wagombea wanyoosheana vidole matumizi ya fedha
BAADHI ya wanasiasa wanaotajwa kutaka kuwania ukuu wa dola mwaka 2015 kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM ), sasa wanadaiwa kusababisha malumbano makali kando ya semina ya mafunzo ya utendaji, yanayowahusisha Wenyeviti na Makatibu wa wilaya na mikoa wa chama hicho, iliyomalizika jana mjini Dodoma. 

RAI limedokezwa kuwa malumbano hayo yametokana na kitendo cha baadhi ya wanasiasa kuitumia semina hiyo kama njia ya ushawishi kwa kutoa rushwa ili kujijengea mazingira ya kuteuliwa kuwa wagombea urais katika uchaguzi mkuu wa 2015, hali iliyowaibua baadhi ya makada wa chama hicho ambao wamewanyooshea vidole vigogo hao.

Habari zilizolifikia RAI kutoka ndani ya semina hiyo iliyohitimishwa jana na Rais Jakaya Kikwete mjini Dodoma, zimeeleza kuwa baadhi ya wajumbe, waliwashambulia kwa maneno makali makada wenzao kuwa tamaa yao ya uongozi inayowasukuma kutumia fedha nyingi kutafuta uungwaji mkono, inakichafua chama.

Mmoja wa wajumbe wa semina hiyo aliyezungumza na gazeti hili (jina lake tunaliifadhi) alisema kuwa, yaliibuka malumbano makali wakati mmoja wa mawaziri vijana na kada wa CCM mwenye ushawishi kwa vijana alipokuwa akiwasilisha mada yake iliyohusu mwelekeo wa CCM na taswira ya wapiga kura katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015.

Inaelezwa kuwa katika mada hiyo, Naibu Waziri huyo kijana alieleza namna CCM kilivyoanza kupoteza mwelekeo na mvuto kwa wapiga kura kwa sababu ya uwepo wa makundi ya wanachama wake wanaotumia fedha kusaka uongozi.

Mtoa habari huyo alieleza kuwa kauli ya waziri huyo ambaye pia amekuwa akitajwa kuendesha mikakati ya chini kwa chini ya kutafuta uungwaji mkono kwa ajili ya kuwania urais 2015, iliibua malumbano kando ya ukumbi wa semina na baadhi ya wajumbe wakimnyooshea kidole kuwa hata yeye anatuhumiwa kutumia fedha katika harakati zake.

Kwa mujibu wa mtoa taarifa wetu, baadhi ya wajumbe walihoji alikopata uhalali wa kuzungumzia jambo hilo ili hali yeye mwenyewe ameutumia mkutano huo kugawa rushwa ya Sh 50,000 kwa makatibu 50 na wenyeviti 50 wa baadhi ya mikoa na wilaya.

Haikufahamika mara moja waziri huyo kijana alikotoa fedha hizo, lakini taarifa zaidi kutoka ndani ya semina hiyo zinaeleza kuwa kuna idadi kubwa ya wapambe wa watu waliokwishaonyesha nia ya kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao, ambao wamekuwa wakijipitisha kwa wajumbe wa mkutano huo na kuwagawia fedha.

RAI limetajiwa majina ya vigogo wawili wa CCM wenye asili ya Kanda ya Ziwa ambao wapambe wao wameonekana wakiwapatia bahasha za kaki baadhi ya wajumbe ambao baada ya kuzifungua wamekaririwa wakieleza kukuta fedha ndani.

Mmoja wa vigogo hao anatajwa kuwa ni waziri mwandamizi katika Serikali ya Rais Jakaya Kikwete, naye anamtumia mmoja wa wabunge wa mkoa wake kugawa kiasi cha Sh 200,000 kwa wajumbe aliokwishawafikia.

Inaelezwa kuwa mpambe huyo wa Waziri aliibua malalamiko kutoka kwa wajumbe wa Zanzibar, ambao hakuwapatia fedha na walipomhoji ni kwanini anawabagua katika mgawo huo, alijibu kuwa hakupewa majina yao lakini watu walio karibu naye wameeleza kuwa Wazanzibari hawapo kwenye mgao kwa sababu hawana nguvu ya ushawishi katika vikao vya uteuzi vya wagombea urais.

Mbali na waziri huyo, anatajwa pia aliyepata kuwa waziri katika moja ya wizara nyeti kabla ya kufanyika kwa mabadiliko ya baraza la mawaziri, ambayo yalimuacha pembeni kuwa naye ametuma wapambe wake katika semina hiyo ambao wamekuwa wakiwafikia wajumbe wa semina hiyo kwa kuwaomba wamuunge mkono katika nia yake ya kuwania urais mwaka 2015.

Wapambe hao wa mwanasiasa huyo kijana, ni wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) na pia walikuwa wabunge katika Bunge lililopita ambao wanawagawia wajumbe wanaowafikia bahasha zenye Sh 100,000 hadi Sh 150,000 ili kuhakikisha mgombea wao anaungwa mkono wakati utakapofika.


Jitihada za gazeti hili kumpata Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahiman Kinana kuzungumzia suala hilo, hazikufanikiwa baada ya simu yake ya kiganjani kuita muda mrefu bila kupokelewa.