Alfajiri ya leo, mtangazaji wa
ITV anayejulikana kwa jina la Ufoo Saro amejeruhiwa vibaya kwa
kupigwa risasi na mchumba wake ambaye baada ya tukio hilo naye
alijipiga risasi na kujiua. Akizungumza na mpekuzi wetu, kamanda
Wambura ambaye ni kamanda wa polisi wa mkoa wa kipolisi wa
kinondoni amesema tukio hilo limetokea majira ya alfajiri ya leo.
Kamanda wambura amedai kuwa mwanaume
aliyetenda mauaji hayo ni mchumba wake na alikuwa anafanya kazi
katika umoja wa mataifa ( UN ) huko sudani ila bado haijafahamika
kitengo alichokuwa akifanyia kazi. Kwa mujibu wa Kamanda Wambura,
inasemekana kulikua kuna ugomvi kati ya wawili hao ambapo walishindwa
kuelewana na ndipo walipoamua kwenda kwa mama mzazi wa Ufoo Saro(mama
mkwe) ili awasuluhishe Baada ya usuluhishi kuanza na
kuonekana kuwa tatizo liko kwa mwanaume, mwanaume huyo alimshutumu
mama mkwe wake kwamba amekuwa na mazoea ya kumtetea mwanae na
ndipo alipotoa bastola na kumpiga mama yake na Ufoo Saro risasi ya
kichwa na kumuua papo hapo....
Alipomuua mama huyo, mwanaume huyo
alimpiga Ufoo Saro risasi mbili , moja ya tumboni na nyingine ya mguuni
na kudhani kwamba amemuua kumbe amemjeruhi tu kisha kujipiga mwenyewe
risasi ya kidevuni na kufariki dunia hapo hapo.
Na Khatimu Naheka KIUNGO mshambuliaji wa Yanga, Mrisho
Ngassa ameikumbuka timu yake ya zamani ya Azam FC baada ya kuonekana
akiwa kwenye Uwanja wa Chamazi Complex nje ya jiji la Dar es Salaam. Ngassa, ambaye awali aliuzwa na Yanga
kwenda Azam FC kwa kitita cha pauni milioni 98, miaka mitatu iliyopita
kabla ya kurudi msimu huu, juzi alitua kwenye Uwanja wa Chamazi na
kushuhudia mechi ya Ligi Kuu Bara kati ya wenyeji na Mgambo Shooting. Ngassa aliyeondoka Azam FC kwa
mgogoro huku timu hiyo ikimpeleka Simba, alikuwa kivutio na wengi
walianza kuonyeshana alipokuwa amekaa jukwaani. Baada ya kufika uwanjani hapo, moja
kwa moja Ngassa alikwenda kukaa alipokuwa amekaa mshambuliaji wa Azam
FC, Gaudence Mwaikimba waliyewahi kukipiga pamoja Jangwani. Mara baada ya mechi hiyo, kiungo huyo
aliyerudi kwa kasi katika Klabu ya Yanga, kwa kuifungia bao moja mpaka
sasa, alisalimiana na baadhi ya wachezaji wa timu hiyo na kuondoka zake. Ngassa alipoulizwa sababu za kwenda uwanjani hapo alisema kwa ufupi: “Nimekuja kutembea tu.”
Tayari Ngassa yupo mjini Bukoba kwa ajili ya mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya wenyeji Kagera Sugar, kesho.
*Asema uamuzi wake haukushirikisha wizara nyingine
*Adai wadau walipaswa kupewa muda zaidi, aonya rushwa WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda amemuonya
Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli kwa mara nyingine tena kuacha tabia
ya kufanya uamuzi wa jambo lolote bila kushirikisha pande zinazohusika. Mbali ya karipio hilo, Waziri Mkuu
amewataka viongozi wengine wa Serikali, kuepuka mfumo usio shirikishi
katika uamuzi wao kwa kuwa unasababisha migogoro ndani ya jamii na
usumbufu kwa Serikali. Akizungumza na waandishi wa habari
jijini Dar es Salaam jana juu ya mgomo wa wasafirishaji wa mizigo na
abiria ulioanza Oktoba 5, mwaka huu, Pinda alisema Serikali imeamua
kurejesha kwa muda wa mwezi mmoja asilimia tano ya uzito wa mizigo
uliozidi kwenye mizani. Alisema hatua zilizochukuliwa na Dk.
Magufuli kufuta vifungu vilivyokuwa vikiruhusu asilimia tano zilifuata
sheria, lakini tatizo lililojitokeza ni kutoshirikisha pande
zinazohusika ili kushauriana na kupata uamuzi wa pamoja. Alisema mbali ya kutoshirikisha pande
hizo, uamuzi wa Dk. Magufuli ulikuwa wa ghafla kwa wasafirishaji
kitendo ambacho kimewapa wakati mgumu wa utekelezaji, kwa sababu
wafanyabiashara walikuwa wameingia mikataba na wateja wao. “Chimbuko la mgogoro huu, ni tangazo
la Dk. Magufuli alilotoa Oktoba mosi, mwaka huu la kuondoa ofa ya
asilimia ya uzito uliozidi, baada ya uamuzi huo wadau wa usafirishaji wa
malori na mabasi waliingia kwenye mgomo na kulalamikia hatua hiyo. “Kutokana na mgogoro huu,
nililazimika kukutana na Dk. Magufuli, baadhi ya mawaziri wa wizara
zenye uhusiano na masuala haya, wanasheria na wataalamu wa masuala ya
usafiri na uchumi. “Kilichoongeza mgogoro ni tafsiri ya
vifungu vya sheria na kwenye kanuni ya 7 (2) na 7(3) ambacho kinaeleza
wasafirishaji wa magari yenye uzito uliozidi, lakini upo ndani ya
asilimia tano ya uzito unaokubaliwa kisheria, wanatakiwa kupunguza
mzigo, kupinga na iwapo watashindwa kutekeleza, watatakiwa kulipia mara
nne ya tozo za kawaida. “Sasa suala la asilimia tano,
lilitokana na ombi la wadau wa usafirishaji kwa aliyekuwa waziri wa
Ujenzi miaka ya nyuma na halikuwa sheria kamili, ndio maana limeondolewa
baada ya kuonekana linatumiwa vibaya.
“Nakubaliana na Dk. Magufuli, wapo
baadhi ya wasafirishaji ni wakorofi na hawataki kufuata sheria…ndio
maana walifanya mazoea ingawa wapo wengine wazuri na hao nawapongeza
sana kutii sheria.
KOCHA Mkuu wa timu ya Yanga, Ernest
Brandts, amesema kuifunga Simba katika mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom
itakayochezwa Oktoba 20 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam, ni kazi rahisi. Brandts amewatoa hofu viongozi na mashabiki wa
Yanga, huku akitamba kupata ushindi dhidi ya mahasimu wao Simba. Akizungumza na RAI jana, Brandts
alisema Simba hawamtishi kwa kuwa ana kikosi bora ambacho kina kila
sababu ya kushinda mechi hiyo. Alisema amekuwa akiifuatilia Simba
mara nyingi inapocheza mechi na hakuna ushindani ambao umekuwa
ukionyeshwa na wachezaji wa timu hiyo, licha ya kupata ushindi katika
mechi zake. “Simba hawana kiwango kikubwa,
wanabebwa na mabao ambayo kwa bahati wamekuwa wakifunga, kikosi changu
mimi ni bora, wachezaji wangu wana nguvu za kutosha na uwezo zaidi
kuhakikisha tunashinda,” alisema.
Yanga tayari imewasili Bukoba kwa ajili ya mechi yao dhidi ya Kagera Sugar itakayochezwa kesho kwenye Uwanja wa Kaitaba
Mwenyekiti wa bukoba veterani Ernest
nyambo akimshukuru bw Ibra (kulia) alieandaa hafra hii jioni ya leo
kuagana na wachezaji wenzake wanaoelekea Arusha. Mashindano hayo
yatafanyika katika uwanja wa shekhe amri abedi,yatakutanisha timu kutoka
mikoa ya Dar-es-salaam,mwanza ,kigoma na wenyeji kitambi noma ya mjini
arusha,pia itakuwepo na michezo mingine kwa ajili ya kumuenzi baba wa
taifa la tanzania,Mwenyekiti ametumia nafasi hii kuwashukuru wadau
mbalimbali wa bukoba walishiriki kwa hali na mali na kufanikisha safari.kingmuddy akipata kitu roho inapenda
dada wa veterani
super mkude kwenye mstari
nyama choma kama kawaida
weka cha kutosha mwili siunauona huu
salumu bonge kama kawaida
veterani,mtensa, super mkude na jamco wakipata msosi
ni full makulaji
jamco akiwa na bw Ibrah alieandaa hafra hii,ongera ibra kwa uzalendo na mapenzi ya kweli kwa wenzako
hafra hii ilifanyika barabara ya uganda katika mgahawa wa Ibracadabraa
BUKOBA FLOW ZONE IKISHILIKIANA NA BUKOBA STARLINK TUNAWATAKIA SAFARI NJEMA NA MUNGU AWATANGULIE.